Tuesday, October 25, 2022

RC SINGIDA : SUALA LA LISHE BORA KWA JAMII NI LA KUFA NA KUPONA

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, akizungumza na wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za Mkoa wa Singida wakati akitiliana saini mkataba na ikiwa ni agizo lililotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan alipokutana na wakuu wa mikoa jijini Dodoma ambapo  aliwaagiza kujipanga na kuongeza jitihada za kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za lishe bora.
Kaimu Afisa Lishe Mkoa wa Singida, Christoweru Barnabas akiwasilisha mpango huo.
Taswira ya kikao hicho cha kutiliana saini mkataba huo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, (kulia)na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda wakisaini mkataba huo. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Michael Matomora.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilayaya Singida DC, Ester Chaulaakisaini mkataba huo.

Viongoziwa Halmashauri ya Manispaa ya Singidawakisaini mkataba huo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, (kulia)na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, SophiaKizigo (kushoto) wakisaini mkataba huo. Wa pili kushoto mwenye ushungi ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Asia Mesos.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, (kulia)na Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Rahabu Mwagisa wakisaini mkataba huo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, (kulia)na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Jerry Muro wakisaini mkataba huo. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Justice Kijazi.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Jerry Muro akimshuhudia Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Justice Kijazi. akisaini mkataba huo. 

Picha ya pamoja baada yakusainiwa kwa mktaba huo.

Na Dotto Mwaibale, Singida

MKUU wa Mkoa Singida, Peter Serukamba, amesema suala la kushughulikia lishe bora kwa jamii ili kuzuia vifo vya wajawazito na watoto wanaowaleta hapa duniani ni la kufa na kupona ambapo  amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kulipa kipaumbele cha kwanza.

Serukamba alitoa agizo hilo jana wakati akitiliana saini mkataba na ma-DC na ma- DED ikiwa ni agizo lililotolewa na rais Samia Suluhu Hassan alipokutana na Wakuu wa Mikoa jijini Dodoma ambapo  aliwaagiza kujipanga na kuongeza jitihada za kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za lishe bora.

"Jambo la lishe na afua za lishe ni la kufa na kupona  tulipe kipaumbele cha kwanza,tukifanikiwa kuifanya jamii yetu iwe na lishe bora hasa kwa watoto kuanzia umri wa mwaka mmoja hadi mitano tutakuwa tumeweka jiwe msingi kwenye kizazi kijacho," alisema.

Serukamba alisema madhala ya watoto kukua bila lishe ni makubwa zaidi kwa jamii ni vile tu hayaonekani haraka hivyo ni jukumu kwa waganga Wakuu wa Wilaya na wataalamu wanaohusika na lishe kuongeza juhudi kutoa elimu kwa wananchi wafahamu mpangilio wa vyakula.

"Tunaweza tukawa tunajiuliza kwanini mitihani watu wanafeli sana tukadhani walimu hawafundishi lakini inaweza kuwa sababu mojawapo ni madhala ya kutopata lishe bora tena hasa kutoka kwa mama anapopata mimba," alisema.

Alisema rais Samia ndio 'champion' wa jambo hili hivyo njia bora ya kumshukru ni kuhakikisha tunamaliza tatizo la lishe ili kuzuia vifo vya akina mama wajawazito na watoto.

"Unaweza kukuta mtu nyumbani kwake ana kila kitu lakini anajua matunda ni kwa ajili ya kuuza tu sio kula,akikamua maziwa ni kuuza tu so kunywa, viongozi wa lishe wa Wilaya tusiishie kwenye makaratasi tu tuelimishe wananchi wajue mpangilio wa vyakula," alisema.

Mkuu wa Mkoa alisema Wakuu wa Wilaya wahakikishe wanasimamia suala la lishe ili Mkoa wa Singida utoke kwenye asilimia 87 na badala yake ufikie asilimia 100.

Serukamba alisema katika kipindi kifupi ambacho amekuwa katika Mkoa wa Singida amejifunza kuwa watendaji kwenye halmashauri wanajua kazi sana lakini tatizo lao usipowafuatilia hawafanyi sio kwa makusudi lakini ndio wameubwa hivyo wanasubiri hadi wasukumwe.

