Friday, July 17, 2020

I&M BANK TANZANIA SUPPORTS THE MIDDLE INCOME STATUS,INAUGURATES ITS MAIN BRANCH AS IT LAUNCHES A SPECIAL ‘I&M TUNAWEZA WOMEN ACCOUNT’

Dar es Salaam.
I&M Bank Tanzania announced the Inauguration of its relocated Main Branch as well as the launch of their first-ever account, exclusively for women in Tanzania.  This two-tier event took place at their Main Branch new premises located at Indira Gandhi Street next to NIDA Textile building, on 15th July, 2020.

The newly refreshed branch is testimony of I&M Bank’s commitment to the market and its customers; loyal to the Bank for over 10 years having taken over from CF Union. Dr. Bernard Y. Kibesse, BOT Deputy Governor, officiated the inauguration and further commended I&M for its good work in support of the economy.

Speaking during the inauguration, Dr. Kibesse further applauded the Bank for its understanding of the needs of their customers and responding positively by ensuring they get the best experience while visiting the Bank, “10 years of existence in the market, with extensive trend of profit making gives the market a very high promising future to bank with I&M”, he capped.

The Bank took the opportunity of the inauguration of the Main Branch, to officially launch I&M Tunaweza Women’ Account, a special product dedicated to women entrepreneurs. Ambassador Bertha E. Semu-Somi, I&M Bank Board member, announced the official launch. 

She said the move will help Tanzanian women to improve their saving culture, while enabling them to meet their targeted economic dreams. 

She noted that the special account dedicated to women, had distinguished features scarcely in the market,
The newly launched ‘I&M Tunaweza Women Account’ comes in 3 variants: Tunaweza Individual Savings Account, Tunaweza Current Account for businesses and Tunaweza Group Account for Associations, with each offering various privileges and benefits to the account holder.

“I am excited by the response of the Guest of honor and our invitees here to witness the inauguration of our Main Branch and the introduction of this most exciting Women Account in the market. 

This year we are celebrating 10 successful years of our existence in the market, having originated from a very strong group bank of I&M holding in Kenya.” Said Baseer Mohammed, I&M Bank’s CEO.

"We salute the spirit of women for striking the perfect balance between managing work and family. We believe that it is our responsibility as an organization to make opportunities available for women to invest in themselves. 

This account has very exciting features with no monthly fees as well as transaction charges to support women in different fields. Said Lilian Mtali, Head of Retail Banking, I&M Bank.

I&M Bank has presence in Dar es Salaam, Arusha, Mwanza and Moshi with fully-fledged branch operations in those specific areas.

 I&M Bank Board Member, Ambassador Bertha Semu-Somi, explaining the unique features of the newly launchedTunaweza Women Account during the bank’s Main branch inauguration.
Ms. Salima Amirali Abji, I&M Bank customershares her testimonial of ‘Tunaweza Women Account’ and commended the bank for realizing the need of many women and decidingto come up with the product to elevate them.  
Ms. Lilian Mtali, Head of Retail Banking, speaking during the launch of the bank’s Main branch located at Indira Gandhi street next to Nida Textile on Wednesday 15th July 2020.
Mr. Stephen K.Basimwaki, I&M Bank  customer  shares his banking journey of over 10 years since the bank opened its doors in Tanzania. He was delighted to see the bank continue growing and providing its customers with such spacious and comfortable building. This happened during the inauguration ceremony of I&M Bank Main branch on Wednesday 15th July 2020.
Guest of Honor Dr. Bernard Kibesse - Deputy Governor, Bank of Tanzania (in the middle) cuts the ribbon tape marking the official launch of new Main branch.From left,Mr. Baseer Mohammed I&M Bank CEO and on the right of Dr Bernard Kibesse is Ms. Lilian Mtali, Head of Retail Banking and Rebecca Sanga the Branch Manager. 
From left, Mr. Baseer Mohammed I&M Bank CEO, Ms. Lilian Mtali, Head of Retail Banking, Dr. Bernard Y.Kibesse Deputy Governor Bank of Tanzania, Amb. Bertha Semu-Somi I&M Bank Board Member and Mr. Bharat RupaleliaI&M Board Director in a photo session after Dr. Bernard Y. Kibesse inaugurated I&M Bank Main Branch on 15th July 2020.

