DC SINGIDA : WAFANYABIASHARA VIPODOZI SHIRIKIANENI NA SERIKALI KATIKA KUDHIBITHI VIPODOZI VYENYE SUMU
Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhandisi Paskas Muragili, akizungumza na Wafanyabiashara wa Vipodozi Mkoa wa Singida Julai 27, 2023, wakati akifungua kikao cha TBS na wafanyabiashara hao cha kutoa elimu juu ya uelewa kuhusu vipodozi vyenye viambata sumu. ....................................................... Na Dotto Mwaibale, Singida MKUU wa Wilaya ya Singida, Mhandisi Paskas Mragili amewataka wafanyabiashara wa vipodozi mkoani hapa kushirikiana na Serikali pamoja na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kudhibiti bidhaa zenye viambata vyenye sumu. Mragili alitoa ombi hilo wakati akifungua kikao cha TBS na wafanyabiashara cha kutoa elimu juu ya uelewa kuhusu vipodozi vyenye viambata sumu Mkoa wa Singida. Hatua ya TBS kutoe elimu hiyo ilifuatia maombi yaliyotolewa na wafanyabiashara hao kwa Mkuu wa Wilaya ya Singida Mwezi Mei, 2023 wakati maafisa wa TBS walipoanzisha operesheni ya kupita katika maduka ya vipodozi kwa lengo ya kuondoa bidhaa hizo katika soko ambazo zinaathari kwa binadamu....