Posts

Showing posts from April, 2022

MWAMKO DUNI WA WAZAZI WAWAKOSESHA WATOTO CHAKULA SHULENI

Image
Ofisa Elimu Msingi katika Manispaa ya Singida, Omary Maje akifafanua jambo kuhusiana na hali halisi ya mwamko wa wazazi juu ya  uchangiaji  chakula kwa wanafunzi. Wanafunzi wakipata chakula moja ya shule za msingi. Na Abby Nkungu, Singida  MWAMKO duni wa wazazi kuwachangia chakula cha mchana watoto wao wanaosoma bado ni changamoto kubwa ambapo asilimia 66.1 ya shule za msingi za Serikali katika Manispaa ya Singida hazitoi huduma hiyo. Hali hiyo inatajwa kuathiri usikivu, umakini, uelewa na ufaulu hasa kwa watoto wasiozidi miaka minane ambao bado wanahitaji lishe bora kwa ajili ya ukuaji wa ubongo ili waweze kufanya  vyema darasani. Ofisa elimu Msingi Manispaa ya Singida, Omary Maje alisema kuwa kati ya shule 53 za msingi  za Serikali zilizopo halmashauri hiyo, 18 tu (sawa na asilimia 33.9) ndizo zinazotoa chakula cha mchana kwa  wanafunzi wake. “Manispaa hii kuna jumla ya shule 71. Shule 53 ni za Serikali, 13 binafsi na 5 za awali tu. Wenzetu wa binafsi shu...

MAJI KUVING'ARISHA KIJIJI CHA STAHABU NA MIKUNGUNI WILAYANI PANGANI MKOA WA TANGA

Image
Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Pangani, Mhandisi Willybroad Mungereza akiwa na Mkandarasi wa Mradi wa Maji Mikinguni, John Msafiri kukagua hatua ya ujnzi ulipofikia. Katibu wa Chama cha Wananchi (CUF), Wilaya ya Pangani mkoani Tanga, Ramadhan Hamad akielezea furaha aliyonayo kwa RUWASA kuwapelekea maji katika kijiji cha Stahabu Meneja wa RUWASA Mkoa wa Tanga, Mhandisi Pendo Omary akielezea waandishi wa habari namna fedha za ustawi zinavyotekeleza miradi ya maji mkoani humo. Muonekano wa nyumba ya kuweka pampu ya Mradi wa Maji Mikinguni wilayani Pangani mkoani Tanga. Muonekano wa tenki la maji kwenye Mradi wa Maji Mikinguni wilayani Pangani mkoani Tanga. Mwananchi wa kijiji cha Stahabu Wilaya ya Pangani Mkoa wa Tanga Mwanaidi Almas akielezea furaha aliyonayo baada ya RUWASA kuwapelekea mradi wa maji. Mwenyekiti wa kijiji cha Stahabu kata ya Mikinguni Mussa Mzee akielezea furaha yao kwa kitendo cha RUWASA kuwapelekea mradi wa maji. Na Selemani Msuya, Pangani WANANCHI wa Vijiji vya Stah...

SHILINGI 500 MILIONI KUMALIZA KERO YA MAJI VIJIJI VYA LWANDE NA SAGASI KILINDI TANGA

Image
Bibi Fatuma Lwande na Mjukuu wake Mwajuma Said wakisafusha ndoo ili kuchota maji Mto Kombe uliopo kijiji cha Lwande kwa matumizi ya nyumbani. Bibi Fatuma Lwande wa kijiji cha Lwande akisafisha ndoo ili kuchota maji mto Kombe kwa matumizi ya nyumbani. Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kilindi, Mhandisi Alex Odena akiangalia Jenereta ambayo itatumika kusukuma maji kuingia kwenye tenki la maji kijiji cha Lwande. Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kilindi, Mhandisi Alex Odena akiangalia Jenereta ambayo itatumika kusukuma maji kuingia kwenye tenki la maji kijiji cha Lwande. Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kilindi,Mhandisi Alex Odena akifafanua jambo kuhusu Mradi wa Maji Lwande. Zainabu Mohamedi wa kijiji cha Sagasi akielezea furaha aliyonayo kwa kupelekewa maji na RUWASA. Na Selemani Msuya, Kilindi WAKALA wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijiji (RUWASA) Wilaya ya Kilindi Mkoa wa Tanga umetumia Sh.milioni 504 za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Uviko-19 kumaliza kero ya maji kijiji cha...

