Posts

Showing posts from November, 2020

KANISA LA MORAVIAN WATAKIWA KUTORIDHIKA NA MAENDELEO WALIONAYO

Image
Mwenyekiti na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji, Yona Mwambeta, akihubiri Jumapili wakati akiongoza harambee  kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la Moraviani Usharika wa Kijichi jijini Dar es Salaam. Waumini wa kanisa hilo wakiwa katika ibada hiyo. Ibada ikiendelea. Ibada ikiendelea. Mwenyekiti na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji, Yona Mwambeta (kushoto) na  Mchungaji wa kanisa hilo Usharika wa Kijichi, Raphael Mwampagatwa wakiwa kwenye ibada hiyo. Maombi yakiendelea. Harambee ikiendelea. Kushoto ni mke wa  Mwenyekiti na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Mchungaji, Yona Mwambeta, Mchungaji Lilian Mwambeta akihesabu sh.550.000 walizotoa kama mchango wao wa ujenzi wa kanisa hilo. Mchungaji Lilian Mwambeta, akimkabidhi fedha hizo Mwenyekiti wa harambe hiyo, Subilaga Mwambeta. Waumini wa kanisa hilo na wachungaji wao wakiwa nje baada ya kuhitimisha harambee hiyo. Na Dotto Mwaibale MWENYEKIT...

MTATURU AANZA KUTEKELEZA AHADI ZA WANANCHI KWA KASI YA 4G

Image
Wachungaji na waumini wa  Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)  Usharika wa Kiaskofu Msalaba Mrefu mjini Singida, wakiwa na pikipiki walizokabidhiwa hivi karibuni na Mbunge  wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu kwa ajili ya kazi za kanisa hilo, Mbunge  wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akimkabidhi pikipiki, Mkuu wa Jimbo la Kusini Usharika wa Issuna, Mchungaji, Obedi Msele. Mbunge  wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akimkabidhi pikipiki, Mchungaji Joyce Madadi wa Usharika wa Ikungi.   Mbunge  wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akimkabidhi pikipiki, Mchungaji, Felix Kibiriti. Na Dotto Mwaibale, Singida. MBUNGE wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu ameanza kutekeleza ahadi zake kwa wananchi kwa kasi ya 4G. Mtaturu ametekeleza ahadi yake  kwa kutoa pikipiki tano kwa Usharika wa Kiaskofu Msalaba Mrefu mjini Singida ambazo alimkabidhi Mchungaji Felix Kibiriti kwa niaba ya Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT...

KAMATI YA USALAMA WILAYA YA IKUNGI SINGIDA YAKAGUA MIRADI YA ELIMU NA AFYA

Image
Wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, wakijadiliana wakati wa ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya Elimu na Afya wilayani humo. Kamati hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wake Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo. Moja ya chumba cha darasa kilicho kaguliwa na kamati hiyo. Baadhi ya madarasa yaliyokaguliwa. Muonekano wa vyoo vya Shule ya Msingi vilivyo kaguliwa na kamati hiyo. Muonekano wa baadhi ya madarasa yaliyokaguliwa na kamati hiyo. Muonekano wa baadhi ya madarasa yaliyokaguliwa na kamati hiyo. Ukaguzi ukiendelea.  Wajumbe wa kamati hiyo wakikagua ujenzi wa Chuo cha Veta. Kushoto mbele ni  Mwenyekiti wa kamati hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo. Muonekano wa ndani wa baadhi ya madarasa ya shule za sekondari yaliyokaguliwa na kamati hiyo. Muonekano wa ndani wa baadhi ya madarasa ya shule za sekondari yaliyokaguliwa na kamati hiyo. Moja ya chumba cha darasa cha shule ya sekondari kilicho kaguliwa na kamati hiyo. Jengo la Maabara lil...

SEKTA YA MISITU IKISIMAMIWA VIZURI INAWEZA KULETA MAPINDUZI MAKUBWA YA MAENDELEO KWENYE VIJIJI

Image
Muwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Nanjita Nzunda  akifungua Warsha na Mkutano Mkuu wa 20 wa Mwaka wa MJUMITA mkoani Morogoro. Mwenyekiti wa MJUMITA, Revocatus Njau akitoa nasaha zake mbele ya wajumbe kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kufungua mkutano huo. Mkurugenzi wa MJUMITA, Rahma Njaidi  akieleza malengo ya Warsha na Mkutano huo Mkuu wa 20 wa Mwaka wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.  Mkurugenzi Msaidizi wa TFCG, Emmanuel Lyimo, akitoa salamu za Shirika lake mbele ya wajumbe wa mkutano huo wa Mwaka wa MJUMITA. Wajumbe wa Mkutano huo Mkuu wa 20 wa Mwaka wa MJUMITA kutoka Kanda zote sita wakifuatilia hotuba na nasaha za ufunguzi wa mkutano huo. Wajumbe wa Mkutano huo Mkuu wa 20 wa Mwaka wa MJUMITA kutoka Kanda zote sita wakifuatilia hotuba na nasaha za ufunguzi wa mkutano huo. Wajumbe wa Mkutano huo Mkuu wa 20 wa Mwaka wa MJUMITA kutoka Kanda zote sita wakifuatilia hotuba na nasaha za ufunguzi wa mkutano huo. Wajumbe wa Mkutano huo Mkuu wa ...

