DC WILAYA YA KALIUA AWATAKA VIJANA KUTUMIA VYAKULA VYENYE LISHE KUKABILIANA CHANGAMOTO YA NGUVU ZA KIUME
Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Dk. Rashid ChuaChua akigawa vyandarua vyenye dawa vilivyotolewa na Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) kwa ajili kukabiliana na ugonjwa wa malaria wilayani humo.
Na Mwandishi Wetu, Kaliua
MKUU wa Wilaya ya Kaliua Dk. Rashid ChuaChua
amewataka wananchi wa Wilaya hiyo hususani vijana kutafuta mbadala wa tatizo la
nguvu za kiume ikiwemo kuzingatia vyakula vya lishe na kuacha kisingizio kuwa
matumizi ya vyandarua vyenye dawa ndio chanzo.
Amesema upendo hekima na huruma ya Rais Dk. Samia
Suluhu Hassan kunusuru wananchi wake kwa kusambaza vyandarua katika wilaya hiyo
ni juhudi ambazo haziwezi kufifishwa na imani potofu.
Akizungumza jana mkoani Tabora wilayani Kaliua
Dk. Rashidi amewataka wananchi hao hususani vijana kutafuta mbadala wa tatizo
la nguvu za kiume, ikiwemo kuzingatia vyakula vya lishe na kuacha kisingizio
kuwa matumizi ya vyandarua vyenye dawa ndio chanzo.
“Kama mashine haifanyi kazi haifanyi tu sio kwa
sababu ya kutumia vyandarua vyenye dawa, tutafute chanzo cha wanaume wengi kuwa
na changamoto ya nguvu za kiume, sisi
wengine tumetumia hivyo vyandarua miaka na miaka na hadi watoto zetu
wanatumia na hatuna hiyo shida,”alisema.
Alieleza, ujio wa vyandarua hivyo ni muhimu hivyo
wananchi wanatakiwa kuunga mkono jitihada hizo lengo ni kujilinda dhidi ya
malaria ambayo ni tishio.
Alithibitisha ya kwamba Tabora ikiwa ni ya kwanza
kitaifa kwa maambukizi ya malaria, Kalihua ni miongoni mwa wilaya zinazoongoza
mkoani humo kutokana na maambukizi ya ugonjwa huo.
Alisema,
uchunguzi wa afya unaonyesha kati ya watoto 10 saba wana maambukizi ya
malaria hatua ambayo serikali imeona ipo haja kuongeza nguvu katika mapambano
hayo ili kuwa na watu wenye afya njema.
“ Wapo watu hawana uelewa wanapotosha jamii na
kusema vyandarua hivyo vinapunguza nguvu za kiume, hakuna ukweli wa dawa
zinazotumika kuzuia mbu katik vyandarua kupunguza nguvu naomba mjue kuwa malaria ni hatari
hivyo, nawasihi wananchi tumieni vyandarua hivi ipasavyo,”alisisitiza.
Kwa upande wake Kaimu Meneja wa MSD Kanda ya
Tabora Adonizedeck Tefurukwa, alisema,
MSD itahakikisha vyandarua 245, 777 vinasambazwa katika vituo 246 sawa na kaya
59,154 za wilaya ya Kaliua kama ilivyokusudiwa.
“Tutasambaza vyandarua kutoka katika ghala letu
la MSD Kaliua kwa kutumia magari yetu zaidi ya 13 makubwa na madogo, lengo ni
kuhakikisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria yanafikiwa,”alisema.
Aliongeza kuwa, MSD ikiwa ndio msambazaji mkuu wa
bidhaa za afya kwa vituo 7, 000 vya umma na binafsi vilivyoidhinishwa na
serikali itahakikisha inasambaza vyandarua hivyo hadi vituoni bila kujali
kupanda kwa gharama za usafirishaji ikiwemo bei ya mafuta na kupanda kwa dola.
Naye Mwakikishi wa Wizara ya afya Wilfred
Mwaifongo alisema, wananchi wa wilaya hiyo wapokee vyandarua na kutumia kwa
lengo lililokusudiwa ikiwemo kujikinga dhidi ya malaria.
Alisema, hatua hiyo itaimarisha afya zao na
kuchochea ukuaji wa uchumi katika Wilaya ya Kalihua.
Pia Diwani wa kata ya Uyumbu Ramadhani
Mrisho, alieleza kuwa watahakikisha wanatekeleza
maelekezo ya Rais hususani katika maboresho sekta ya afya.
Alisisitiza kuwa, viongozi wa kijiji na halmashauri hiyo hawatakuwa tayari kuona ugawaji wa vyandarua hivyo, unakwama kwa kuwa changamoto ya ugonjwa wa malaria wilayani humo inahitaji ufumbuzi wa pamoja.
Vyandarua vikiendelea kugaiwa.Maafisa wa MSD wakijadiliana wakati wa ugawaji wa vyandarua hivyo.



Comments
Post a Comment