Wednesday, March 30, 2022

WAZAZI WA WANAFUNZI WALIOFAULU KWENDA SEKONDARI LAKINI HAWAJARIPOTI SHULENI KUFIKISHWA KORTINI IRAMBA

Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida Suleiman Mwenda akitoa maelekezo kwa wajumbe wa kamati ya Siasa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo wakati wakikagua moja ya caravati linalojengwa katika Barabara ya Maluga Mtaa Saba -Misuna na Mgungia hadi Kaselya wakati kamati hizo zilipokuwa zikikagua  miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wake Tarafa ya Shelui wilayani humo jana.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iramba, Samuel Ashery akizungumza wakati kamati hizo zilipokuwa zikikagua mradi wa maji wa Kijiji cha Wembere uliopo katika Tarafa hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Innocent Msengi akizungumza kwenye ziara hiyo.
Afisa Tarafa ya Kinampanda Cholo Mtaki akiwatambulisha viongozi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Kitukutu wakati wa ziara ya kamati hizo.
Meneja wa Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Iramba Mhandisi Ezra Mwacha akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi wa maji wa Kijiji cha Wembere.
Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Misigiri akitoa taarifa ya mradi wa vyoo na uwekaji wa miundombinu ya maji katika zahanati hiyo.
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kitukutu Dada Kazimoto akizungumza mbele ya kamati hiyo.
Ukaguzi wa tenki la maji katika zahanati hiyo ukifanyika.
Diwani wa Kata ya Ulemo akichangia jambo kwenye ukaguzi wa mradi huo wa vyoo.
Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Ulemo Luka Kasanga akitoa taarifa ya ujenzi wa zahanati hiyo.
Muonekano wa zahanati hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akichangia jambo wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa zahanati hiyo ya Ulemo.
Muonekano wa bweni la Wasichana wa Shule ya Sekondari ya Tumaini baada ya ujenzi wake kukamilika
Wajumbe wa kamati hizo wakipokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Shule ya Wasichana ya Tumaini, Mwalimu Zainabu Mtinda ya kukamilika kwa ujenzi wa bweni katika shule hiyo.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya KengyegeMwalimu Emmanuel Twiyogehe akitoa taarifa ya ujenzi wa shule mpya ya Sekondari ya Maluga.
Muonekano wa baadhi ya majengo yanayoendelea kujengwa Shule mpya ya Maluga.
Mafundi wakiendelea na ujenzi wa shule hiyo mpya ya Maluga.

Mkzi wa Kijiji cha Maluga akiishukuru Serikali na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa shule hiyo.
Diwani wa Kata ya Maluga akichangia jambo kuhusu ujenzi wa shule hiyo.
Wajumbe wa kamati hizo wakikagua ujenzi wa shule hiyo.
Mafundi wakiendelea na ujenzi wa shule hiyo.


Mkutano wa hadhara ukiendelea Kijiji cha Kitukutu.
Mkutano ukiendelea.Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Iramba Michael Abbas akizungumza wakati akiwatambulisha viongozi wa chama hicho kwenye mkutano huo.

Katibu wa CCM wa Wilaya ya Iramba, Comrade Ephrahimu Kolimba akizungumza kwenye mkutano huo.
Afisa Elimu Sekondari wa Wilaya hiyo Mr Mwajala akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo ambapo aliwahimiza Wazazi na Walezi kuhamasika kuchangia chakula cha wanafunzi wakiwa shuleni.


Mkaguzi wa mradi wa maji wa Kijiji cha Wembere ukifanyika.
Muonekano wa mradi huo wa maji wa Kijiji cha Wembere.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Wembere Eliud Mbogo akiishukuru Serikalikwa kuwapelekea mradi huo.
DC Mwenda akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo wa maji.
Makofi yakipigwa kufurahia mradi huo.
Ukaguzi wa ujenzi wa Kituocha Afya cha Umtoa ukiendelea.
Muonekano wa baadhi ya majengo yanayoendelea kujengwa ya Kituocha Afya Mtoa
Mganga Mkuu Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mtoa, Sori Abushehe akitoa taarifa ya ujenzi wa kituo hicho.
Muonekano wa chumba cha maabara ya Shule ya Sekondari ya Mtoa kinachoendelea kujengwa.Ukaguzi wa ujenzi wa maabara hiyo ukiendelea

