Posts

Showing posts from November, 2022

MILA, DESTURI ,UKOSEFU WA ELIMU VIMETAJWA KUWA NI SABABU YA KUWEPO KWA VITENDO VYA UKATILI MKOANI SINGIDA

Image
p> Mmoja wa Shujaa kutoka Taasisi ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA)  akitolewa damu kwa ajili ya kuchangia akiba ya damu wakati Mashujaa kutoka SMAUJATA  walipotembelea Hospitali ya Makiungu iliyopo wilayani Ikungi kwa ajili ya kutoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili, pamoja na kuwajulia hali wagonjwa ambapo pia walifanya usafi katika maeneo mbalimbali ya Hospitali hiyo katika ziara iliyofanyika jumamosi.. Uchangiaji wa damu ukifanyika. Mashujaa wakifanya usafi kuzunguka viunga mbalimbali vya Hospitali hiyo. Usafi ukiendelea. Mashujaa wa SMAUJATA wakiwafariji wagojwa kwa kufanya maombi pamoja. Sabuni zikitolewa kwa wagonjwa. Picha ya pamoja wakati wa ziara hiyo. Na Dotto Mwaibale , Singida MILA na desturi na ukosefu wa elimu vimetajwa kuwa sababu ya kuwepo kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii kwa watoto ikiwa ni pamoja na kuendelea kuwepo kwa vitendo vya ukeketaji kwa watoto wadogo. Sababu hizo zimetolewa na wananchi wa Wilaya ya S...

TARI UKILIGURU YAELIMISHA MANUFAA KILIMO CHA PAMBA

Image
Mratibu wa zao la Pamba nchini kutoka Kituo cha Utafiti cha Kilimo Ukiliguru Dk. Paul Saidia (wa kwanza kushoto) akifuatilia tukio la utiaji saini wa mkataba wa utekelezaji wa mradi wa 'Beyond Cotton' unaolenga kuinua thamani ya zao la pamba kwenye mnyororo wa thamani kwa wilaya za Kwimba, Magu na Misungwi jijini Mwanza-unaofadhiliwa na Brazil kwa kushirikiana na Tanzania kwa gharama ya Dola 930,118 (Tsh.Bilioni 2.17) na kutekelezwa na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), Taasisi ya Utafiti wa Kilimo nchini (TARI) na Bodi ya Pamba (TCB). Wengine pichani ni wataalamu mbalimbali watakaoungana na taasisi hizo kutekeleza mradi huo. .Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), David Basley akikagua na kufanya uhakiki wa vifaa mbalimbali vitakavyotumika kufundishia wakulima wa pamba kupitia mradi huo. Mkuu wa Wilaya ya Magu Salum kali aliyevaa suti (katikati) akiwa na wataalamu mbalimbali wanaotekeleza mradi wa kuongeza thamani kwenye zao la pamba nda...

WAKULIMA WILAYA YA MAGU WAPATA MAFUNZO YA KILIMO CHA PAMBA CHENYE TIJA KUPITIA MRADI WA BEYOND COTTON

Image
Mkulima wa Kijiji cha Chandulu Wilaya ya Magu mkoani Mwanza akijifunza kupanda mbegu za pamba kwa kutumia teknolojia rahisi inayotumia muda mfupi baada ya kupata mafunzo kupitia mradi wa  ‘Beyond Cotton, unaotekelezwa na  Taasisi ya Utafiti wa Kilimo nchini (TARI), Bodi ya Pamba (TCB) na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP)

KATIBU TAWALA MKOA WA SINGIDA AKABIDHI PAMPU 13 ZA UMWAGILIAJI KWA VIJANA

Image
Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko (katikati) akikabidhi pampu 13 za umwagiliaji zinazotumia nishati ya jua kwa vikundi 13 vya  Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya  Manyoni, Itigi, Mkalama, Singida, Manispaa na Iramba zenye thamani ya Sh.Milioni 23.4 katika hafla iliyofanyika jana Shirika la Sema. Wa pili kulia mbele ni Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani.. Vifaa hivyo vikikabidhiwa. Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko (katikati) akikabidhi pampu hizo. Wa pili kutoka kushoto ni Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani. ............................................................. Na Mwandishi Wetu, Singida   KATIBU Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko  amekabidhi pampu 13 za umwagiliaji zinazotumia nishati ya jua kwa vikundi 13 vya vijana  Vijana Halmashauri ya Manyoni, Itigi, Mkalama, Singida, Manispaa na Iramba zenye thamani ya Sh.Milioni 23.4. Akizungumza na vijana hao katika Ukumbi wa Ofisi z...

