Posts

Showing posts from December, 2022

REA YAZINDUA MRADI WA KUSAMBAZA UMEME MAENEO YA VIJIJI MIJI SINGIDA, MKANDARASI AKABIDHIWA RASMI MBELE YA DC

Image
 Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili (katikati) kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida akiwasha kifaa maalumu cha kupiga king'ora kuashiria uzinduzi rasmi wa mradi mpya wa  kusambaza umeme kwenye Vijiji Miji viliyopo pembezoni mwa Manispaa ya Singida katika hafla iliyofanyika Kata ya Mwankoko Desemba 29,2022 ambao utagharimu Sh. 7.11 Bilioni zilizotolewa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) amapo  Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) litakuwa msimamizi wa mradi huo.  Na Dotto Mwaibale , Singida SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua mradi mpya wa kusambaza umeme kwenye Vijiji Miji viliyopo pembezoni mwa Manispaa ya Singida ambao utagharimu Sh. 7.11 Bilioni na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) litakuwa msimamizi wa mradi huo. Mradi huo wa kusambaza umeme katika Vijiji Miji (Peri-urban Electrification)  ambao umezinduliwa Desemba 29, 2022 Kitongoji cha Kitope Darajani Kata ya Mwankoko utatekelezwa kwenye vito...

KANISA LA ABC LATOA NGUO, MCHELE KWA WAJANE, WAGANE JIJINI DAR ES SALAAM

Image
  Askofu Mkuu wa Kanisa la ABC Tanzania lililopo Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam, Flaston Ndabila (kushoto)) akizungumza na wajane na wagane wakati wa hafla ya kukabidhi  msaada wa chakula (mchele) nguo na fedha iliyofanyika leo Desemba 26, 2022. Mjumbe wa Serikali ya mtaa wa Mandela, Tabrisa Bushiri akitoa neno la shukurani. Mke wa Askofu Ndabila, Janeth Ndabila  akitoa nguo katika hafla hiyo. Mke wa Askofu Ndabila, Janeth Ndabila akitoa msaada wa nguo katika hafla hiyo. Mjumbe wa Serikali ya Mtaa huo Juma Hassan akizungumza. Wajane wakiwa kwenye hafla hiyo. Hafla ikiendelea. Mchele ukiwa kwenye mifuko tayari kwa kugaiwa walengwa.  Nguo za aina mbalimbalizilizotolewa kwa walengwa. Picha ya pamoja baada ya kutolewa kwa msaada huo. Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam.   KANISA la Abundant Blessing Church (ABC) lililopo Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam limetoa msaada wa chakula, nguo za aina mbalimbali, viatu na fedha kwa ajili ya kuwasaidia Wagane na W...

SHILINGI 67 MILIONI KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO JIMBO LA SINGIDA MASHARIKI

Image
 Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu  akiongoza kikao cha kamati ya mfuko wa Jimbo kilichoketi jana Disemba 22, 2022 jimboni humo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ally Mwanga. Na Dotto Mwaibale,  Singida   ZAIDI ya Sh.67 Milioni zimeelekezwa kuchagiza na kuchochea miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo la Singida Mashariki. Akizungumza Disemba 22,2022 wakati akiongoza kikao cha kamati ya mfuko wa Jimbo, Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu alisema fedha hizo zinakwenda kutekeleza miradi mbalimbali kwenye jimbo hilo na akaomba zikatumike kukamilisha miradi yenye viwango na thamani halisi ya fedha hizo.  Katika hatua nyingine   Taasisi ya Tanzania Youth  Elite Community (TYEC) kwa kuutambua  uzalendo  halisi wa nchi imemtunuku tuzo ya heshima mbunge huyo ikiwa ni kutambua juhudi zake katika kuchagiza maendeleo ya wananchi jimboni humo. Katibu Mtendaji wa Taasisi hiyo Shigel...

MBUNGE SINGIDA MJINI ATOA MILIONI 5 KUCHANGIA UJENZI WA ZAHANATI

Image
 Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Mwalimu Mussa Sima (katikati) akiwa katika picha na Wazee baada ya kufanya kikao na baraza la wazeewa Kata ya Unyianga katika ziara yake aliyoifanya juzi ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo. Na Dotto Mwaibale,  Singida.   MBUNGE wa Jimbo la Singida Mjini Mwalimu Mussa Sima ametoa Sh. Milioni 5 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Zahanati ya Unyianga iliyopo Manispaa ya Singida ambapo Serikali ilitoka Sh. 50 Milioni. Ujenzi wa Zahanati hiyo umekwisha kamilika na tayari watumishi wawili wamekwisha fika ambao ni daktari na muuguzi. Akizungumza wakati wa ziara yake aliyoifanya juzi Desemba 20, 2022 ya kukagua miradi ya maendeleo Sima alisema Serikali umefanywa kazi kubwa katika jimbo kwa kutoa Fedha nyingi. Miradi aliyoitembelea na kuikagua ni ujenzi wa Shule ya Sekondari katika kata hiyo, ujenzi wa madarasa mawili shule ya Msingi ambapo alichangia Sh. 2 Milioni na kukagua ujenzi wa barabara za Kindai-Unyianga inayojengwa sambamba na mad...