Meneja wa TARURA wa wilaya hiyo Venance Kibona akitoa taarifa ya ujenzi wa Barabara ya Shelui kwenda Tintigulu.
DC Mwenda akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nselembwe wakati wa ukaguzi wa barabara hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda pamoja na wajumbe wa kamati hizo wakisaidia kuchanganya mchanga wa ujenzi wa nyumba ya watumishi wa Kituo cha Afya Shelui.
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Shelui, Alex Mpwenku akitoa Taarifa ya ujenzi wa nyumba ya watumishi wa kituo hicho.

Tuesday, March 29, 2022

TANZANIA YAJIPANGA KUTUMIA WANAHABARI KUFIKIA MAAZIMIO YA MALABO

p>

Meneja wa Kituo cha Utafiti cha TARI Mikocheni Dkt.Joseph Ndunguru akifungua mafunzo hayo ya kitaifa ya siku nne kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TARI.
Afisa Programu ya CAADP -XP4, Bi. Futh Magagula akitoa salamu za Taasisi ya Uratibu wa Tafiti za Kilimo Afrika (CCARDESA) wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo jijini Dar es salaam.

Meneja wa Mawasiliano na menejimenti ya Maarifa kutoka Taasisi ya Utafiti Tanzania (TARI) Dkt. Richard Kasuga akieleza malengo ya Mafunzo hayo ya Kiataifa ya siku nne kwa Maafisa mawasiliano, Wanahabari na wadau wengine.

Afisa Habari na Menejiment ya Maarifa kutoka kutoka Taasisi ya Uratibu wa Tafiti za Kilimo Afrika (CCARDESA) Bi. Bridget Kakulwa akieleza akieleza matarajio ya Mafunzo hayo.Bwana Shadrack Ndalawa msimamizi wa dawati la CAADP Wizara ya Kilimo akieleza utekeeleaji wa maazimio Malabo upande wa TanzaniaWashiriki wa Mafunzo hayo wakifuatilia Hotuba za ufunguzi. 

Washiriki wa Mafunzo hayo wakifuatilia Hotuba za ufunguzi.


 Washiriki wa Mafunzo hayo wakifuatilia Hotuba za ufunguzi.


Washiriki wa Mafunzo hayo wakifuatilia Hotuba za ufunguzi.

Mafunzo yakiendelea.

Washiriki wa Mafunzo hayo wakifuatilia Hotuba za ufunguzi.

Mafunzo yakiendelea

Washiriki wa Mafunzo hayo wakifuatilia Hotuba za ufunguzi.



Na Calvin Gwabara – Dar es salaam.

MAAFISA Mawasiliano na Waandishi wa habari wametakiwa kutumia taaluma zao kufikisha matokeo ya tafiti na vumbuzi mbalimbali zinazozalishwa na watafiti nchini kwa Wakulima na wafugaji ili zisaidie kutatua changamoto zinazoikabili sekta hiyo ili kuinua uchumi wa watu na taifa kwa ujumla.

Wito huo umetolewa na Meneja wa kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Mikocheni Dkt. Joseph Ndunguru wakati akifungua mafunzo ya kitaifa ya siku nne ya kuwajengea uwezo Maafisa mawasiliano, Wagani na Waandishi wa habari namna ya kuchakata matokeo ya Tafiti na kuwafikishia walengwa sambamba na kufuatilia na kutoa taarifa za utekelezaji wa maazimio ya Malabo ulioandaliwa na Taasisi ya Uratibu wa Tafiti za Kilimo (CCARDESA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI).

“Mafunzo haya ni muhimu sana kwa maafisa mawasiliano hawa kutoka vituo vyote vya utafiti nchini, Wizara ya Kilimo, Wizara ya mifugo na Uvuvi, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Mamlaka ya Hali ya Hewa pamoja na Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari maana wana jukumu kubwa la kuhakikisha wanatafsiri matokeo ya tafiti kwa lugha rahisi na kuwafikishia walengwa na kwa kufanya hivyo kutasaidia wakulima kulima kilimo chenye tija na pia kusaidia kufikia malengo ya Maazimio ya Malabo” alisema Dkt. Ndunguru.

