Posts

Showing posts from May, 2022

WANANCHI WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA UJENZI BANDARI YA UVUVI KILWA

Image
Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kulia) akimuonesha Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Mhe. Mashimba Ndaki (kushoto) eneo  ambalo limetengwa kwa ajili ya kujenga Bandari ya Uvuvi lililopo Wilayani Kilwa Mkoani Lindi. Waziri Ndaki alitembelea eneo hilo Mei 27, 2022 kwa lengo la kulikagua kabla ya ujenzi kuanza rasmi. Akiwa katika ziara hiyo, Waziri Ndaki alisema Serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa bandari hiyo ambao utaanza mapema mwezi Juni..

WAZAZI SINGIDA WAHIMIZWA KUWALEA WATOTO KATIKA MAADILI MEMA.

Image
 Kamishina wa Chama cha Skauti Wilaya ya Singida na Afisa Vijana Mkoa wa Singida Frederick Ndahani akiwa kwenye sherehe ya Wazazi na Walezi wenye watoto wao ambao ni Skauti wilayani humo iliyofanyika jana. Mkuu wa Chuo cha VETA Mkoa wa Singida, Paul Batoleki ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika Siku ya Wazazi Wenye Watoto Skauti Manispaa ya Singida akizungumza kwenye hafla hiyo.

DC IKUNGI AONGOZA MAZISHI YA MTOTO ALIYE UAWA NA TEMBO

Image
 Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Jerry. Muro jana Mei 27/2022 amewaongoza mamia ya wananchi wa Kata ya Ntuntu kijiji cha Ntuntu Kitongoji cha Wangama katika mazishi ya mtoto Zaurati Japhari Shaban mwenye miaka miwili na miezi nane alieuwawa na Tembo majira ya asubuhi saa mbili walipokwenda kuteka maji na mama yake.

DC IKUNGI AONGOZA UTATUZI WA MGOGORO YA ARDHI KATA YA PUMA NA DUNG'UNYI

Image
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Jerry Muro (kulia) akizungumza na wananchi wakati wa utatuzi wa mgogoro wa Ardhi baina ya kata mbili za Dung'unyi na Puma katika eneo la vijiji vya Wibia na Dung'unyi katika Mbuga ya Njori mkoani Singida jana.

TAKUKURU SINGIDA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO YA ZAIDI YA SH. BILIONI 4.4

Image
Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)  Mkoa wa Singida Mzalendo Widege akitoa taarifa kwa waandishi wa habari leo Mei 25, 2022 ya kila ya robo ya mwaka inayohusu utendaji kazi wa taasisi hiyo katika maeneo matatu ambayo ni Uchunguzi, Elimu kwa Umma na Uzuiaji wa Vitendo vya Rushwa kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2022. Kulia ni Afisa wa TAKUKURU, Richard Balina. Maafisa wa TAKUKURU wakiwa katika mkutano huo wa kutoa taarifa kwa Umma kupitia vyombo vya habari.

WILAYA YA IKUNGI, KIWOHEDE KUANZA MRADI WA UJENZI WA JENGO LA MILIONI 117

Image
Mkuu wa W ilaya ya Ikungi, Jerry Muro akionesha picha inayoonesha jinsi   jengo la kisasa la MKONO SHUFAA lenye thamani ya Sh.117 Milioni litakalo jengwa na Shirika lisilo la Kiserikali la KIWOHEDE wilayani humo baada ya kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo hilo, Justa Mwaituka (kulia) ambae kwa pamoja wamekubaliana kuanza ujenzi huo wakati wowote kuanzia sasa.

MBUNGE KINGU AKAGUA ENEO ITAKAPO JENGWA SHULE SHIKIZI KIJIJI CHA MASWEYA

Image
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Abubakar Muna (katikati mwenye fulana ya blue) akiwa na Wananchi wa Kijiji cha Masweya baada ya kukagua eneo itakapo jengwa Shule Shikizi ya Kitongoji cha Nsonga Ndogo wilayani Ikungi mkoani Singida. Ukaguzi wa eneo hilo ukifanyika.

WILAYA YA IKUNGI NI SALAMA KWA WAFUGAJI NA WAKULIMA

Image
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi  Jerry Muro (wa nne kulia) akiongoza kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Ikungi kilichoketi na wananchi kwa ajili ya kumaliza mgogoro baina ya baadhi ya wafugaji kutoka Mkundi mkoani Shinyanga, Iramba na Igunga dhidi ya wananchi wa Kata ya Mwaru Kijiji cha Mdughuyu kilichoketi jana wilayani humo mkoani Singida. Aliyeketi kushoto kwa meza ni Diwani wa Kata ya Mwaru, Iddi Makangale.

DK .MAHENGE ASISITIZA UMUHIMU WA KUFIKIWA MALENGO YA CHANJO

Image
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk.Binilith Mahenge akiwa amempaka mtoto wakati akisubiri apatiwe chanjo Kata ya  Iguguno wilayani Mkalama wakati alipoongoza uzinduzi wa kampeni ya chanjo ya polio uliofanyika Mei 18,2022. Kutoka kulia ni Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali ya Mitaa (TAMISEMI) Cuthbert Kong'ola, Dk.Ritha Willilo kutoaka Shirika la Afya Duniani (WHO) Mganga Mkuu Mkoa wa Singida, Victorina Ludovick, Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Honest Nyaki, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Ibrahim Pazia na Mkuu wa wilaya hiyo, Sophia Kizigo.

TIA SINGIDA WAHITIMISHA TAMASHA LA WIKI YA MICHEZO, WAHIMIZWA KUHAMASISHA SENSA

Image
Mgeni Rasmi Afisa Vijana Mkoa wa Singida Frederick Ndahani (mwenye skafu) akimkabidhi kombe kepteni wa timu ya mpira wa miguu ya Diploma mwaka wa kwanza, Anuary Amimu (kushoto) baada ya kuibuka washindi dhidi ya Timu ya Bachelor mwaka wa pili katika Tamasha la Michezo la wiki moja la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida lililofikia tamati leo Mei 23, 2022 katika viwanja vya kampasi hiyo mjini Singida. Kulia ni Mratibu wa Tamasha hilo, Mwalimu Ambwene Kajula na Muhadhiri Flora Lemnge.  Furaha baada ya ushindi. Mshindi wa MISS TIA, Haika Amiry (katikati) akiwa na mshindi wa pili Sumaiya Adam (kushoto) na Mshindi wa Tatu, Tumaini Donald (kula) wakati wakiangalia fainali ya mpira wa miguu kati ya wanafunzi wa Diploma mwaka wa kwanza na Bachelor mwaka wa pili. Furaha ya ushindi baada ya kukabidhiwa kombe kwa Timu ya Diploma mwaka wa kwanza. Majaji wa tamasha hilo wakijitambulisha kwa staili ya kusakata Rhumba. Wanafunzi wakiwa kwenye tamasha hilo. Tamasha likiendelea. Bi...