STARA THOMAS, HAFSA KAZINJA KUKABIDHIWA KADI ZA MATIBABU NA WAZIRI BASHUNGWA
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa. Wanamuziki Stara Thomas na Hafsa Kazinja wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Umoja wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO), Eric Kisanga (kushoto) na Katibu Mkuu wa umoja huo, Stella Joel (kulia) baada ya kufanya mazungumzo jijini Arusha juzi kuhusu Kongamano la Fursa kwa wanamuziki litakalofanyika Februari 20, 2021 Jijini humo. Na Dotto Mwaibale. WANAMUZIKI Maarufu Nchini Stara Thomas na Hafsa Kazinja ni miongoni mwa baadhi ya wanamuziki watakao pata kadi za bima ya afya ya Taifa (NHIF) zitakazotolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa. Bashungwa ambaye atakuwa mgeni rasmi atatoa kadi hizo katika Kongamano la Fursa kwa wanamuziki litakalofanyika Februari 20, 2021 Jijini Arusha. "Mastaa hawa Stara Thomas na Hafsa Kazinja tayari wametimiza vigezo vya kupata kadi hizo za bima ya afya baada ya kukutana na Rais wa Umoja wa Wanamuzi...