SINGIDA YAWANOA WANAUSHIRIKA

Image
  Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Singida, Thomas Nyamba akiongea na Waandishi wa Habari.                    Mwenyekiti wa   Chama Kikuu Cha Ushirika  cha Wakulima Mkoa wa Singida (SIFACU LTD) Yahaya Ramadhani  akiongea na Waandishi wa Habari   Wajumbe wa Bodi na Watendaji wa   Vyama vya Ushirika  katika  Mkoa Singida  wakipewa mafunzo                             ......................................   John Mapepele na Rose Nyangasa, Singida Mkoa wa Singida umeandaa  mafunzo  ya siku  tatu ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa Bodi na Watendaji wa   Vyama vya Ushirika  katika  Mkoa ili kuwasaidia  kuacha  kufanya kazi kwa  mazoea  badala yake w...

VIJIJI VYA LIWALE MKOANI LINDI VYANEEMEKA NA UHIFADHI WA MISTU

Image
Katibu Tawala wa Wilaya  ya Liwale mkoani Lindi, Rajabu Kambangwa  akizungumza na wandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini kuhusu mchango wa sekta ya misitu kwenye wilaya hiyo. Afisa Sera na Majadiliano  wa Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA) Elida Fundi   akizungumza na waandishi wa habari walipokuwa kwenye ziara ya kuona namna Vijiji vya Darajani, Mihumo na Mtawatama zilivyofanikiwa katika jitihada za utunzaji shirikishi wa misitu. Afisa Misitu wa Wilaya ya Liwale Nassoro Ali Mzui akizungumza na waandishi wa habari kuhusu jitihada wanazozifanya kwa kushirikiana na Serikali za vijiji na wadau wengine wa misitu kwenye ulizi shirikishi wa misitu. Afisa Sera na Majadiliano  wa Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA) Elida Fundi akiwa kwenye picha ya pamoja na kamati ya maliasili ya kijiji cha Mtawatawa Wilayani Liwale.   Na Calvin  Gwabara, Liwale. ZAIDI ya shilingi milioni 957 zimepatikana kweny...

AFISA VIJANA SINGIDA AWATAKA VIJANA KUTUMIA FURSA YA MSIMU HUU WA MVUA KWA KILIMO

Image
Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani.    Na Mwandishi Wetu, Singida KAIMU Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani amehamasisha vijana mkoani hapa na kwingineko nchini kuhakikisha wanatumia fursa ya msimu huu wa mvua kujikita katika kilimo cha kibiashara ili kujiongezea kipato. Akizungumza mkoani hapa jana, Ndahani alisema anaamini kijana yeyote atakayethubutu kujiingiza katika kilimo kamwe hatajutia kutokana na faida kubwa atakayoipata. "Nawahamasisha vijana wenzangu tujitokeze tukalime, tusiiache mvua hii ikapita bure. Kwa wasio na mashamba wasisite kwenda kukodi...shamba la kukodisha gharama yake ni wastani wa kati ya shilingi elfu 25 na 30 kwa ekari moja," alisema. Alisema wakati serikali ikipambana kuhamasisha mageuzi ya kilimo ni jukumu la vijana kuhakikisha wanaunga mkono juhudi hizo kwa kutambua kilimo ndio uti wa mgongo wa uchumi wa Taifa. Ndahani alisema takribani asilimia 60 za malighafi ya viwanda vilivyopo nchini hutegemea kilimo hivyo ni ...

MEYA SINGIDA AJIVUNIA KUIACHA MANISPAA IKIWA NA HATI SAFI

Image
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida aliyemaliza muda wake, ambaye ni Diwani wa Kata ya Mtamaa mkoani hapa, Gwae Chima Mbua (katikati), akiongoza moja ya vikao vya baraza la madiwani. Na Godwin Myovela, Singida MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Singida aliyemaliza muda wake, ambaye ni Diwani wa Kata ya Mtamaa mkoani hapa, Gwae Chima Mbua, amesema mpaka sasa anajivunia kuiacha manispaa hiyo ikiwa inashikilia cheti cha hati safi kutokana na usimamizi madhubuti uliojengwa katika misingi ya nidhamu, hususan kwenye eneo la makusanyo na matumizi ya fedha za umma. Akizungumza na vyombo vya habari mkoani hapa leo, vilivyomtaka aeleze kwanini anastahili tena kupewa dhamana ya nafasi ya umeya na si diwani mwingine, alijibu kila mgombea hupimwa kwa uwajibikaji wake na sio kimitazamo wala mihemko. Alisema mpaka alipokabidhi ofisi hiyo hivi karibuni, aliacha manispaa hiyo ikiwa kwenye makusanyo ya takribani asilimia 83, sambamba na kufanikiwa kuwaunganisha madiwani na watumishi katika kuendelea kuijeng...

SPRF INAVYOSHIRIKISHA WANAFUNZI KUTOKOMEZA UKATILI

Image
Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Munkinya, Yoden Ngogo akiwakaribisha Maafisa wa Shirika lisilo la Kiserikali la Stars of Poverty Rescue Foundation (SPRF) la mkoani Singida mwishoni mwa wiki,  kuzungumza  na wanafunzi wa shule hiyo, kuhusiana na masuala yahusuyo athari za ukatili wa kijinsia. Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Munkinya wakisikiliza mafunzo ya ukatili wa kijinsia yalikuwa yakiwasilishwa na watendaji wa SPRF (hawapo pichani) Wanafunzi wa Munkinya Sekondari wakiwasilisha mpango kazi wa utekelezaji majukumu yao kuhusiana na vita iliyopo dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia. Mafunzo yakiendelea. Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Siuyu wakifuatilia mafunzo hayo. Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Ikungi, Paul Mgelwa akifuatilia mafunzo hayo, kulia ni wanafunzi wa Shule ya Sekondari  Siuyu. Mratibu wa Mradi kutoka SPRF, Mwalimu Bernard Maira akizungumza na wanafunzi wa sekondari ya Siuyu (hawapo pichani) Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Siuyu wakifuatilia ma...