SERIKALI YA AUSTRIA NA SHIRIKA LA C.I.P WAWEZESHA MAFUNZO YA LUGHA YA ALAMA WAZAZI WENYE WATOTO VIZIWI-SINGIDA

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Community Initiatives Promotion (CIP) la mkoani Singida, Afesso Ogenga akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya lugha ya alama yaliyowahusisha Wazazi na Walezi mkoani Singida jana. Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika hilo Parinemas Mashanjara akizungumza katika hafla hiyo.         Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Singida, Tumaini Christopher ambaye alikuwa mgeni rasmi aki funga mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Singida. Afisa Elimu Maalum wa Manispaa ya Singida Philipina Mboya akizungumzia umuhimu wa elimu hiyo. Afisa Elimu Kata ya Misuna, Nembris August akizungumzia mafunzo hayo na kutoa shukurani kwa shirika hilo kwa msaada mkubwa wanaotoa katika shule hiyo. Mkuu wa Shule ya Msingi Tumaini Viziwi, Francis Edward akizungumzia historia ya shule  hiyo. Hafla ya kufunga mafunzo hayo ikiendelea. Mshiriki wa mafunzo hayo Mnkwimba John akielezea faida aliyoipata kwa kupata mafunzo hay...

VIONGOZI WILAYA YA IKUNGI WAENDELEA NA MKAKATI WA KUNUSURU MSITU WA ASILI WA MINYUGHE

Image
Mhifadhi Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Samuel  Matura (kulia) akimuonesha ramani  Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Ikungi mkoani Singida  ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo, Jerry Muro (kushoto) wakati wajumbe wa kamati hiyo, walipokuwa wakikagua Msitu wa Asili wa Minyughe ambao umevamiwa na kufanyika uharibifu mkubwa wa mazingira. Wajumbe wa kamati hiyo wakipitia ramani ya msitu huo. Majadiliano yakifanyika wakati wa ziara hiyo. Safari ya ukaguzi wa msitu huo ikifanyika. Muonekano wa baadhi ya maeneo ya msitu huo. Muonekano wa mazao yaliyolimwa ndani ya msitu huo. Muonekano sehemu ya msitu huo. Magari yakichanja mbugu ndani ya msitu huo wakati wa ukaguzi. Mashamba ya alizeti yakiwa yamelimwa ndani ya msitu huo.

WIZARA YA UWEKEZAJI VIWANDA NA BIASHARA YAIPONGEZA SUA KWA TAFITI ZAKE

Image
   Naibu Waziri wa Uwekezaji Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe akifungua Warsha hiyo   Kiongozi wa Mradi huo wa  TRADE HUB nchini Tanzania Prof. Reuben Kadigi akizungumza na wadau lengo la warsha hiyo. Mhadhiri Muandamizi wa Uchumi Kilimo na Masoko Dk. Fulgence Mishili akitoa  salamu kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo.

MATOKEO YA UTAFITI WA MAJI JIJI LA DODOMA

Image
Mtafiti kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Profesa Japhet Kashaigili akifafanua jambo wakati wautoajiwa uwasilishwaji wa matoke ya utafiti wa miaka mitano wa chanzo cha maji cha Jiji la Dodoma Makutupora.   Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji kutokaWizaraya Maji Dkt George Lugomela akitoa neno wakati akifungua Warsha hiyo ya siku moja ya kupokea matokeo ya utafiti wa mradi wa GroFutures Jijini Dodoma. Mtafiti Mkuu wa Mradi huo Profesa. Richard Tayrol kutoka katika Chuo Kikuu cha jiji la London nchini Uingereza akichangia kwenye uwasilishaji wa matokeo hayo. 1 Mmoja ya wakulima ambao wamepata nafasi ya kuhudhuria Warsha hiyo kwa niaba ya wa  kulima wengine Dkt. Huruma Msuya akizungumza na SUA MEDIA nje ya Warsha hiyo. Mtafiti kutoka Chuo Kikuu cha Cardiff cha nchiniUingereza Dkt. Adrian Healy  akizungumza wakati akiwasilisha sehemu ya utafiti wake. Picha ya pamoja ya Mgeni rasmi, Watafiti pamoja na wadau wengine kutoka sekta mbalimbali walioshiriki katika warsha...