Posts

Showing posts from March, 2023

SINGIDA YAJIDHATITI KUTUMIA MFUMO WA MSHITIRI KUPATA BIDHAA ZA AFYA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba akizungumza na wadau wa Sekta ya Afya wakati akifungua mafunzo ya wawezeshaji wa Mfumo Mshitiri kutoka Halmashauri Saba za mkoa huo katika mkutano uliofanyika mjini hapa Machi 30, 2023. Kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida, Victorina Ludovick na kulia ni  Mwezeshaji wa kitaifa wa mfumo huo kutoka Wizara ya TAMISEMI, Emmanuel Mayunga, Na Dotto Mwaibale, Singida MKOA  wa Singida umeendelea kujidhatiti na kuongeza ufanisi katika upatikanaji wa huduma bora za afya kwa kutekeleza afua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutumia mfumo wa Mshitiri kwa bidhaa za afya zinazokosekana Bohari ya Dawa (MSD). Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba wakati akifungua mafunzo ya wawezeshaji wa Mfumo Mshitiri kutoka Halmashauri Saba za mkoa huo ambazo ni Itigi, Iramba, Singida Manispaa, Ikungi, Manyoni, Singida DC na Mkalama. “Kutokana na changamoto na kuibuka kwa hoja mbalimbali za ununuzi wa bidhaa za afya vituoni, Ofisi ya ...

SUA KUJA NA MAPENDEKEZO YA SERA BORA ZA BIASHARA YA MAZAO YA KILIMO NA NYAMA PORI NCHINI.

Image
Kaimu Rasi wa Ndaki ya Uchumi Kilimo na stadi za Biashara Dkt. Zena Mpenda akifungua warsha ya Wadau wa Mradi wa TRADE HUB kujadili matokeo ya utafiti.  Na Amina Hezron, Morogoro   WADAU wa zao la Soya kahawa miwa na nyama pori wametakiwa kushiriki kikamilifu kwenye kutoa mapendekezo  na maoni yao kwenye Mradi wa Utafiti wa Biashara,Maendeleo na Mazingira (TRADE Hub) ili matokeo yatakayopatikana yaweze kuinua tija ya mazao hayo nchini. Hayo yameelezwa na Kaimu Rasi wa Ndaki ya Uchumi Kilimo na stadi za Biashara Dkt. Zena Mpendu aliyemuwakilisha Rasi wa Ndaki hiyo Dkt Damas Philip katika  warsha iliyoandaliwa na mradi huo ili kuwasilisha matokeo ya awali ya utafiti wao kwa wadau ili kupata maoni yao  juu ya namna bora ya kufanya biashara ya haki na endelevu. Amewataka wadau hao kuzingatia kuwa tasnia hizo zinagusa kwa namna moja ama nyingine maisha na maendeleo ya wadau mbalimbali pamoja na uchumi na maendeleo ya nchi kwa ujumla hivyo watumie fursa hiyo kwa makin...

RC SINGIDA ATAKA WANANCHI KULIPA BILI ZA MAJI KILA MWEZI ILI KUISAPOTI SUWASA GHARAMA ZA UENDESHAJI

Image
Mkuu  wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (wa pili kushoto) na viongozi mbalimbali wakivuta pazia kuashiria uzinduzi  wa mradi wa maji wa Kata ya Unyambwa uliogharimu zaidi ya Sh.Milioni 622 ambao utawanufaisha wananchi zaidi ya 6120 wa vijiji vya kata hiyo.   Na Dotto Mwaibale, Singida   MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba amehimiza watumiaji wa maji k ulipa ankara za maji kila mwezi bila kulaza ili kuiwezesha Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Singida (SUWASA) iweze kumudu gharama mbalimbali za uendeshaji, matengenezo na sehemu ya uwekezaji.   Serukamba ameyasema hayo leo Machi, 17,2023 wakati akizindua  mradi wa maji wa Kata ya Unyambwa uliogharimu zaidi ya Sh.Milioni 622 ambao utawanufaisha wananchi zaidi ya 6120.   Serukamba alisema wananchi mbali na kulipa ankara za maji kwa wakati pia wajiepushe na vitendo vya wizi wa maji kwani jambo hilo linaongeza mzigo wa gharama  kwa SUWASA na wateja wake.   Aidha, Serukamba alitaja ...