Akiwasilisha Mpango huo wa Afua za Lishe, Kaimu Afisa Lishe Mkoa wa Singida, Christoweru Barnabas alisema malengo ya mpango huo ni kuhakikisha wilaya zote zinasimamia ipasavyo utekelezaji wa  afua za lishe.

Akizungumzia malengo ya mkataba huo alisema Lengo kubwa ni kufanikisha suala la kuboresha hali ya lishe na kupunguza athari za utapiamlo katika wilaya,kuhakikisha kuwa Wilaya inasimamia ipasavyo utekelezaji wa  afua zalishe na kuchukua hatua madhubuti za kupunguza hali duni ya lishe katika  wilaya.

Alitaja malengo mengine kuwa ni kupanga, kutenga na kutoa fedha zote kwa ajili ya kutekeleza afua za lishe katika mipango ya halmashauri kwa mujibu wa miongozo na maelekezo ya Serikali sanjari na kutoa taarifa ya utekelezaji kila mwezi na kila robo mwaka kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa.

WATANZANIA WAASWA KUACHA KUHAMISHIA FARAGHA MTANDAONI

Mkurugenzi Msaidizi wa Usalama Mtandao wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Stephen Wangwe akizungumza katika mafunzo ya usalama mtandao kwa Wanafunzi wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia Zanzibar (KIST) leo Oktoba 25, 2022 . 

Mkurugenzi Msaidizi wa Usalama Mtandao wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Stephen Wangwe  akisisitiza jambo wakati wa mafunzo hayo.

Washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo.

Mafunzo yakiendelea..

Mafunzo yakitolewa. 

.................................................

Na Mwandishi wetu, WHMTH, Zanzibar.

 

WATANZANIA wameshauriwa kuacha tabia ya kuchapisha picha na video za faragha mtandaoni kwa kuwa ni kinyume na maadili ya kitanzania lakini pia mhusika anaweza kupata madhara ya kisaikolojia kutokana na udhalilishaji anaoweza kuupata mtandaoni. 

Mkurugenzi Msaidizi wa Usalama Mtandao wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Stephen Wangwe amezungumza hayo wakati akitoa mafunzo ya usalama mtandao kwa wanafunzi wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia Zanzibar (KIST) Oktoba 25, 2022 . 

Amesema kuwa, matukio ya picha na video za faragha mtandaoni yanazidi kuongezeka na asilimia kubwa zinawekwa bila idhini ya wahusika baada ya kusalitiwa na watu waliowaamini au baada ya kupoteza kifaa cha TEHAMA kilichohifadhi picha hizo. 

“Tunapaswa kufikiri kwanza kabla ya kupiga, kurekodi, kutuma  na kusambaza matendo ya faragha katika mtandao ili kulinda heshima binafsi na kulinda maadili ya kitanzania”, amezungumza Mhandisi Wangwe 

Ameongeza kuwa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, inazungumza wazi kuwa uchapishaji wa picha au video za faragha mtandaoni (ponography) ni kosa kisheria na adhabu yake ni faini si chini ya  milioni 20, au kifungo kisichopungua miaka saba  au vyote kwa pamoja. 

Mhandisi Wangwe ametoa rai kwa jamii kulinda faragha zao kwa kuhakikisha faragha inabaki kuwa faragha lakini pia kuhakikisha wanalinda vifaa vyao vya TEHAMA kwa kuweka password imara na ikiwezekana zaidi ya moja ili ikitokea kimepotea basi iwe ngumu mtu kufungua au kuona kilichopo ndani. 

Naye Mtaalamu wa Usalama Mtandao, Bw. Yusuph Kileo amesema kuwa udhalilishaji wa kimtandao unaongezeka katika jamii na madhara yake ni makubwa sana kwa wahusika ikiwa ni pamoja na msongo wa mawazo au hata vifo hutokea. 

“Ni kosa kisheria kudhalilisha watu kwa njia ya mtandao na faini yake si chini ya milioni tano, kifungo cha miaka mitatu au vyote kwa pamoja lakini pia ni muhimu jamii kuhakikisha hatutengenezi mazingira ya kufanyiwa udhalilishaji mtandaoni”, amesisitiza Kileo. 