Saturday, July 11, 2020

JPM AMWAGA KIWANDA KIKUBWA CHA KUKU NA KLINIKI YA KISASA YA MIFUGO SINGIDA



Waziri wa Mifugo na Uvuvi (mwenye kofia nyeusi) Luhaga Mpina akishiriki katika zoezi la uchanjaji wa mifugo kitaifa pamoja na wataalam wa mifugo lililofanyika leo kwenye kijiji cha Kinyangiri wilayani Mkalama mkoani Singida ambapo Serikali imeahidi kuwezesha kujenga kiwanda kikubwa cha machinjio ya kisasa kitakacholisha Tanzania na nchi mbalimbali duniani.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi (mwenye kofia nyeusi) Luhaga Mpina wa kwanza kulia akifuatiwa na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Singida ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Injinia Jackson Masaka na Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida ndugu Beatus Choaji wakiwa kwenye sherehe za uzinduzi wa uchanjaji wa mifugo kitaifa pamoja na wataalam wa mifugo lililofanyika leo kwenye kijiji cha Kinyangiri wilayani Mkalama mkoani Singida.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi (mwenye kofia nyeusi) Luhaga akionyeshwa kifaa maalum cha kuchanjia mifugo wakati wa zoezi la uchanjaji wa mifugo kitaifa pamoja na wataalam wa mifugo lililofanyika leo kwenye kijiji cha Kinyangiri wilayani Mkalama mkoani Singida.

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi (mwenye kofia nyeusi) Luhaga akihutubia umati wa wadau wa mifugo wakati wa zoezi la uchanjaji wa mifugo kitaifa pamoja na wataalam wa mifugo lililofanyika leo kwenye kijiji cha Kinyangiri wilayani Mkalama mkoani Singida.
Umati wa wadau wa mifugo wakati wa zoezi la uchanjaji wa mifugo kitaifa pamoja na wataalam wa mifugo lililofanyika leo kwenye kijiji cha Kinyangiri wilayani Mkalama mkoani Singida.



Na John Mapepele, Singida

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina amesema Serikali inakusudia kuwezesha kujenga kiwanda kikubwa cha kisasa cha kuchaka nyama ya kuku kwenye Mkoa wa Singida kitakacholisha Tanzania na nchi mbalimbali duniani ambacho kitakuwa kinafanya uzalishaji ifikapo Desemba mwaka huu ili kuinua hali za wafugaji wa kuku wa Singida na kuongeza pato la taifa.

Mbali na kiwanda hicho, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inatarajia kujenga Kliniki bora ya kisasa ya mifugo kwenye Halmashauri ya Mkalama.

Kliniki hiyo ni miongoni mwa Kliniki 30 ambazo zinazijengwa nchi nzima na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli kwenye Halmashauri mbalimbali.

Waziri Mpina ameyasema haya kwenye hotuba yake ya uzinduzi wa Kampeni ya Chanjo za Mifugo Kitaifa kwenye kijiji cha Kinyangiri katika Wilaya ya Makalama mkoani Singida ambayo imelenga kutokomeza magonjwa mbalimbali ya mifugo (hususan magonjwa 13 ya kipaombele) ambayo yamekuwa kikwazo katika uzalishaji na biashara ya mifugo ndani na nje ya Tanzania.

“Tumeona hapa uzalishaji mkubwa sana wa kuku Singida, sasa ninaagiza mambo makubwa mawili Bodi ya Nyama na Dawati la linaloshughulikia Sekta Binafsi katika Wizara yangu kuwezesha kujenga kiwanda cha kuchakata nyama ya kuku na tutakizindua kikiwa kinatoa huduma ifikapo Desemba mwaka huu"Alisema

"Lakini la pili ninamuagiza Mkurugenzi wa Uzalishaji na Masoko na Dawati la Sekta Binafsi kuunda vikundi na kuwaletea vitotoleshi vya kisasa ili kuongeza kasi ya uzalishaji wa kuku ili kuwezesha upatikanaji wa malighafi za kiwanda kwa uhakika” alisisitiza Waziri Mpina.