KAMATI YA BUNGE PAC YARIDHISHWA MRADI WA KIWANDA CHA MIPIRA YA MIKONO CHA MSD

Image
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya  Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Japhet Hasunga, akizungumza wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi wa kiwanda cha mipira ya mikono cha Bohari ya Dawa (MSD) kilichopo Idofi-Makambako mkoani Njombe.  Na Mwandishi Wetu, Njombe KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imesema imeridhishwa na maendeleo ya mradi wa kiwanda cha mipira ya mikono cha Bohari ya Dawa (MSD) kilichopo Idofi-Makambako mkoani Njombe na kuahidi kuishauri serikali kuongeza bajeti ya shilingi bilioni 12, kuwezesha mradi huo kukamiloka kuanza kazi ifikapo Julai mwaka huu. Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya PAC Japhet Hasunga, amesema kamati imeishauri bodi ya Wadhamini MSD na Menejimenti kuwa wabunifu kufikia adhma ya serikali ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kufikia  uchumi wa viwanda. Amesema kutokana na tathimini ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), inaonyesha ujenzi wa kiwanda hicho umefikia asilimia 70, ambapo kamati imeona haja kwa hatua ziliz...

MAFUNDI 1800 KUKUTANA KWENYE KONGAMANO MJINI IRINGA MACHI 17, 2023

Image
Mafundi umeme wakiwajibika sehemu ya mafunzo. Na Mwandishi Wetu, Iringa ZAIDI ya mafundi 1800 wa aina mbalimbali wanatarajia kukutana pamoja katika kongamano kubwa litakalo fanyika Mjini Iringa lengo kubwa likiwa kupanua wigo wa ajira na kuongeza fursa kwenye kundi hilo muhimu kwenye jamii. Meneja wa FundiSmart, Fabian Mwiga amesema kongamano hilo litafanyika Machi 17, 2023 katika ukumbi wa Masiti, Manispaa ya Iringa. Kiuhalisia, mafundi ni kati ya kundi lililoachwa pembeni licha ya kuwa vitu vingi zinavyoizunguka dunia vinatokana na uwepo wa fundi.  “Tunawakutanisha mafundi mbalimbali bila kujali aina ya ufundi wao, mpaka sasa tunao mafundi 1800 waliojiandikisha,” amesema Mwiga. Amesema kwenye kongamano hilo mafundi watapata fursa ya kujua umuhimu na thamani ya kazi yao, elimu ya afya na bima, fedha, sheria, akiba na huduma bora kwa wateja. “Sekta ya ufundi ni nyeti na mafundi wanazo ndoto zao, sasa wanaweza kufikia ndoto zao ikiwa tutawaonyesha mlango wa kupita, FundiSmart imekuj...

TACAIDS YAWASILISHA TAARIFA KUHUSU MUUNDO NA MAJUKUMU YAKE KWA KAMATI YA BUNGE AFYA NA UKIMWI

Image
     Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge na Uratibu,  Mhe George Simbachawene    akizungumza na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI walipokutana na TACAIDS wakati wa wasilisho la muundo na majukumu ya TACAIDS kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika Ukumbi wa Ofisi za Bunge jijini Dodoma, Leo Machi,12, 2023. Na Nadhifa Omar, Dodoma. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe.George Simbachawene amesema Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu itaendelea kutoa ushirikiano unaostahiki kwa kamati ya Afya na masuala ya UKIMWI kutekeleza majukumu kwa kufuata miongozo,maoni na ushauri unaotolewa na kamati hiyo. Kauli hiyo amaitoa leo Machi12 ,2023 baada ya Tume ya kudhibiti UKMWI Tanzania (TACAIDS) kuwasilisha Taarifa kuhusu muundo na majukumu yake kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika Ukumbi wa Ofisi za Bunge jijini Dodoma. Awali akiwasilisha taarifa hiyo Mkurugen...

KATAMBI: HALMASHAURI ACHENI URASIMU MIKOPO MNAYOTOA KWA VIJANA, WANAWAKE NA WALEMAVU

Image
Naibu  Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu,   Patrobas Katambi, akiwa ameshika keki maalumu aliyoandaliwa na Wanafunzi wa Chuo cha Ufundi na Marekebisho kwa watu wenye Ulemavu Sabasaba-Singida  wakati wa ziara yake mkoani hapa ya kukagua shughuli mbalimbali zilizo chini ya wizara yake. Na Dotto Mwaibale, Singida NAIBU Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu,  Patrobas Katambi, amezitaka Halmashauri za Wilaya na Manispaa nchini kuacha urasimu wa kutoa fedha zilizotolewa kwa vikundi vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu zinazotokana na asilimia 10 ya mapato ya halmashauri hizo. Katambi alitoa maagizo hayo juzi katika ziara ya kukagua miradi inayotekelezwa inayotokana na asilimia 10 za mapato ya halmashauri wakati akizungumza na viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Ikungi mkoani hapa. Hatua ya Katambi kutoa maagizo hayo ilifuatia baada ya Mwenyekiti wa Kikundi cha Vijana Chapa Kazi, Mwanahamisi Omari, k...