Posts

Showing posts from March, 2021

ESTL YAKUTANA NA MAKUNDI MBALIMBALI NDANI YA JAMII KUJADILI NAMNA YA KUTOKOMEZA UKATILI NA UKEKETAJI SINGIDA

Image
Mratibu wa mradi wa kutokomeza ukatili na ukeketaji kutoka Shirika la   la kiserikali la Empower Society Transform Lives (ESTL) ,   Annamaria Mashaka akitoa mafunzo mbele ya watu maarufu na Mangariba wastaafu, mafunzo yaliyofanyika jana katika Shule ya Sekondari Mungumaji. Wakatikati mbele ni Mohamed Msafiri mtu maarufu, wa kwanza kulia ni Mwalimu Doris Pantaleo na kushoto ni Hamida Senge wote wakazi wa Kata ya Mungumaji wakifuatilia mafunzo. Mmoja wa watoa elimu kutoka Shirika la ESTL,  Brigita Mwaka akitoa mafunzo kwa Vijana wa Mungumaji walio nje ya Shule..  Afisa Ufatiliaji na tathimini  wa Shirika  lisilo la kiserikali la Empower Society Transform Lives (ESTL)Mkoa wa Singida, Philbert Swai, akielekeza jambo katika kikao hicho. Na Dotto Mwaibale, Singida SHIRIKA lisilo la kiserikali la Empower Society Transform Lives (ESTL)Mkoa wa Singida limekutana na makundi mbalimbali ya wakazi wa Kata ya Mungumaji kujadili namna ya kutokomeza ukatili wa ki...

TIA YAOMBA KUIDHINISHIWA BAJETI YA BILIONI 46.4

Image
Makamu Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala  wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania  (TIA)  Dkt. Modest Assenga, akisoma taarifa ya utekelezaji wa mipango na bajeti ya taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022 katika kikao cha tatu cha baraza kuu la nne la wafanyakazi wa taasisi hiyo kilichofanyika jana ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine  (SUA) mkoani Morogoro. Meneja wa TIA Kampasi ya Mtwara, Criph Swallo, akichangia jambo kwenye kikao hicho. Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi (RAAWU) Mkoa wa Mbeya Martin Mnyili, akichangia jambo kwenye kikao hicho. Picha ya pamoja ya washiriki wote wa kikao hicho.   Na Mwandishi Wetu, Morogoro TAASISI ya Uhasibu Tanzania  (TIA) inaomba kuidhinishiwa  bajeti ya Sh.Bilioni 46.4 kwa mwaka wa fedha 2021/ 2022 ili iweze kutekeleza mipango yake. Hayo yamebainishwa na Makamu Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala Dkt. Modest Assenga wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa mipango na bajeti ya taasisi hiyo kwa mwaka...

TAMUFO YAOMBOLEZA KIFO CHA DKT. JOHN MAGUFULI

Image
 Katibu Mkuu wa  Umoja  Wanamuziki Tanzania  (TAMUFO) , Stella Joel   Na Dotto Mwaibale  UMOJA wa Wanamuziki Tanzania  (TAMUFO) wametoa salamu za rambi rambi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt.John Magufuli kilichotokea Machi 17, 2021katika Hospitali ya Mzela jijini Dar es Salaam.  Salamu hizo za rambi rambi pia wamezitoa kwa Waziri Mkuu, viongozi mbalimbali, mjane wa marehemu Janeth Magufuli ,Rais wa Zanzibar na wananchi kwa ujumla. Akizungumza na waandishi wa habari Katibu Mkuu wa TAMUFO, Stella Joel alisema kifo cha Rais Magufuli wamekipokea kwa mshituko  mkubwa na kuwa watamkumbuka  milele daima. "Tunamshukuruaa Mungu kwa ajili ya maisha ya Rais Magufuli ambaye katika uongozi wake aliinua  Tasinia ya Muziki kwa kuwasaidia wasanii kwa kutatua  changamoto zao mbalimbali" alisema Joel. Alisema Rais Magufuli alifanikiwa kuzipatia ufumbuzi...

