WILAYA YA MKALAMA WAPOKEA MWENGE WA UHURU 2023 KUTOKA IRAMBA, WAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI
Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moses Machali (kulia) akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda baada ya kumaliza mbio zake wilayani humo Septemba 23, 20223 katika makabidhiano yaliyofanyika Viwanja vya Chuo cha Ufundi cha FDC kilichopo Kata ya Msingi wilayani humo. .............................................................................. Na Dotto Mwaibale, Mkalama WILAYA ya Mkalama mkoani Singida imepokea Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 kutoka Wilaya ya Iramba mapokezi yaliyofanyika Septemba 23, 2023 Kata ya Msingi wilayani humo na kupongezwa kwa utekelezaji wa miradi ambapo kesho alfajiri Septemba 24, 2023 utakabidhi mbio hizo Wilaya ya Singida DC. Akizungumza wakati akiupokea Mwenge wa Uhuru, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moses Machali alisema ukiwa wilayani humo utatembelea, utakukagua, kufungua, kuzindua na kuweka jiwe la msingi kwenye miradi mbalimbali yenye thamani ya Sh. Bilioni 1.7. " Mwenge wa Uhuru ukiwa katika wilaya yetu uta...