DC IRAMBA AGUSWA NA ADHA YA WANANCHI KIJIJI CHA MSAI KUKOSA ZAHANATI
Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda (katikati) akishiriki kufyatua matofali wakati wa mfululizo wa ziara yake ya kikazi ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo aliyoifanya Kata ya Shelui na Mtoa wilayani humo jana May 29, 2023 akiwa ameongoza na wataalam, watendaji wa Kata na Tarafa pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama. ...................................................... Na Mwandishi Wetu, Iramba MKUU wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amesema atafanya mawasiliano na wahusika wa sekta ya afya ili ziweze kupatika fedha za kumalizia ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Msai Kupatikana kwa fedha hizo na kukamilika kwa ujenzi wa zahanati hiyo kutawaondolea adha wananchi ya kutembea umbali mrefu kwenda kupata huduma za matibabu maemo mengine. Mwenda ameyasema hayo wakati alipokuwa kwenye ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika Kata yaMtoa na Shelui pamojana kusikiliza kero za wananchi ili kuzitafutia u...