CCM SINGIDA KUIBUKA NA USHINDI WA KISHINDO
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais John Magufuli akizungumza na Wazee wa Mkoa wa Dodoma baada ya kuhitimisha kampeni zake za uchaguzi Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Alhaji Juma Hassan Kilimba akiwa katika moja ya mikutano ya kampeni Tarafa ya Makiungu mkoani hapa. Na Godwin Myovela, Singida MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani hapa Alhaji Juma Hassan Kilimba amesema kwa idadi ya kura zote zitakazopigwa kwa nafasi ya Udiwani, Ubunge na Rais, chama hicho kinatarajia kuibuka na ushindi wa asilimia 83.75 Akitoa ufafanuzi mbele ya vyombo vya habari jana, Kilimba alisema kwa kuanza na madiwani CCM ilisimamisha viti vyote 136, na kati ya hivyo viti 35 vilipita bila kupingwa hatua iliyokifanya chama hicho kubaki kikishindania viti 101 vya nafasi hiyo pekee. Kilimba alisema kwa upande wa Ubunge walifanikiwa kusimamisha wagombea wote 8 kwa idadi ya majimbo yaliyopo, na katika siku zote 60 za Kampeni, kuanzia Septemba walipoanza m...