SERIKALI YATOA SH.173 MILIONI KWA AJILI YA MAFUNZO YA UFUNDI KWA VIJANA SINGIDA.
Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Musa Sima, akionesha umahiri kwa kushona nguo wakati alipotembelea chuo cha ufundi na marekebisho kwa watu wenye ulemavu cha Sabasaba (VTC) kilichopo Kata ya Utemini mjini hapa.. Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Musa Sima, akizungumza na wanafunzi wa chuo hicho. Mkuu wa chuo hicho, Fatuma Malenga akizungumzia juu ya utekelezaji wa program ya kukuza ujuzi kwa vijana inayofadhiliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu. Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Musa Sima, akimsalimia kwa unyenyekevu mkubwa mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho. Na Dotto Mwaibale, Singida. SERIKALI imetoa Sh.173.7 kwa ajili ya gharama ya mafunzo ya ufundi kwa vijana mkoani hapa. Hayo yamesemwa jana na Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Musa Sima wakati alipotembelea chuo cha ufundi na marekebisho kwa watu wenye ulemavu cha Sabasaba (VTC) kilichopo Kata ya Utemini mjini hapa. Akiwa chuoni hapo Sima aliweza kuzungumza na vijana 70 wanaopata el...