RC SINGIDA AKABIDHI BASI HOSPITALI YA MANDEWA KWA AJILI YA KUSAFIRISHIA WAFANYAKAZI.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge. Basi namba STL 9908 lililokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge kwa ajili ya wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida. Na Mwandishi Wetu, Singida. MKUU wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge amezindua Rasmi na kukabidhi basi aina ya Coaster kwa ajili ya kusafirishia wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Mandewa iliyopo mkoani hapo kama kitendea kazi kitakachowasaidia kuongeza ufanisi katika utendaji kazi. Akizungumza na wafanyakazi akiwa Hospitalini hapo baada ya kuwakabidhi basi Mkuu wa Mkoa amewapongeza watumishi kwa namna ambavyo wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu na wengi wao wakitumia bodaboda kufika kazini lakini pia hawakukata tamaa. RC Mahenge amemtaka Afisa usafirishaji wa Hospitali ya Mkoa wa Singida kuhakikisha basi hilo linatunzwa na kuzingatia muda wa kufanyia huduma (service) kila inapofika muda wake ili kulifanya lidumu kwa muda mrefu na kuendelea kuwasaidia wat...