TAASISI YA WaLOTa YA MKOANI SINGIDA YAMLILIA DKT. MAGUFULI

Image
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Kuimarisha Maadili na Usaidizi kwenye Utumishi wa Umma na Sekta Binafsi (WoLaoTa), Samwel Olesaitabau, akizungumza na waandishi wa habari  (hawapo pichani)  wakati akituma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea siku ya Jumatano majira ya saa 12:00 jioni  Machi, 17/2021, katika Hospitali Nzela Dar es Salaam.  Na Dotto Mwaibale, Singida. MTENDAJI  Mkuu Taasisi ya Uboreshaji Maadili kwenye Utumishi wa Umma na Sekta Binafsi Tanzania (WoLaOTa), Samwel Olesaitabau ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea siku ya Jumatano majira ya saa 12:00 jioni  Machi, 17/2021, katika Hospitali Nzela Dar es Salaam. Akitoa salamu hizo  mbele ya wanahabari mjini hapa, Olesaitabau alisema kuwa ni tukio lililoshtua wengi maeneo mbalimbali ya nchi, ni ...

UMOJA WA DINI MBALIMBALI MKOA WA SINGIDA WAOMBOLEZA KIFO CHA JPM

Image
Mwenyekiti wa Umoja wa dini mbalimbali Mkoa wa Singida, Hamisi Kisuke, akisoma  salamu za rambirambi za umoja huo mbele ya waandishi wa habari mjini hapa kufuatia  kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Joseph Magufuli. Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Singida, Alhaji Burhan Amri Mlau akisaini katika kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa Tanzania Dkt. John  Magufuli. Alhaj Burhan amemuelezea Dkt. Magufuli kuwa ni mtu aliyetumia uwezo wake wote wa kielimu  kutafuta njia bora ya kuwatumikia watanzania na kuwainua kiuchumi. Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Singida, Elisante John, akisaini katika kitabu hicho. Mchungaji Rehema Gwao wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kati , akisaini katika kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa Tanzania Dkt. John  Magufuli. Viongozi wa dini wakisubiri kusaini katika kitabu hicho. Mwenyekiti wa Istiq...

RAIS SAMIA AANZA NA WAANDISHI WA HABARI

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akila kiapo cha uaminifu   Na John Mapepele, Dodoma Tanzania imeandika historia ya kuwa na Rais mwanamke wa kwanza kwenye nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameapishwa rasmi tarehe 19 Machi, 2021 kushika wadhifa huo kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Mhe, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi, 2021.   Kwa Mujibu wa ibara ya 37(5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kijiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana namaradhi ya mwili au  kushindwa  kutekeleza kazi za rais, basi  Makamu wa Rais ataapishwa  na atakuwa Rais kwa muda  uliobaki katika kipindi cha miaka mitano.   Mara baada ya kula kiapo Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan akiwa na majon...

KANISA LA ABC LAMPONGEZA MAMA SAMIA, LAMLILIA JPM

Image
Askofu Kiongozi wa Kanisa la ABC, Flaston Ndabila Na Dotto Mwaibale ASKOFU Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing Center (ABC) la Tabata  Mandela jijini Dar es Salaam, Flaston Ndabila kwa niaba ya waumini wa kanisa hilo wamempongeza  Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania. Mbali na pongezi hizo Askofu Ndabila ametumia nafasi hiyo kumpa pole Rais Samia Suluhu Hassani kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt.John Magufuli kilichotokea jana Hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam kwa ugonjwa wa moyo. Wengine waliyopewa pole ni mjane wa marehemu Janeth Magufuli, viongozi mbalimbali na watanzania wote kwa ujumla. Ndabila akimzungumzia Hayati Rais John Magufuli alisema watanzania watamkumbuka kwa mambo yote ya maendeleo aliyofanya. "Kila ninapofikiria mambo ambayo Mungu alimpa neema Rais wetu Magufuli kuyatenda nakumbuka vile Bwana yetu Kristo alivyo kuwa akifanya kazi zake hapa duniani." alisema Ndabila. Ndabila akimtolea mfano Yesu...

