WANANCHI IBOFWE WAMBEBA MBUNGE NYAMOGA WAKISHUKURU KWA UJENZI WA ZAHANATI, BARABARA
Wananchi wa Kijiji cha Ibofwe, Kata ya Irole wilayani Kilolo mkoani Iringa wakiwa wamembeba Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Justine Nyamoga ikiwa ni kuonesha shukurani zao baada ya mbunge huyo kufanikisha ujenzi wa Zahanati na Barabara katika kijiji hicho. Mbunge Nyamoga alibebwa leo wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika kijiji hicho. Na Mwandishi Wetu, Kilolo, Iringa Awali, wananchi wa Kijiji cha Ibofwe, Kata ya Irole Wilayani Kilolo walimuomba Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Justine Nyamoga ashuke kwenye gari kisha wakampakia kwenye bodaboda. Ilipobaki umbali wa kama kilometa moja hadi kufika eneo la mkutano, wananchi hao wakamuomba ashuke kwenye bodaboda ili wambebe. Haikuwa rahisi kwake kukubali kubebwa lakini kwa sababu yalikuwa ndiyo mapokezi ya wanakijiji, hakuwa na budu kukubali. "Mbunge wetu, kikosi cha mapokezi kipo tayari kukubeba, sisi wananchi tumeamua kukubeba na usihofi hatutakuangusha," alisema mmoja wao huku akipiga saluti. Mwen...