TAKUKURU SINGIDA YAOKOA ZAIDI YA SH.MILIONI 156 ZA MIRADI YA MAENDELEO
Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Mkoa wa Singida, Sipha Mwanjala akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Januari 31, 2024 ya utendaji kazi kwa kipindi cha Oktoba hadi Desemba 2023. ............................................................ Na Dotto Mwaibale, Singida TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Mkoa wa Singida imeokoa zaidi ya Sh.Milioni 156 baada ya kufuatilia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida, Sipha Mwanjala akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Januari 31, 2024 ya utendaji kazi kwa kipindi cha Oktoba hadi Desemba 2023 alisema miradi iliyofuatiliwa ilikuwa ni 11 yenye thamani ya zaidi ya Sh.B ilioni 5 katika sekta za Elimu na Afya. Mwanjala alisema miradi hiyo inajumuisha ujenzi wa Shule za Sekondari za Kutwa na za Kata iliyotekelezwa kupitia mradi wa kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) ambao unahusisha ujenzi na ukarabati wa Shule za Sekondari...