Mpina amesema magonjwa mengi ya mifugo ni yale ya kuambikiza hususani yanayotokea kwa mlipuko na kusabisha vifo na hasara kubwa kwa wafugaji na kufafanua kuwa hadi sasa tayari, Serikali imekiimarisha kiwanda cha chanjo cha Tanzania Vaccine Institute (TVI) na kinazalisha aina sita (6) ya chanjo za kipaumbele na kitaanza kuzalisha aina nyingine tatu kufikia mwezi Desemba, 2020.

Mbali na Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuanza kutengeneza chanjo sita Mpina amesema mapinduzi na mageuzi makubwa yamefanyika ili kuhakikisha kuwa Sekta ya Mifugo inatoa mchango mkubwa katika uchumi wa nchi na kwa mwananchi mmoja mmoja tofauti na awali ambapo sekta hiyo na wafugaji walidharaulika sana.

Ametaja baadhi ya mambo yaliyoboreshwa kwenye eneo la chanjo hapa nchini kuwa ni pamoja na Wizara yake kupitisha Mpango wa Ununuzi wa Chanjo za Mifugo kwa Pamoja (Vaccine Bulk Procurement Plan);

Serikali kutangaza Bei Elekezi ya chanjo aina 13 za magonjwa ya kipaumbele ambapo chanjo zimepungua bei kwa zaidi ya asilimia 60;

Amebainisha kuwa, Katika mwaka 2019/2020, Serikali katika kiwanda cha TVI imezalisha jumla ya dozi 53,851,850 za chanjo za magonjwa ya mlipuko na yanayovuka mipaka na chanjo hizi zote zimechanja mifugo.

Pia, Wizara imevutia wawekezaji na kiwanda kikubwa cha Hester Biosciences Africa Limited kinajengwa na kitakapokamilika kitakuwa kinazalisha aina 37 ya chanjo za wanyama.

Ameongeza kuwa katika mwaka 2019/2020, utoaji wa chanjo umeimarika ambapo Halmashauri 103 kati ya 185 sawa na asilimia 56 zimeshiriki kikamilifu katika kutoa chanjo kwa mifugo

Aidha Mpina amesema kutokana na mikakati ya Wizara yake ya kudhibiti utoroshaji wa mifugo kutoka nchni kwenda nchi za nje na udhibiti wa uingizaji holela wa bidhaa za mifugo nchini kupitia “Operesheni Nzagamba” Serikali ya awamu wa Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliweza kukusanya zaidi ya bilioni 50 kwa mwaka ukilinganisha na Shilingi bilioni 9.5 zilizokuwa zikikusanywa katika kipindi cha nyuma kwa mwaka.

Akitoa maelekezo kwa wataalam Waziri Mpina amewataka wataalmu wote wa mifugo ngazi ya Wizara, Mikoa, Wilaya na Kata kuhakikisha uchanjaji wa mifugo unatekelezwa kikamilifu kulingana na kalenda ya chanjo kwa kuwa ni suala la kisheria ambapo amemtaka Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) kuhakikisha unasimamia jukumu hili na yeye kupatiwa ripoti ya chanjo hizo kila mwezi.

Pia amewataka Wataalamu wote wa mifugo kuhakikisha wanatoa elimu ya chanjo kwa wafugaji ili watambue umuhimu na faida za kuchanja mifugo yao na kwamba, Serikali imeshaandaa mazingira wezeshi ya upatikanaji wa chanjo kila mahali na kwa bei elekezi.

Amesema kulingana na Kalenda ya chanjo kitaifa, mwezi Juni mpaka Augosti, 2020 ni msimu wa chanjo za Homa ya Mapafu ya Ng'ombe, Homa ya Mapafu ya Mbuzi, Sotoka ya Mbuzi na Kondoo, Ugonjwa wa kutupa mimba na Ugonjwa wa Miguu na Midomo.

Hivyo, ametoa wito kwa madaktari wa mifugo wote nchini kuhakikisha kwamba chanjo hizi zinatolewa kikamilifu.

Aidha ameziagiza Halmashauri zote ambazo hazitowi huduma ya chanjo kwa mifugo yao kufanya hivyo mara moja kuanzia mwezi huu wa Julai, 2020.

