RC SINGIDA : SUALA LA LISHE BORA KWA JAMII NI LA KUFA NA KUPONA
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, akizungumza na wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za Mkoa wa Singida wakati akitiliana saini mkataba na ikiwa ni agizo lililotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan alipokutana na wakuu wa mikoa jijini Dodoma ambapo aliwaagiza kujipanga na kuongeza jitihada za kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za lishe bora. Kaimu Afisa Lishe Mkoa wa Singida, Christoweru Barnabas akiwasilisha mpango huo. Taswira ya kikao hicho cha kutiliana saini mkataba huo. Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, (kulia)na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda wakisaini mkataba huo. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Michael Matomora. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilayaya Singida DC, Ester Chaulaakisaini mkataba huo. Viongoziwa Halmashauri ya Manispaa ya Singidawakisaini mkataba huo. Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, (kulia)na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, SophiaKizigo (kushoto) wakis...