Sunday, February 27, 2022

WAZAZI SINGIDA WAOMBWA KUWARUHUSU WATOTO KUJIUNGA NA SKAUTI

Kijana wa Skauti akitoa maelezo ya shughuli zinazofanywa na chama hicho  wakati wa maadhimisho ya  siku ya Mwanzilishi wa Skauti Duniani Baden Powells yaliyofanyika Shule ya Msingi ya Kindai iliyopo Manispaa ya Singida mwishoni mwa wiki..
Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Singida akitoa mafunzo ya jinsi ya kujiokoa na majanga mbalimbali katika maadhimisho hayo. Kushoto mwenye Skafu ni Afisa Vijana Mkoa wa Singida Frederick Ndahani.

Friday, February 25, 2022

MADIWANI MKALAMA WAPIGA STOP TABIA YA HAMISHA HAMISHA WALIMU WAKUU

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Asia Messos, akizungumza na Madiwani katika mkutano wa kawaida wa robo ya pili wa Februari 23 na 24 wa mwaka wa fedha wa 2021/ 2022 uliofanyika jana wilayani humo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo James Mkwega.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo James Mkwega akisisitiza jambo kwenye kikao hicho.
Wimbo wa Taifa ukiimbwa.
Madiwani wakiwa kwenye kikao hicho.

Madiwani wa Viti maalum wakiwa kwenye kikao hicho. Kutoka kushoto ni Miriamu Hussein kutoka Kata ya Iguguno Tarafa ya Kinyagiri, Florence Misahi kutoka Nkinto Tarafa ya Kurumi, Habiba Omari kutoka Kinampundu Tarafa ya Nduguti, Maria Kitalama kutoka  Nduguti Tarafa ya Nduguti na Zaina Kihara kutoka Kinyagiri Tarafa ya Kinyagiri.
Kikao kikiendelea.

Mkuu wa Wilaya hiyo Sophia Kizigo  akitoa onyo kwa watu wanaojiita waganga wakienyeji maarufu kama lambalamba kuacha mara moja kupiga ramli chonganishi na kuwa atakayebainika akiendelea kufanya vitendo hivyo atakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Katibu Tawala, Elizabeth Rwegasira, akichangia jambo kwenye kikao hicho..

Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.

 Katibu wa Vikao wa Halmashauru hiyo (CC), Daudi Makendi akiongoza kikao hicho.

Maswali yakiulizwa.
Diwani wa Viti Maalumu wa Kata ya Kinampundu, Habiba Omary akiuliza swali. 
Duncan Kifaluka wa Idara ya Afya akijibu maswali kwenye kikao hicho. 
Diwani wa Viti Maalum wa Mkalama mjini, Zainabu Kihara akiuliza swali.
Afisa Elimu Taaluma Sekondari Ernest Stephene, akijibu maswali kwenye kikao hicho.
Maswali yakiulizwa.
Maswali yakiulizwa.

Wednesday, February 23, 2022

SHIRIKA LA SPRF LAFANYA MDAHALO WA VIONGOZI WA VIJIJI WILAYANI IKUNGI KUANGALIA JINSI WANAVYOSHUGHULIKIA MATUKIO YA UKATILI WA KIJINSIA

Mratibu wa Mradi wa Shirika la Jiokoe na Umaskini yaani Stars of Poverty Rescue Foundation (SPRF)  Benard Maira, akizungumza na viongozi wa vijiji wilayani Ikungi mkoani Singida wakati wa mdahalo uliohusu haki za binadamu na namna ambavyo matukio ya ukatili wa kijinsia yanavyoshughulikiwa uliofanyika jana.
Mshauri wa Masuala ya Sheria wa shirika hilo na Mratibu Msaidizi wa mradi huo , Paul Kigeja akitoa mada kwenye mdahalo huo.

Tuesday, February 22, 2022

MADIWANI HALMASHAURI YA IRAMBA WAPITISHA RASIMU YA BAJETI ZAIDI YA SH.41.1 BILIONI

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida Innocent Msengi, akizungumza leo kwenye baraza la madiwani ambalo limepitisha rasimu ya bajeti ya zaidi ya Sh.41.1 Bilioni. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Michael Matomora na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Monica Samwel.
Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Michael Matomra akizungumza kwenye kikao hicho.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda akizungumza kwenye kikao hicho.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Iramba, Sango Songoma akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Madiwani wakiwa kwenyekikao hicho.
Mkuu wa Polisi wa Wilaya hiyo, Henry Makwasa, akijitambulisha kwenye kikao hicho baada kuhamia wilayani humo hivi karibuni.
Kikao kukiendelea.
Madiwani wakipitia makabrasha kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Afisa Elimu Msingi wa Wilaya hiyo Asia Matitu akijitambulisha kwenye kikao hicho baada ya kuhamia wilayani humo hivi karibuni akitokea mkoani Kigoma.
Taswira ya kikao hicho.

Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Daudi Madelu akizungumza kwenye kikao hicho.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iramba, Ephrahimu Kolimba akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Samuel Ashery akizungumza kwenye kikao hicho.
Wataalamu na wakuu wa  idara mbalimbali wa halmshauri hiyo wakiwa kwenye kikao hicho.
kikao kikiendelea


Na Dotto Mwaibale, Iramba


BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida limepitisha Rasimu ya Mpango wa Bajeti kwa Mwaka wa fedha 2022/2023.