Rashidi Salim Abdallah , mwanafunzi wa TEHAMA wa Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia Zanzibar amesema kupitia mada zilizotolewa na wataalamu wa usalama mtandao wamejifunza kujiuliza nini faida ya vitu wanavyoposti mtandaoni na kuepuka vishawishi vya kuwaamini na kuwatumia picha za faragha watu wanaokutana nao na kuanzisha mahusiano mtandaoni. 

Imeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.


Monday, October 24, 2022

RUVU SEKONDARI YAHITAJI MILIONI 794 KUFANIKISHA UJENZI WA UZIO

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ruvu mkoani Pwani wakiwa wamebeba keki iliyotolewa na wanafunzi waliosoma katika shule hiyo kuanzia mwaka 1977 hadi sasa ikiwa ni ishara ya kuzindua Kampeni ya ujenzi wa kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga uzio wa Shule hiyo ili kuimarisha usalama wa wanafunzi wa kike.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Ruvu mkoani Pwani Juliana Chimanzi (wa tatu kulia) akiwa na baadhi ya walimu waliofundisha katika shule hiyo( walioko kulia) wakiwa na baadhi ya wanafunzi waliosoma shuleni hapo kuanzia mwaka 1977 wakikata keki kuashiria uzinduzi wa Ujenzi wa uzio wa Shule hiyo .Wanafunzi hao wameamua kuchangishana fedha ili kusaidia kununua sehemu ya vifaa vya ujenzi na kukabidhi kwa uongozi wa Shule hiyo jana.
Zawadi zikitolewa.

Victoris Massawe( wa pili kulia) ambaye ni moja ya wanafunzi waliosoma katika Shule ya Ruvu Sekondari ambaye pia ni mmoja ya Waratibu wa michango ya wanafunzi akikabidhi tofali kwa Waziri MKuu wa Wanafunzi wa Shule hiyo Minael Katamba (kushoto) jana baada ya wanafunzi waliosoma kwenye shule hiyo kuanzia mwaka 1977 mpaka sasa kuamua kuchangia vifaa vya ujenzi kwa ajili ya kuanza ujenzi wa uzio wa Shule hiyo.

Baadhi ya wanafunzi walisoma katika Shule ya Sekondari Ruvu mkoani Pwani kuanzia mwaka 1977 hadi sasa wakiwa na baadhi ya wanafunzi walioko sasa pamoja na walimu wakiwa wameshika moja ya tofali kuashiria makabidhiano ya vifaa vya ujenzi kwa ajili ya kuanza ujenzi wa uzio wa Shule hiyo ambayo kwa sasa ni ya wanafunzi wa kike peke yake.Vifaa vya ujenzi matofali na nondo vimekabidhiwa shuleni hapo na wanafunzi waliosoma kwenye shule hiyo kuanzia mwaka huo ambao wameamua kuchangishana fedha kusaidia sehemu ya uzio wa Shule.
 Mwenyekiti wa Wanafunzi waliosoma kwenye shule hiyo,  Veronica Chambuso akizunguza katika tukio hilo. 
Dada Mkuu wa Shule ya Sekondari Ruvu Jacquline Mgisha, akuzungumza katika tukio hilo.

 Wanafunzi wa kwanza kabisa kuanza kusoma katika Shule ya Sekondari Ruvu iliyopoanza  mwaka 1977 wakijitambulisha kwa wanafunzi na walimu walioko sasa baada ya kufika shuleni hapo kwenye tukio la kukabidhi vifaa vya ujenzi nondo na matofali ili kuanza ujenzi wa uzio wa Shule hiyo.


 Na Mwandishi Wetu, Pwani


UONGOZI wa Shule ya Ruvu Sekondari umesema kiasi cha Sh.milioni 794.9 kinahitajia kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa uzio shule hiyo kwa lengo la  kuimarisha usalama wa wanafunzi wa kike 850 wanaosoma kwenye shule hiyo. 