KITUO KIPYA CHA AFYA KATA YA NTUNTU IKUNGI MKOANI SINGIDA KUANZA KUTOA HUDUMA

Image
Muonekano wa jengo la Kituo cha Afya cha Kata ya Ntuntu kilichopo wilayani Ikungi mkoani Singida ambacho kimetakiwa kuanza kutoa huduma za utabibu mara moja ifikapo Novemba, 28, 2022 baada ya ujenzi wake kukamilika kwa asilimia 99. Wajumbe wa kamati ya ujenzi wa kituo hicho wakifanya ukaguzi wakiongozwa na Mkurugenzi wa Huduma za Afya Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR- TAMISEMI) Dkt.Ntuli Kapologwe wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutembelea kituo hicho na kukikagua aliyoifanya wilayani humo hivi karibuni. Ukaguzi wa kituo hicho ukifanyika. Picha ya pamoja baada ya kukaguliwa kwa kituo hicho. Na Dotto Mwaibale, Singida WANANCHI wa  Kata ya Ntuntu Walayani Ikungi mkoani hapa wanatarajia kuanza kupata huduma za kitabibu katika Kituo kipya Cha Afya Cha  Ntuntu baada ya ujenzi wake kukamilika kwa asilimia 99. Akizungumza  hivi karibuni wakati wa ziara yake Mkurugenzi wa Huduma za Afya Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Of...

TIA SINGIDA YATOA SEMINA YA UJASIRIAMALI KWA WANAFUNZI ILI KUPUNGUZA CHANGAMOTO YA AJIRA

Image
 Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania, (TIA) Profesa William Pallangyo akizungumza wakati akifungua semina ya Ujasiriamali kwa wanafunzi wa taasisi hiyo ambayoitawasaidia kuanziisha biashara mbalimbali watakapomaliza masomo yao.   Semina hiyo ya siku moja ilifanyika leo katika Taasisi hiyo Kampasi ya Singida. .Mratibu wa Ujasiriliamali , Imani Matonya akizungumzia umuhimu wa semina hiyo kwa wanafunzi hao. Makamu Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu- Taaluma, D k . Momole Kasambala akizungumza katika semina hiyo. Wanafunzi wakishiriki kwenye semina hiyo. Semina ikiendelea. Mratibu wa Ujasiriamali na Kituo Atamuzi wa Kampasi ya Singida , Mohamed Kaluse (kushoto) akiwa na mratibu mwenzake kutoka Dar e Salaam wakati wa semina hiyo. Wanafunzi wa Taasisi hiyo wakiwa kwenye semina hiyo. Semina ikiendelea. Picha ya pamoja. Picha ya pamoja.  Na Dotto Mwaibale, Singida   TAASISI ya  Uhasibu Tanzaia  (TIA ) , Kampasi ya  Singida imetoa semina...

TARI, BODI YA PAMBA NA WFP WASAINI RASMI MAKUBALIANO YA KIUTENDAJI KUINUA ZAO LA PAMBA

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo nchini  (TARI) Dkt. Geofrey Mkamilo (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa WFP, Sarah Gordon-Gibson wakisaini mkataba wa ushirikiano wa kiutendaji utakaowaongoza kutekeleza programu ya kuinua tija kwenye mnyororo wa thamani wa zao la pamba na chakula lishe-ikiwemo mazao ya maharagwe, viazi, mahindi na mbogamboga kwa wilaya za Kwimba, Magu na Misungwi mkoani Mwanza-Novemba 21,2022. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo nchini  (TARI) Dkt. Geofrey Mkamilo (kulia) akipeana mkono na Mkurugenzi Mkazi wa WFP, Sarah Gordon-Gibson baada ya kusaini mkataba huo. Mwakilishi wa Bodi ya Pamba nchini (TCB), ambaye pia ni Mkurugenzi wa Huduma za Usimamizi wa bodi hiyo, James Shimbe (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa WFP, Sarah Gordon-Gibson wakisaini mkataba wa ushirikiano wa kiutendaji utakaowaongoza kutekeleza programu ya kuinua tija kwenye mnyororo wa thamani wa zao la pamba na chakula lishe-ikiwemo mazao ya maharagwe, viazi, m...

DORIS MOLLEL FOUNDATION WAPOKEA MITUNGI 200 YA GESI YA ORYX ILI KUWAPATIA WAJAWAZITO WILAYANI SERENGETI

Image
Meneja Masoko wa Kampuni ya Oryx Peter Ndomba (wa tatu kulia) akikabidhi mtungi wa gesi kwa mmoja ya wanawake wajazito wa Kata ya Rubanda kwa niaba ya wanawake wengine wajawazito wa wilaya ya Serengeti.Wa pili kulia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mary Masanja akishuhudia utolewaji wa mitungi hiyo ya gesi kwa wanawake wajawazito wa Wilaya ya Serengeti mkoani Mara.   Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mary Masanja (watatu kulia) akipokea mtungi wa gesi kutoka kwa Meneja Masoko wa Kampuni ya Oryx Peter Ndomba(wan ne kushoto).Tukio hilo limefanyika jana eneo la Rubanda wilayani Serengeti mkoani Mara wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mtoto Njiti iliyoratibiwa na Taasisi ya Doris Mollel Foundation ambayo imejikita katika kusaidia mtoto njiti na lengo la mitungi hiyo ni kuwawezesha wanawake kutumia nishati safi ya kupikia. Meneja Masoko wa Kampuni Peter Ndomba(kulia) akipokea cheti cha shukrani kutoka kwa Naibu Waziri wa Afya Dk.Godwin Mollel wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mto...