VIJANA SINGIDA WAMLILIA RAIS DR. JOHN MAGUFULI

Image
Kaimu Afisa Vijana  Mkoa wa Singida Frederick Ndahani. Mwanaharakati wa masuala ya kijamii  Mkoa  wa Singida, Stella Mwagowa Afisa Mtendaji wa Kata ya Dung'unyi  wilayani  Ikungi mkoani hapa, Yahaya Njiku.   Na Dotto Mwaibale, Singida  VIJANA mkoani hapa wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za  kifo cha Rais Dkt. John Magufuli kilichotokea Jana.  Akizungumza na waandishi  wa habari mkoani hapa jana kwa niaba ya vijana hao Kaimu Afisa Vijana  Mkoa wa Singida Frederick Ndahani alisema   watamkumbuka  Rais Magufuli kwa kuwafundisha  kuwa wazalendo wa Taifa letu. "  Vijana na  baadhi ya watanzania tulikosa uzalendo lakini Magufuli akatuhasa na kutusihi tuwe wazalendo."  alisema Ndahani. Ndahani alisema kuonesha jinsi  alivyo  kuwa akiwapenda  vijana  alitoa  nafasi nyingi za uongozi  wakiwemo wakuu wa wilaya, mikoa na baadhi  yao  aliwateua  kuwa  m...

UPATIKANA WA MAJI SAFI NA SALAMA WILAYANI MKALAMA SINGIDA KUONGEZEKA

Image
Mkuu wa Wilaya ya Mkalama (katikati kulia)  Mhandisi Jackson Masaka na Mkurugenzi Msaidizi kutoka Wizara ya Maji,  Rosemary Rwebugisa ( katikati kushoto) wakifungua kitambaa kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Maji uliopo Kata ya Nduguti Wilayani humo jana kwenye maadhimisho ya wiki ya Maji. Wananchi na viongozi wakishangilia wa uzinduzi wa mradi huo wa maji. Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Lucy Boniphace akimtwisha ndoo mkazi wa Kata ya Nduguti baada ya kuzinduliwa kwa mradi huo. Maadhimisho hayo yakiendelea. Wananchi wakiwa kwenye mkutano wa hadhara Kata ya Nduguti yalipo fanyika maadhimisho hayo.   Na Mwandishi Wetu, Singida. HALI ya upatikanaji wa Maji safi na salama katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama mkoani Singida inatarajiwa kuongezeka hadi kufikia 76.8% kutoka 65.8% ya sasa baada ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini kuchimba na kukarabati visima katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo. Meneja wa wakala huo (RUWASA) Wilaya Mhandisi ...

WANUFAIKA WA TASAF IRAMBA MKOANI SINGIDA WAOMBA WATAALAMU WA KILIMO NA MIFUGO

Image
Mnufaika wa mpango wa kunusuru Kaya Masikini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii  (TASAF) wilayani Iramba mkoani Singida, Magreth  Peter akiswaga ng'ombe wake aliowapata baada ya kuwezeshwa na mpango huo.. Mnufaika wa mpango wa kunusuru Kaya Masikini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii  (TASAF)  Magreth  Peter (kushoto) mkazi wa Kijiji cha Kengege akizungumza na viongozi wa kijiji hicho pamoja na maafisa habari kutoka TASAF makao makuu waliomtembelea kujua mafanikio yake na changamoto alizo nazo. Mnufaika wa mpango huo, Ukende  Kidyusi akiwa na wajukuu zake mbele ya nyumba yake ya kisasa aliyoijenga baada ya kuwezeshwa na TASAF. Mnufaika wa mpango huo, Joyce Mpugi akiwa na mume wake mbele ya nyumba yao ya kisasa waliyoijenga baada ya kuwezeshwa na TASAF huku wakiwa na kuku ambao ni zao lililotokana na mpango huo.. Nyumba ya tembe iliyo kuwa ikitumiwa na Mariam Danford na wazazi wake kabla ya kujengwa nyumba yao ya kisasa. Hii ni nyumba ya kisasa y...