Ripoti ya idadi ya mifugo na aina ya chanjo inayotolewa iwe inaletwa kwa Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) kila wiki

Thursday, July 2, 2020

SPORTPESA YAIPA SIMBA SC SH MILIONI 100 KWA KUTWAA TAJI LA LIGI KUU TANZANIA BARA

Wadhamini wakuu wa klabu ya Simba SC, Sport Pesa Tanzania wakiwakabidhi mfano wa hundi ya Shilingi Milioni 100, Nahodha wa klabu hiyo, John Raphael Bocco baada ya kushinda ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa mara ya tatu mfululzo. Fedha hizo zimetolewa kama sehemu ya makubaliano ya mkataba wa udhamini uliosainiwa mwaka 

TAKUKURU MKOA WA SINGIDA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI HAKIMU, MZAZI MWENZAKE KWA TUHUMA ZA KUOMBA RUSHWA


 Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Singida , Adili Elinipenda, akizungumza leo asubuhi kuhusu kukamatwa, Bahati  Ilikunda Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kilimatinde wilayani Manyoni na Mzazi mwenzake Haji Bwegege kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa. Kulia ni Afisa wa TAKUKURU, Shemu Mgaya.
Maafisa wa TAKUKURU wakiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari.




Na Dotto Mwaibale, Singida

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Singida inatarajia kuwafikisha kwenye Mahakama ya Wilaya ya Manyoni, Bahati  Ilikunda Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kilimatinde na Mzazi mwenzake Haji Bwegege ambao kwa pamoja wanatuhumiwa kwa makosa ya kuomba na kupokea Rushwa kinyume na kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na.11 ya Mwaka 2007.

Akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye ofisi  za PCCB, Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Singida, Adili Elinipenda, alisema walipokea taarifa kutoka kwa mwananchi mmoja ambaye jina lake wamelihifadhi, kuwa Bahati Ilikunda wa Mahakama ya Mwanzo Kilimatinde Wilayani Manyoni anaomba Rushwa ya shilingi 350,000/=, ili atoe upendeleo kwa mtoa taarifa kwenye shauri la madai namba 03/2020, shauri ambalo lipo mbele yake .

Alisema Juni 28/ 2020 huko wilayani Manyoni  maeneo ya kituo cha mabasi yaendayo Dodoma, Maofisa wa TAKUKURU walimkamata Haji Bwegege ambaye ni mzazi mwenzake na Bahati baada ya kupokea rushwa ya  shilingi 170,000/= ikiwa ni sehemu ya  shilingi 350,000/=zilizoombwa.

Alisema uchunguzi wa TAKUKURU mkoa wa Singida umejiridhisha kuwa Haji Bwegege na Bahati Ilikunda  wana mahusiano ya kifamilia (Wana mtoto waliyezaa pamoja) jambo linaloashiria uwezekano wa Bahati kumtumia Haji katika kupokea rushwa anazoziomba. 

Ofisi ya TAKUKURU Mkoa wa  Singida inatoa shukrani za dhati kwa Idara ya Mahakama mkoani hapa kwa jinsi wanavyoshirikiana kwenye mapambano dhidi ya Rushwa  kuanzia Mahakama ya Mwanzo hadi Mahakama ya Mkoa.

NDALICHAKO ATIMIZA AHADI ATOA VYEREHANI 10 VETA MPANDA



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ametimiza ahadi ya kutoa vyerehani 10 kwa wanafunzi waliohitimu​ mafunzo ya ushonaji kutoka Chuo cha Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi​ Mpanda​ wanaotoka katika mazingira magumu.

Akizungumza katika halfa hiyo Mkoani Katavi, Profesa Ndalichako amesema ahadi hiyo aliitoa​ mwaka 2018 baada ya kuwakuta vijana wadogo wamemaliza masomo ya darasa la saba na kushindwa kuendelea na masomo ya sekondari​ na kujiunga na mafunzo ya ushonaji katika chuo hicho kupitia msaada wa kanisa.


“Mwaka juzi nilifika katika chuo hiki na kuwakuta hawa vijana wawili wadogo wakiwa katika mafunzo ya ushonaji na nilipozungumza nao niligundua kuwa wametoka katika mazingira magumu, hivyo kushindwa kuendelea na masomo ya sekondari, ndipo nilipowaahidi kuwapatia vyerehani watakapomaliza ili viwawezeshe kujiajiri.​ Hata hivyo, nimetoa vyerehani 10 ili na wengine wenye mazingira ya namna hiyo waweze kupata,” amesema Waziri Ndalichako.