Akizungumza jana wakati wa tukio la upokeaji wa vifaa vya ujenzi (matofali na nondo) vilivyotolewa na wanafunzi waliosoma shule hiyo tangu ilipoanzishwa mwaka 1977 mpaka sasa,  

Mkuu wa Shule ya Ruvu Sekondari Juliana Chimanzi alisema uzio wa shule ni muhimu kwani kuna changamoto ya mifugo kuingia eneo la shule lakini pia wezi na vibaka. 

"Nitoe  Serikali, wadau na kwa namna ya kipekee wanafunzi waliopita hapa kokote waliko watusaidie.Shule yetu ina idadi kubwa wanafunzi wasichana ambao wanafikia 850 , tunahitaji kuweka ulinzi kwa kujengewa uzio.Tumefanya tathimini Sh.Sh.milioni 794.9 zinahitajika,”aamesema. 

Awali akizungumza baada ya kukabidhi vifaa hivyo vya ujenzi, Mwenyekiti wa Wanafunzi waliosoma kwenye shule hiyo kwa nyakati tofauti Veronica Chambuso kuanzia mwaka 1977 amesema wameona wachangishane ili peleka vifaa vitakavyosaidia kuanza ujenzi wa uzio. 

“Tumeleta matofali na nondo , huu ni mwanzo lakini tunaendelea kuwaomba waliosoma Ruvu Sekondari kuanzia mwaka 1977 mpaka sasa na miaka inayokuja, wazazi , wafadhili na wale wanaoguswa na ulinzi wa watoto wa kike tushirikiane kwani ukimlinda mtoto wa kikekwani  akapata elimu itamsaidia na taifa litanufaika,”alisema Chambuso. 

Amefafanua kwamba  shule hiyo ilijengwa mwaka 1977 baada ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kuomba msaada Serikali ya Cuba, hivyo wanamshukuru kwa upendo wake na katika kumuenzi wameona kuna uhitaji mkubwa wa uzio. 

Kwa upande wao Waratibu wa Uchangiaji huo ambao nao ni sehemu ya wanafunzi waliosoma shule hiyo Devota Makililo na Victoris Massawe wameendelea kuhamasisha wadau kuendelea kuchangia ujenzi huo. 

“Tunaomba wadau na Wizara ya Elimu kuona huruma kwa shule ya wasichana watusaidie kwenye kujenge uzio.Pia kwa unyenyekevu mkubwa tunamuomba Rais Samia Suluhu Hassan atusaidie kufanikisha ujenzi huu.Watoto kike wakihitaji kuangaliwa na amekuwa akilisemea hilo mara kwa mara,”ameongeza. 

Wakati huo huo Dada Mkuu wa Shule ya Sekondari Ruvu Jacquline Mgisha anayesoma kidato cha Sita alisema wanashukuru wanafunzi waliopita shuleni hapo kutambua umuhimu wa jambo hilo. 

“Uzio ni muhimu sana kwetu , hivi makazi ya watu yamekuwa karibu na shule na hivyo kuhatarisha usalama wa wanafunzi.Pia tunamuomba mama yetu Rais Samia Samia Suluhu kutusaidia na hatimaye tuwe na uzio na sisi tutamlipa kwa kufanya vizuri kwenye masomo,”amesema. 

Thursday, October 20, 2022

VETA YATOA SHUKRANI KWA RAIS SAMIA KWA KUTOA FEDHA ZA KUIMARISHA MAFUNZO YA UFUNDI

Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Dodoma, John Mwanja akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa chuo hicho kwa Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Neema Mwakalyelye (kushoto), wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja ya kukagua ujenzi wa chuocha VETA wilayani Ikungi mkoani hapa juzi. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Jerry Muro.

Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Neema Mwakalyelye (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Ikungi. Kutoka kulia waliosimama mbele ni ni Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Ikungi, Erick Nyoni, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida,Widege Mzalendo, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi,Jerry Muro, Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, Mika Likapakapa na Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Dodoma, John Mwanja. Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ikungi (OCD) Suzana Kidiku na kushoto kwake ni Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Winfrida Funto.

 

Na Dotto Mwaibale, Singida

 

MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha mafunzo ya ufundi stadi nchini na kutoa fedha za miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa vyuo vipya na uboreshaji wa vyuo vya zamani.

