Posts

Showing posts from April, 2023

BOHARI YA DAWA (MSD) KANDA YA KATI YAKUTANA NA WADAU WAKE KATIKA KIKAO KAZI

Image
Meneja wa Bohari ya Dawa (MSD)  Kanda ya Kati, John Sipendi, akizungumza na wadau wa MSD katika kikao kazi kilichofanyika wilayani Kondoa mkoani humo Aprili, 29, 2023. .............................................................  Na Mwandishi Wetu, Dodoma  BOHARI ya Dawa (MSD) Kanda ya Kati Dodoma imekutana na wadau na wateja wake wakiwemo waganga wakuu, wafamasia na watendaji wa halmshauri kuhakikisha wanajadili uboreshaji wa huduma za afya na upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa uhakika ili kupunguza kero kwa wananchi.  Katika mkutano huo wadau hao wamekubaliana kuunga mkono jitihada za Rais Dk.Samia Suluhu Hassan za maboresho sekta ya afya kwa vitendo kwa kutumia taaluma zao kutoa huduma stahiki.  Akizungumza jana wilayani Kondoa mkoani Dodoma Meneja wa MSD Kanda ya Kati, John Sipendi alisema, lengo la MSD kurejesha mikutano hiyo ya pamoja na wadau ni kukubali kukoselewa, kujenga mazingira ya kupunguza changamoto za pande zote mbili, kubadilisha uzoefu na ...

TAASISI YA PROFESSOR MWERA FOUNDATION YAWAOMBA WALIMU SINGIDA KUANZISHA MFUKO WA ELIMU

Image
Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara,Hezbon Mwera, akizungumza na wadau wa sekta ya elimu na walimu katika mkutano wa wadau wa elimu 2023 Mkoa wa Singida uliofanyika Aprili 27, 2023. Na Dotto Mwaibale , Singida MKURUGENZI  wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara, Hezbon Mwera amewaomba walimu Mkoa wa Singida kuanzisha mfuko wa elimu ambao utasaidia kwa shughuli mbalimbali katika sekta ya elimu. Mwera alitoa ombi hilo jana wakati akizungumza na walimu hao kwenye mkutano wa wadau wa elimu mkoa wa Singida  wa mwaka 2023 uliofanyika Aprili 27, 2023, Ukumbi wa Social Mission mjini hapa. “Nashauri kila halmshauri za mkoa wa Singida kwa kuwashirikisha wadau wengine anzisheni mfuko wa elimu ambao utakuwa ukisaidia kuboresha masualayote yanayohusu elimu katika maeneo hayo na mkoa wa Singida kwa ujumla,” alisema Mwera. Akizungumzia suala la upatikanaji wa chakula mashuleni alisema jambo hilo ...

TANESCO SINGIDA YATOA FUTARI KWA MAKUNDI MBALIMBALI KWA AJILI YA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

Image
Viongozi mbalimbali wa Ofisi ya Sheikh Mkoa wa Singida, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) baada ya kupokea msaada wa futari  kutoka shirika hilo kwa ajili ya kuwasaidia watu mbalimbali wakiwepo wenye mahitaji maalum. Dotto Mwaibale na Hamis Hussein - Singida SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO )  Mkoa wa Singida limetoa Sadaka ya Futari kwa  Wajane, Yatima, Wazee na watu wengine wenye mahitaji maalum mkoani hapa. Akizungumza kwa niaba ya Meneja wa Tanesco  Mkoa wa Singida Afisa Usafirishaji wa shirika hilo, Juma Omary alisema shirika hilo limeitikia wito wa Ofisi ya Sheikh wa Mkoa wa Singida ambayo ambaye alitoa wito kwa wadau mbalimbali kusaidia makundi mbalimbali yenye uhitaji katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. “Leo tupo katika tukio  muhimu la kuwasaidia wenzetu wenye mahitaji,  Sheikh wa Mkoa alitupa ujumbe ili tusaidie jambo hilo  kwa kuwa shirika letu linashughulika na kuhud...