Aidha, Waziri huyo amemuagiza Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi Mpanda kuona namna ya kuwapatia nafasi ya kuendelea na ngazi nyingine ya mafunzo watoto hao​ ili kuwawezesha kuwa mahiri katika ushonaji na kuhakikisha anawasimamia na kuwashauri popote watakapokuwa wanafanya shughuli zao.

Mkuu wa Chuo cha Ufundi Mpanda Elisha amemshukuru waziri kwa kutimiza ahadi aliyoitoa mwaka 2018 kwani inakwenda kuinua watoto wanaotoka katika familia masikini, na kuahidi kuendelea kuwasimamia ili cherehani hizo ziwe na manufaa kwa watoto wenyewe na familia zao.

Mmoja wa wanafunzi waliopatiwa cherehani Gift Giles amemshukuru Waziri kwa kuwapatia cherehani hizo ambazo zinakwenda kubadili maisha yao kwani zitawawezesha kupata fedha ambazo zitawasaidia kujiendeleza katika masomo


Naye mmoja wa walezi wa wanafunzi hao Bibi Flora Cosmas amemshukuru Mhe. Ndalichako na kuahidi kuwasimamia ili waweze kutumia machine hizo vizuri ikiwa ni pamoja na kuwaendeleza zaidi kiujuzi.

"Sisi walezi wa vijana hawa tunamahukuru sana Mhe. Waziri​ kwa kuguswa kwake kuamua kwa moyo wake kufanya jambo hili kubwa maana anakwenda badili naisha ya vijana hawa ambao hawakuwa na uwezo wa kununua hizi cherehani" amesema bi Cosmas.

DKT. NCHIMBI AMPA TANO RAIS KWA KUIINGIZA TZ KATIKA UCHUMI WA KATI


 Mkuu wa MKoa wa Singida Dkt. Rehema
Nchimbi akifunga  mafunzo maalum ya  siku sita kwa wadau zaidi ya 300 kutoka katika mikoa mbalimbali nchini  yaliyokuwa yameandaliwa na Baraza la Taifa  la watu wanaoishi na  virusi vya UKIMWI (NACOPHA) kupitia “Mradi wa Hebu Tuyajenge” unaotekelezwa katika kipindi cha miaka mitano 2019-2024, unaofadhiliwa na  Shirika la Marekani  la  Maendeleo ya Kimataifa (USAID) katika mikoa 22 Tanzania Bara. kushoto Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Rahabu Mwagisa, Kulia Mkurugenzi wa Utatifi wa NACOPHA  Pantaleo Shoki

>Awataka wenye virusi kufanya kazi bila hofu
                                       >Awaonya wanaomchokoza,asisitiza hatatia nia


Na John Mapepele
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi amempongeza Rais Magufuli kwa kuvunja rekodi ya  maendeleo kabla ya mwaka 2025 na kuifanya Tanzania kuingia kwenye nchi za uchumi wa kati duniani Julai Mosi mwaka huu.  
Huku akiwahimiza watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI nchini  kufanya kazi kwa  bidii bila kuwa na hofu sambamba na kumtanguliza Mungu na kutumia fursa za mikopo inayotolewa na Serikali ya Awamu ya Tano ili  ku kuinua hali za maisha na kuongeza pato la taifa kwa ujumla

Dkt. Nchimbi ameyasema hayo leo katika Mji Mdogo wa Manyoni mkoani  Singida alipokuwa akifunga  mafunzo maalum ya  siku sita kwa wadau zaidi ya mia 3 kutoka katika mikoa mbalimbali nchini  yaliyokuwa yameandaliwa na Baraza la Taifa  la watu wanaoishi na  virusi vya UKIMWI (NACOPHA) kupitia “Mradi wa Hebu Tuyajenge”.
Mradi huo unaotekelezwa katika kipindi cha miaka mitano 2019-2024,unaofadhiliwa  na  Shirika la Marekani  la  Maendeleo ya Kimataifa (USAID) katika mikoa 22 Tanzania Bara.