AIRTEL YAIUNGA MKONO BODI YA FILAMU TANZANIA KUFANIKISHA TAMASHA LA TUZO ZA FILAMU TANZANIA 2022, JOTI AWA KINARA

Image
 Rais wa Shirikisho la Sanaa za Maonesho Tanzania Bi. Synthia Henjewele akimkabidhi Balozi wa Airtel Tanzania Lucas Mhuvile almaarufu Joti Tuzo Filamu Bora - Ucheshi (Best Comedy) kupitia Tuzo za Filamu Tanzania 2022 zilizofanyika Disemba 17, 2022 Ukumbi wa Mikutano wa  Kimataifa  wa AICC jijini Arusha. ................................................... . Na Mwandishi Wetu, Arusha. KAMPUNI ya Airtel Tanzania inayotoa huduma za mawasiliano ya simu imekuwa sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuinua Sekta ya Filamu naMichezo ya Kuigiza nchini ambapo ilikuwa moja ya Makampuni yaliyodhamini Tamasha la Tuzo za Filamu Tanzania linaloratibiwa na Serikali kupitia Taasisi yake ya Bodi ya Filamu Tanzania. Kilele cha Tamasha la Tuzo za Filamu Tanzania 2022 kimefanyika Tarehe 17 Disemba, 2022 jijini Arusha katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha - AICC,ni Tamasha la pili kuratibiwa na Serikali kupitia Bodi ya Filamu, ambapo limetoa jumla ya washindi wa Tuzo 32 ku...

WACHAKATAJI WA MAZAO YA UVUVI MKOANI KIGOMA WAPIGWA MSASA

Image
Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia masuala la Udhibiti Ubora wa Mazao ya Uvuvi na Masoko, kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bw. Steven Lukanga akizungumza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wachakataji wa mazao ya uvuvi Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma (kulia ) ni Afisa Mtaalam Mnyororo wa  Thamani wa Uvuvi na Ufugaji Viumbe Maji  Hashim Muumin. Na Devotha Songorwa, Kigoma WACHAKATAJI wa mazao ya uvuvi nchini wametakiwa kutumia fursa ya teknolojia katika shughuli zao ili kuboresha mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi na kukabiliana na upotevu wa mazao hayo katika Ziwa Tanganyika. Hayo yamesemwa na Afisa Mtaalam Mnyororo wa  Thamani wa Uvuvi na Ufugaji Viumbe Maji  Hashim Muumin  wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wachakataji, wavuvi na  wafanyabiashara yaliyoandaliwa na Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kupitia miradi yake ya  FISH4ACP  na Flexible Multi-partner Mechanism (FMM) mafunzo ...

MBUNGE SINGIDA MJINI MUSSA SIMA ADHAMINI NA KUZINDUA LIGI YA MINGA CUP

Image
Mbunge  wa Jimbo la Singida Mjini Mussa Sima akizungumza wakati wa uzinduzi wa mashindano ya ligi ya mpira wa miguu ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Kata ya Minga yajulikanayo  Minga Cup katika hafla iliyofanyika jana Desemba 19, 2022 Uwanja wa Shule ya Msingi Minga Manispaaya Singida.. Mbunge Sima akimtambulisha Diwani wa Kata ya Mwankoko, Emmanuel Emadaki ambaye alikuwa ameongozana naye kwenye uzinduzi wa mashindano hayo. Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Minga, Masanja Christopher akizungumza wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo. Diwani wa Kata ya Minga, Ibrahim Mrua akizungumza wakati wa uzinduzi huo. Mbunge wa Singida Mjini Mussa Sima akimkabidhi mpira Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Minga, Masanja Christopher. Mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji na washiriki wa uzinduzi wa mashindano hayo.  Na Dotto Mwaibale, Singida.   MBUNGE wa Jimbo la Singida Mjini Mussa Sima amedhamini na kuzindua ma...