 

Pongezi hizo zimetolewa juzi na Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Dodoma, John Mwanja mbele ya Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Neema Mwakalyelye kwa niaba ya mkurugenzi mkuu wa VETA wakati wa kikao na viongozi mbalimbali wa wilaya ya Ikungi cha kupata taarifa ya ujenzi wa chuo cha ufundi VETA kilichojengwa wilayani humo na VETA Kanda ya Kati-Dodoma kwa usimamizi wa TAKUKURU.

Aidha Mwanja alitoa shukurani hizo za dhati kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Neema Mwakalyelye kwa usimamizi thabiti katika shughuli za serikali hivyo kuifanya serikali ya Awamu ya sita ing’are katika kuwaletea wananchi maendeleo yao.

 

Katika hatua nyingine Mwanja alitoa shukrani kwa uongozi wa chama na serikali wa  Mkoa wa Singida na Wilaya ya Ikungi kwa ushirikiano wao mkubwa wanaowapa katika kutekeleza mradi huo wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya ya Ikungi.

 

Akizungumzia faida ya chuo hicho mara kitakapokamilika alisema kinatarajiwa kuhudumia wakazi wapatao 343,985 wa Wilaya ya Ikungi na wakazi  wapatao  1,754,370  wa  Mkoa  wa  Singida.  Pia,  wakazi  wa  mikoa  jirani  watanufaika  na huduma za chuo.

.

Alisema katika utaoaji wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi kwenye kozi za muda mrefu na kozi za muda mfupi,  chuo  hicho kitajielekeza  katika  kutoa  mafunzo  kwenye  maeneo  ya  kimkakati  kulingana  na mahitaji ya shughuli za kiuchumi wanazofanya wananchi wa Wilaya ya Ikungi na Mkoa wa Singida kwa ujumla.

 

Alisema katika kutekeleza mradi huo VETA imekumbana na changamoto mbali mbali kama

kupanda  kwa  bei  ya  vifaa  vya  ujenzi  wakati  wakiendelea  na  utekelezaji  wa  mradi,  hali iliyopelekea  pesa  iliyotengwa  kutokidhi  mahitaji  halisi  ya  mradi  kutokana  na  bei  za  vifaa kupanda zaidi ya matarajio ya awali.

.

Alitaja changamoto nyingine waliyokumbana nayo ni uwezo mdogo wa kiuchumi wa mafundi waliowatumia hivyo kupelekea kushindwa kuwalipa vibarua wao kwa wakati na kupelekea baadhi yao kuacha kazi, hivyo kupelekea kuchelewa kwa utekelezaji wa mradi.

 

“Sisi watumishi wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) husunani  VETA Kanda ya Kati tunaahidi kuendelea kutekeleza mradi huu na mingine yote kwa uadilifu mkubwa, na kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu, miongozo na maelekezo mbalimbali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania” alisema Mwanja.