Amesema kwa sasa Serikali ya Awamu ya Tano imepiga hatua kubwa ya kupiga vita unyanyapaa dhidi ya watu wanaishi na virusi vya UKIMWI na kwamba watu wote wana haki na fursa sawa  mbele ya Serikali yao hivyo hakuna sababu ya  wao kuendelea kujinyanyapaa  wenyewe  na badala yake wawe walimu wa kuwaelimisha wengine kwenda kupima na kutambua hali zao  na kuendelea kuchapa kazi ili kuinua uchumi wan chi yetu.

“Kubwa ndugu zangu hapa ni  kumtanguliza  Mungu mbele, kutoa hofu na  kuachana  na mambo yote ambayo yanapelekea  kudhoofu kwa afya zetu kama vile unywaji wa pombe  hata kama wake zetu wanapika  kwa ajili ya biashara na badala yake tutumie juisi lishe za matunda ya asili kama vile  Sasati, Ubuyu na Ukwaju” amesisitiza Dkt. Nchimbi

Umewaelekeza  Wataalam wa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Singida kuangalia namna  ya kuja na mikakati madhubuti ya kiuendelevu ya kuwakopesha wanaoishi na UKIMWI  ili kuwaletea maendeleo huku akisisitiza kuwa  Mkoa wake utaendelea kutekeleza mikakati iliyojiwekea ya kuinua maisha  ya wanainchi wake ikiwa ni pamoja na mkakati wa kuwavusha salama mama na mtoto.

Aidha ameweka msimamo wake wa kutokuonesha nia yeyote ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge katika uchaguzi wa mwaka huu huku akiwaonya watu ambao wamekuwa wakianza kudanganya kuwa atagombea ambapo alisisitiza kuwa nafasi hiyo ya ukuu wa Mkoa aliyopewa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli ni ya heshima kubwa.

“Naomba niliseme  hili, na tayari nimeshalisema mara kadhaa  hata hivi karibuni nilipokuwa nyumbani kwangu, kijijini Matufa,  Babati Manyara nilipo hudhuria mazishi ya mtoto wa Kaka yangu aliyefariki kwa ajali ya Pikipiki kwamba nilikwenda kuungana na familia yangu katika msiba wa kijana wetu na si vinginevyo. Ninaridhika sana na nafasi hii niliyo nayo ya ukuu wa Mkoa” alisema Dkt. Nchimbi huku akishangiliwa na umati wa  wadau wa mafunzo hayo

Baadhi ya waombolezaji wamesikika kupongeza msimamo wa kiongozi huyo, huku wakisema  kuwa Msimamo huo unapaswa kuigwa na viongozi wengine  kwa kuwa umejikita katika kuwaletea maendeleo wananchi badala ya kuwa na tamaa za madaraka.

“Binafsi nampongeza sana Mama Nchimbi  kwani kwa muda wote amekuwa aking’ang’ana na kuwaunganisha watu wote bila kujali dini wala rangi kwa, hata sisi leo ametutia moyo sana kiasi kwamba  baada ya kutoka hapa tumekuwa na nguvu mpya  ya kuchapa kazi na kushirikiana na Serikali yetu ya  kujiletea maendeleo Zaidi ili tutoke katika nchi za uchumi wa kati na kwenda katika nchi tajiri duniani na tuna imani kubwa chini ya Rais wetu Magufuli tutafika” amesema Amina  Huredi ambaye ni Mshiriki wa mafunzo hayo kutoka Singida

Mkurugenzi wa Utatifi wa NACOPHA  Pantaleo Shoki  amemshukuru Mkuu wa Mkoa na kumhakikishia kuwa  wataendelea kushikiana na Serikali ili kuhakikisha kuwa malengo ya Mradi huo yanatimia kama yalivyopangwa.
Shoki  amesema Mradi  unalenga kufikia Mkakati wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na UKIMWI(UNAIDS) wa 95-95-95 yaani  asilimia 95 ya watu wote wanaoishi na maambukizi ya VVU wawe wamepima na kugundua afya zao,asilimia 95 ya watu wote waliopimwa na kukutwa na maambukizi wawe wameanza tiba na asilimia 95 walio kwenye tiba wawe wamefubaza virusi hivyo ifikapo 2030