KATIBU TAWALA SINGIDA: WAANDISHI WA HABARI KUWENI WAZALENDO KWA KUANDIKA HABARI ZENYE TIJA
Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dorothy Mwaluko (kushoto) akifungua mkutano wa Uhamasishaji wa Program ya Shule Bora kwa Wasimamizi wa vyombo vya habari na Wahariri Mkoa wa Singida uliofanyika leo Januari 31, 2023 wilayani Manyoni mkoani hapa. Na Dotto Mwaibale , Manyoni WAANDISHI wa Habari Mkoa wa Singida wametakiwa kuwa wazalendo kwa kuandika habari zenye tija kwa mkoa na Taifa kwa ujumla . Wito huo umetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dorothy Mwaluko wakati akifungua mkutano wa uhamasishaji wa program ya Shule Bora kwa Wasimamizi wa vyombo vya habari na Wahariri Mkoa wa Singida uliofanyika leo Januari 31, 2023 wilayani Manyoni mkoani hapa. “Waandishi wa habari mnatakiwa muwe wazalendo kwa kuandika habari nyingi za maendeleo ili kuutangaza mkoa wetu na si kuandika zile zinazohusu mabaya tu japo hazikatazwi” alisema Mwaluko. Aidha Mwaluko aliwataka wanahabari kwenda vijiji kuandika habari za uchunguzi ambazo zitasaidia kuibua changamoto za wananchi, watumishi wa afya n...