TAKUKURU YAIPONGEZA VETA KWA UJENZI CHUO CHA UFUNDI WILAYA YA IKUNGI

Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Neema Mwakalyelye akizungumza na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Ikungi juzi wakati wa ziara yake ya siku moja ya kukagua ujenzi wa Chuo cha Ufundi  ambapo aliipongeza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)-Kanda ya Kati-Dodoma kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa mradi wa Chuo cha Ufundi cha VETA Wilaya ya Ikungi mkoani Singida.
Msimamizi wa ujenzi wa chuo hicho, Daudi Mrutu (kushoto) akitoa maelezo ya ujenzi wa chuo hicho kwa Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Neema Mwakalyelye (wa nne kutoka kulia. Wengine kutoka kulia ni Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida, Widege Mzalendo, Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Dodoma, John Mwanja na  Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Ikungi, Erick Nyoni.
Ukaguzi wa jengo la Utawala wa chuo hicho ukifanyika.
Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Dodoma, John Mwanja (wa pili kulia) akitoa maelezowakati wa ukaguzi wa jengo la utawala wa chuo hicho.
Safari ya ukaguzi wa majengo ya chuo hicho yakifanyika.
Muonekano wa moja ya nyumba ya walimu wa chuo hicho.
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida, Widege Mzalendo (kushoto) , akielekeza jambo wakati wa ukaguzi huo.
Muonekano wa baadhi ya majengo ya chuo hicho.
Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Neema Mwakalyelye (katikati) akiangalia baadhi ya samani zilizonunuliwa kwa ajili ya chuo hicho.
Msimamizi wa ujenzi wa chuo hicho, Daudi Mrutu (kulia) akitoa maelezo wakati akionesha vifaa mbalimbali vilinyonunuliwa kwa ajili ya chuo hicho.
Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Neema Mwakalyelye akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Jerry Muro wakati wa mkutano wa kupata taarifa ya ujenzi uliofanyika ukumbi wa chakula wa chuo hicho.
Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Dodoma, John Mwanja akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa chuo hicho.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Jerry Muro akizungumza wakati wa mkutano huo.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Singida, Mika Likapakapaaakizungumza katika mkutano huo.. Kushoto ni Katibu wa CCM Wilaya ya Ikungi Stamili Dendego na kulia ni Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida, Widege Mzalendo.
Mkutano ukiendelea.
Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Neema Mwakalyelye (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Ikungi. Kutoka kulia waliosimama mbele ni ni Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Ikungi, Erick Nyoni, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida,Widege Mzalendo, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi,Jerry Muro, Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, Mika Likapakapa na Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Dodoma, John Mwanja. Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ikungi (OCD) Suzana Kidiku na kushoto kwake ni Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Winfrida Funto.
 

Na Dotto Mwaibale, Singida

NAIBU Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Neema Mwakalyelye ameipongeza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)-Kanda ya Kati-Dodoma kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa mradi wa Chuo cha Ufundi cha VETA Wilaya ya Ikungi mkoani Singida.

Mwakalyelye alitoa pongezi hizo juzi wakati akizungumza na viongozi wa Wilaya ya Ikungi wakiwepo wajumbe wa kamati ya ulizi na usalama wa wilaya hiyo alipokuwa katika ziara ya siku moja ya kutembelea chuo hicho na kukagua ujenzi wake uliofanywa na VETA Kanda ya kati kwa kusimamiwa na TAKUKURU.

Aliwapongeza VETA kwa kukamilisha ujenzi huo kwa muda mfupi na kuwa amefarijika sana na kama wanavyofahamu Serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kwa miradi ya namna hiyo ya kimkakati na akasisitiza kuwa litakuwa ni jambo la kuvunja moyo na kuhuzunisha pale ambapo kutakuwa na ufujaji au upotevu wa utekelezaji wa mradi ambao hauonekani moja kwa moja lakini unaonekana katika viwango vya mradi husika.

“Nifaraja nimekuja na kuona hatua mliyofikia majengo mliyojenga na miundombinu ipo katika viwango tarajiwa vinavyotakiwa na Serikali na hilo nalo ni sababu nyingine ya kuwapongeza wale wote mlioufikisha ujenzi huu katika hatua hii nzuri licha ya mradi kuwa na changamoto kubwa” alisema Mwakalyelye.

Alisema VETA wanakuwa mfano wa kuigwa kwa sababu miradi ya namna hiyo inaendelea katika sehemu mbalimbali ya nchi na kama mkurugenzi alivyosema kuwa nia ya Serikali ni kuwa mwaka wa fedha ujao kila wilaya ambazo ni takribani 62 zitakuwa na miradi yenye sura kama hiyo ikiendelea.

Alisema kutokana na hali hiyo hatarajii kusikia VETA amekwenda Waziri Mkuu kufungua mradi wa chuo na kukutana na sintofahamu  kwa sababu Ikungi wanauzoefu wa kutosha wa kuonesha miradi ya namna hiyo inaweza kufanyika na thamani ya fedha ikaonekana na kupatikana .

“Nimtake Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Dodoma John Mwanja ampelekee ujumbe huu Mkurugenzi Mkuu wa VETA nchini kuona kwamba miradi kama hii inayofanywa vizuri itumike kama miradi ya mafunzo ya ndani kwa ajili ya kujengeana uwezo katika maeneo mengine ambayo miradi ya namna hiyo inapelekwa” alisema Mwakalyelye..