WAZIRI ULEGA AKABIDHI MADUME YA NG'OMBE KWA VIKUNDI VYA WAFUGAJI WILAYA YA MKALAMA

Image
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akiswaga ng'ombe katika hafla ya kukabidhi madume bora 40 ya ng'ombe  kwa vikundi vya wafugaji wilayani Mkalama mkoani Singida Aprili, 6, 2023. Na Dotto Mwaibale, Mkalama   WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, amekabidhi madume bora 40 ya ng'ombe kwa vikundi vya wafugaji wilayani Mkalama mkoani Singida ukiwa ni mkakati wa serikali wa kufanya mabadiliko ya sekta mifugo wenye lengo la kuboresha mbari za mifugo ili kuwa na mifugo yenye tija zaidi. Akikabidhi ng'ombe hao jana katika hafla iliyofanyika Kijiji Cha Iguguno wilayani hapa, alisema serikali imenunua madume ya ng'ombe 366 kwa thamani ya zaidi ya Sh.Milioni 878.4 ambao watagawiwa wafugaji kwenye halmashauri nane nchini. Ulega alisema baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kufungua milango, nchi nyingi zimekuwa zikihitaji nyama kutoka Tanzania lakini bahati mbaya ng'ombe za asili zinazofugwa na wafugaji hapa nchini hazina uzito nyingi zinakuwa kati ya kilo 80 hadi...

MSD YAANDAA SEMINA KWA WAHARIRI VYOMBO VYA HABARI, KUFANYIKA JIJINI DODOMA

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Mavere Tukai   Na Dotto Mwaibale, Babati BOHARI ya Dawa (MSD) imeandaa Semina maalum kwa Wahariri wa vyombo vya habari nchini itakayofanyika kwa siku mbili mkoani Dodoma. Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai imeeleza kuwa semina hiyo itaanza kesho Aprili 5, 2023 na kufikia tamati kesho kutwa Aprili 6, 2023 na kuwa itafanyika katika Ukumbi wa Tume ya Uchaguzi  mkoani humo. "Lengo la semina hii ni kuwajengea uelewa kuhusu majukumu ya MSD ambayo ni manne ya kuzalisha, kununua, kutunza na kusambaza bidhaa za afya nchini sambamba na maboresho mbalimbali yanayofanywa na taasisi hiyo kupitia mpangomkakati wake wa muda mfupi na mrefu" alisema Tukai. Tukai alisema mbali na kuwajengea uelewa Wahariri juu ya majukumu na maboresho ya MSD, semina hiyo pia itatoa fursa kwa MSD kutoa ufafanuzi juu ya masuala kadhaa ambayo yamekuwa yakijitokeza kwenye jamii, kufanya ziara naokwenye maghala ya MSD kuangalia mfumo ...

KAMATI YA BUNGE PIC YAIPA KONGOLE REA KWA KASI YA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI

Image
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee PIC), Augustino Vulu, akizungumza wakati kamati hiyo ilipotembea mradi huo wa kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili (R3R2) katika vijiji vya Irisya, Masutianga na Munyu vilivyopo Wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida, Aprili Mosi, 2023. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy. Na Dotto Mwaibale, Singida KAMATI ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (Public Investment Committee PIC) imewapongeza  Wakala wa Nishati Vijijini (REA)  kwa mradi wa usambaji wa a umeme katika vijiji vitatu vilivyopo Wilaya ya Ikungi mkoani Singida.. Vijiji vilivyonufaika katika mradi huo ni Munyu, Irisya na Masutianga vyote vikiwa Kata ya Irisya wilayani humo. Wajumbe hao wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa PIC, Augustino Vulu wametoa pongezi hizo Aprili 1, 2023 baada kutembelea mradi huo wa kusambaza Umeme Vijijini Awamu ...