KUNA UMUHIMU WA MIFUKO YA KUHIFADHIA DAMU KUDUMU KWA MUDA WA MIEZI 5 MPAKA 9
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Mavere Tukai ........................ Na Mwandishi Wetu. BOHARI ya Dawa (Msd), imesema kuna haja ya kuwa na akiba ya mifuko ya kuhifadhia damu itakayodumu kwa kipindi cha kuanzia miezi mitano hadi tisa, kuepuka kuadimika kwa bidhaa hizo. Kauli hiyo ya MSD inakuja katika kipindi ambacho, akiba ya mifuko hiyo kwa sasa ni miezi mitatu, jambo linalopaswa kuongezeka kutokana na ongezeko la mahitaji ya damu linalosababishwa na ajali. Akizungumza jana Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wataalamu wa Maabara, alisema MSD inaona kuna haja ya kutafuta mbinu thabiti itakayowezesha kuwa na akiba kubwa ya mifuko na hivyo kuwa na uhakika wa upatikanaji wa damu salama kwa wananchi. Alisisitiza kuwa, damu ni suala linaloamua maisha ya watu na mahitaji yake ni muhimu hasa kwa wajawazito, hivyo kuna haja ya kuhakikisha inapatikana kwa uhakika. Katika kufanikisha hilo, alisema kuna h...