Mpango huo umepitishwa katika kikao cha Baraza hilo kilichofanyika jana  katika ukumbi mdogo wa Halmashauri hiyo ambapo limepitisha Rasimu ya Bajeti yenye makisio yenye thamani ya Sh.41,163,999,997.24 Bilioni katika bajeti hiyo kutokana na vyanzo mbalimbali vya mapato.

 Akizungumza katika kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Michael Matomora alisema katika rasimu fedha kutoka mapato ya ndani Sh.5,384,746,533.24, ruzuku ya Serikali ni 25,407,823,634.10 huku wahisani ikiwa ni Sh10,371,426,830.

Alisema mwaka ujao wa fedha wa 2022/ 2023 halmashauri hiyo imekisia kutumia jumla ya 41,,163,996,997.24 kutokana na vyanzombalimbali.

Alisema kutoka mapato ya ndani wametenga Sh. 23,,526,000, matumizi ya kawaida Sh.2,143,494,086.24, miradi ya maendeleo,3,217,726,444 jumla ya mapato ya ndani ikiwa ni Sh.5,384,745,533.24.

Akielezea ruzuku ya Serikali alisema mishahara ni Sh.20,418,014,391, matumizi ya kawaida Sh. 1,000,776,000,miradi ya maendeleo Sh.3,989,033,243 jumla ikiwa ni Sh. 25,407,823,634.

Alitaja fedha kutoka kwa wahisani ni Sh.10,371,426,830 huku jumla yake ikiwa ni Sh. 41,163,996,997.24.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iramba Innocent Msengi aliwapongeza madiwani kwa kupitisha rasimu hiyo ambayo ameitaja kuwa ni ya kipekee na ya mfano.

"Nitumie nafasi hii kuwapongeza madiwani kwa kuandaa rasimu hii nzuri na ya kipekee hivyo nawaombeni mkaitekeleze katika kukusanya mapato ili tuwenze kusonga mbele" alisema Msengi.

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda alishukuru madiwani hao kwa kupitisha rasimu hiyo na akatumie nafasi hiyo kuwaomba madiwani hao kwenda kuhimiza wananchi wao kujitokeza kwa wingi wakati wa zoenzi ya sensa ya watu na makazi na anuani za makazi.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iramba, Ephrahimu Kolimba aliwaomba madiwani hao kwenda kuzisimamia vizuri fedha hizo na akataka kuwepo na mashindano ya kuwashindanisha kwa utendaji kazi wao na washindi wapatiwe zaidi pamoja na wananchi wao waliofanya kazi husika.

 

Sunday, February 20, 2022

SERIKALI YAAGIZA KUZIFUTA LESENI ZAIDI YA 500 ZA UTAFITI WA MADINI WILAYANI IRAMBA


Askari wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Iramba akimpigia saluti  Naibu Waziri wa Madini Dk. Lumomo Kiruswa (katikati) mara baada ya kuwasili viwanja vya Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kwenye  kongamano la wadau kujadili fursa na changamoto kwenye sekta ya madini lililoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda (wa kwanza kushoto) lililofanyika wilayani humo jana.
Naibu Waziri wa Madini Dk.Lemomo Kiruswa (wa pili kutoka kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mjiolojia Mbeleye David wakati alipotembelea Banda la Wizara ya Madini katika kongamano la wadau kujadili fursa na changamoto kwenye sekta ya madini lililoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda mkoani Singida jana. Wa kwanza kushoto ni mkuu wa wilaya hiyo, Suleiman Mwenda
Naibu Waziri wa Madini Dk.Lemomo Kiruswa (wa pili kutoka kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mjiolojia Agnetha Kato (kushoto) wakati alipotembelea Banda la Wizara ya Madini katika kongamano la wadau kujadili fursa na changamoto kwenye sekta ya madini lililoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda mkoani Singida juzi. Wa tatu kulia ni mkuu wa wilaya hiyo, Suleiman Mwenda
Kaimu Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Singida,Chone Malembo, akizungumzia masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya madini mkoani hapa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Javan Diamonds Project (JDP) inayojishughulisha na Utafiti wa Almasi, Javan Bidogo ambaye pia ni mmiliki wa mradi wa utafutaji wa Almasi katika Kijiji cha Mbelekese kilichopo wilaya humo akitoa taarifa ya mradi huo kwenye kongamano hilo.
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye kongamanohilo.
Kongamano likiendelea.
Maswali yakiulizwa kwenye kongamano hilo.
Mwenyekiti wa Wachimbaji wadogo wa Wilaya ya Iramba, Ramadhani Masoud akiuliza swali kwenye kongamano hilo.
Mchimbaji wa madini Yusuph Kityapi akichangia jambo kwenye kongamano hilo.
Mchimbaji wa madini Wilfred Shalua akiuliza swali kwenye kongamano hilo.
Mwenyekiti wa Wachimbaji Wilaya ya Ikungi, Seleman Dude akichangia jambo.M
Mjiolojia Charles Moe, kutoka Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) ambaye alimwakilisha Mtendaji Mkuu (CEO) wa Taasisi hiyo akichangia jambo kwenye kongamano hilo..
Vijana wa Sisi Tanzania Mkoa wa Singida wakiwa katika picha ya pamoja katika kongamano hilo.
Kongamano likiendelea.
Wadau wakiwa kwenye kongamano hilo.
Washiriki wakiwa kwenye kongamano hilo.
Mmojawa kada wa ChamaCha Mapinduzi (CCM) kupitia UVCCM Mkoa wa Dodoma, AsiaNdula (kushoto)  akiwandani ya kongamano hilo
Kongamano hilo likifanyiwa dua na Sheikh Omari Hassan.