BENKI YA CRDB YAJA NA HATIFUNGANI YA KIJANI
Na Selemani Msuya WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo ametoa rai kwa wananchi, kampuni za sekta binafsi na umma, taasisi za serikali kutoka ndani na nje ya nchi kuwekeza katika hatifungani ya kijani au “Green Bond” ya Benki ya CRDB. Profesa Kitila ametoa raia hiyo leo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Hatifungani ya Kijani uliofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na watu wa kada mbalimbali wa ndani na nje ya nchi. Amesema uamuzi wa Benki ya CRDB kuja na hatifungani hiyo ya kijani na kutoa fursa kwa wananchi na taasisi mbalimbali kununua hisa na fedha zitakazopatikana kuelekezwa kwenye miradi ya mazingira ni wa kuigwa na taasisi nyingine kwani unaenda kusaidia serikali kutekeleza miradi mingi. Kitila amesema serikali ina mipango mingi ya kuhakikisha miradi ya kuzuia uharibifu wa mazingira unaosababishwa mabadiliko ya tabianchi kutokea, hivyo ujio wa Kijani Bond ni wazi kuwa lengo hilo litaweza kutumia. "Kijani Bond i...