Alisema haitakuwa na maana kuona mradi wa Ikungi umekamili vema lakini baada ya siku au miezi kadhaa katika maeneo mengine eti mkuu wa chuo au mkurugenzi wa kanda wa VETA wamesimamishwa kwa ujenzi uliochini ya kiwango hivyo kwa uzoefu huo walioupata Ikungi wautumie katika maeneo mengine ili kuepuka hasara inayoweza kutokea kutokana na watu wasio na ufahamu kamili au kuwa na nia ovu ambapo aliomba wapewe ushirikiano katika uendelezaji wa wilaya hiyo ambayo inakuwa kwa kasi kubwa.

Aidha Mwakalyelye aliwataka viongozi wilayani humo kuhakikisha wanasimamia vizuri ununuzi wa mbembejeo za kilimo na mapato yote yanayokusanywa yanaingizwa kwenye akaunti za Serikali na si vinginevyo.

Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati John Mwanja akitoa taarifa ya ujenzi wa chuo hicho alisema Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya ya Ikungi chenye umiliki wa Hati namba: 2218- SGD  kinajengwa  katika  Kijiji  cha Muungano,Kata  ya Unyahati  wilayani  Ikungi  katika  mkoa  wa Singida kwenye eneo lenye ukubwa wa ekari 50.

Alisema Mradi huo  ulianza mnamo mwezi Machi, 2020 ukisimamiwa na chuo cha VETA Singida na ulipaswa kutekelezwa kwa muda wa miezi sita hata hivyo, haukuweza kukamilika kwa wakati kutokana na changamoto kadhaa zilizojitokeza na baadaye mradi kusimama kwa muda wa mwaka mmoja.

Alisema Mkurugenzi Mkuu wa VETA Februari 28/2022 alihamishia majukumu ya usimamizi wa Ujenzi wa chuo hicho  kutoka Chuo cha VETA Singida kwenda ofisi ya  Mkurugenzi wa VETA Kanda ya kati ambaye hadi sasa ndiye anaendelea na usimamizi wa ujenzi huo ambao unatekelezwa kwa  mfumo wa “Force Account”.

Akizungumzia utekelezaji wa ujenzi huo alisema unahusisha jumla ya majengo 17 ambayo ni Jengo moja la utawala, Majengo manne  ya karakana, jengo moja la madarasa mawili makubwa, majengo mawili  ya mabweni  (Wasichana na Wavulana), Bwalo la chakula na Jiko, Majengo Matatu  ya vyoo (Wasichana Wavulana  na  Watumishi),  nyumba  mbili  za  watumishi,  jengo  la  umeme,  Jengo  la  bohari  na kibanda cha mlinzi. Kwa wastani hatua ya ujenzi hadi sasa imefikia asilimia 96.

Mwanja alisema mradi wa ujenzi wa chuo hicho unatarajiwa kukamilika mwishoni katikati ya mwezi Novemba, 2022 na kuwezesha kutoa nafasi ya kufanya ukamilishaji wa taratibu zingine zenye kuwezesha utoaji wa mafunzo katika chuo.

Alisema  chuo kitakapokamilika, kitaendesha mafunzo ya kozi ndefu na fupi na kkuwa ya muda mrefu yatachukua muda wa miaka miwili hadi mitatu ambayo  yatatolewa katika fani zipatazo sita katika awamu ya kwanza mara chuo kitakapokamilika ambazo ni Uhazili na Kompyuta (Secretarial and Computer Application),Ushonaji (Design Sewing and Cloth Technology), Uashi (Masonry and Bricklaying),Umeme wa Majumbani (Electrical Installation),Ufundi Magari (Motor Vehicle Mechanics) na Uchomeleaji Vyuma (Welding and Metal Fabrication).

Alisema chuo  kitakuwa  na  uwezo  wa  kudahili  wanafunzi  240  wa  kozi  ndefu  na  uwezo  wa  kuchukua wanafunzi 144 wa bweni  (wasichana 64 na wavulana 80).

Alisema pia, kutakuwa na mafunzo ya muda mfupi (Short Courses) yatakayochukua muda wa mwezi mmoja hadi miezi sita kwa wastani mafunzo hayo yanakadiriwa kudahili wanafunzi wapatao 250 hadi 900 kwa mwaka kutegemeana na mahitaji ya jamii na shughuli za kiuchumi za eneo hilo.