Aidha amefafanua kuwa kupitia mafunzo hayo kutawawezesha kujua Maazimio saba ya Malabo na hivyo kuchochea Serikali kutimiza malengo yake ya kutenga asilimia kumi ya Pato la taifa kuingiza kwenye kilimo na ushiriki wa wadau wengine katika kusaidia kuinua kilimo na kuinua uchumi wa jamii na taifa.

Dkt. Ndunguru amesema zaidi ya asilimia 55 ya Waafrika wamejiajiri kwenye sekta ya kilimo lakini bado kilimo hakijatoa  mchango unaokusudiwa katika kuinua pato la taifa na hii ni kutokana na sababu mbalimbali ambazo zingine tayari sababu hizo majibu yake yamepatikana kupitia tafiti za kisayansi lakini hazijawafikia walengwa.

Kwa upande wake Afisa Programu ya CAADP -XP4 kutoka CCARDESA Bi. Futh Magagula ameipongeza Tanzania kwa kuwa nchi ya kwanza kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa kwenye mkutano wa mwisho uliofanyika Afrika kusini kwa kufanya mafunzo haya kwa wataalamu hawa wa mawasiliano ili kufahamu mchango wao katika kusaidia utekelezaji wa maazimio ya Malabo.

“Hii inaonyesha kuwa Tanzania inazingatia na kuyachukulia umuhimu maazimio ya Malabo lakini pia CCARDESA inazingatia sana swala la usimamizi wa maarifa kwani ni sehemu ya maeneo muhimu katika mpango mkakati wake wa muda mrefu” alieleza Bi. Futh.

 Ameendelea kusema kuwa Programu ya CAADP -XP4 inaendelea kusaidia nchi za ukanda wa SADC kuweza kufikia maazimio ya Malabo hivyo mafunzo hayo ya kitaifa yana umuhimu mkubwa kwa CCARDESA kwa ujumla.

Bi. Magagula ameushukuru Umoja wa Ulaya (EU) kufadhili Programu ya CAADP -XP4 na kuwezesha kufanikishwa kwa mafunzo haya muhimu pamoja na IFAD kwa kusaidia masuala ya kitaalamu.

Nae Meneja wa Mawasiliano na menejimenti ya Maarifa kutoka Taasisi ya Utafiti Tanzania (TARI) Dkt. Richard Kasuga amesema mafunzo haya ni moja ya mikakati ya kuhakikisha matokeo ya tafiti yanawafikia wakulima kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Kitaifa, Kikanda na kimataifa wamekuwa wakishirikiana kujenga katika masuala ya menejimenti ya maarifa na mawasiliano.

“Mafunzo haya yaliyoandaliwa kwa Tanzania ni kuhakikisha tunajenga uwezo kwa wataalamu wetu ili waweze kuchakata na kuweza kusambaza taarifa hususani matokeo ya utafiti ili yaweze kuwafikia walengwa mbalimbali wakiwemo wakulima wasindikaji na wadau wengine muhimu katika sekta hiyo” alisisitiza Dkt. Kasuga.

Ameongeza kuwa wanafanya hivyo kwakuwa kama tafiti zinazofanywa na TARI au CCADERSA unaweza kufanya vizuri na kuwainua Wananchi wa Tanzania basi unaweza pia kusaidia kuinua wananchi wa nchi nyingine za kusini mwa Afrika kama vile Malawi, Zambia, Zimbabwe na nchi zingine.

Dkt. Kasuga amesema pamoja na masuala ya kubadilishana maarifa lakini pia wana shughulika na kutangaza masuala mbalimbali kama vile utekelezaji wa maazimia ya Malabo utekezaji wake kupitia taasisi mbalimbali ili yaweze kueleweka kwa Wananchi na wadau ili wananchi waweze kushirikiana na serikali yao kuhakikisha kilimo kinawaletea maendeleo.