WANANCHI WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA UJENZI BANDARI YA UVUVI KILWA
Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kulia) akimuonesha Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Mhe. Mashimba Ndaki (kushoto) eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya kujenga Bandari ya Uvuvi lililopo Wilayani Kilwa Mkoani Lindi. Waziri Ndaki alitembelea eneo hilo Mei 27, 2022 kwa lengo la kulikagua kabla ya ujenzi kuanza rasmi. Akiwa katika ziara hiyo, Waziri Ndaki alisema Serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa bandari hiyo ambao utaanza mapema mwezi Juni..