Posts

Showing posts from November, 2023

BOHARI YA DAWA (MSD) YATWAA TUZO YA MLIPA KODI BORA 2023

Image
 Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai (kushoto) akipokea tuzo ya mlipa kodi bora. MSD Yatwaa Tuzo Ya Mlipakodi Bora 2023 ..............................................   Na Mwandishi Wetu BOHARI ya Dawa (MSD), imetwaa tuzo ya Mlipakodi Bora kwa mwaka 2023 ya Mamlaka ya Kodi Tanzania. Tuzo hizo zimetolewa  usiku wa Novemba 24, 2023 katika hafla maalum ya wiki ya Mlipakodi zilizofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijiini Dar es Salaam ambako Bohari hiyo imeibuka mshindi wa kwanza katika kipengele cha WalipakodiWalipakodi wa Kati kwa Mkoa wa Kikodi wa Temeke. Akipokea tuzo hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai amesema ushindi huo una maana kubwa kwa Bohari hiyo na Watanzania. Amesema MSD ambayo ni moja ya Taasisi za kimkakati za Serikali inayohusika na kuzalisha, kununua, kutunza na kusambaza bidhaa za afya kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya vya Serikali nchini inafuata taratibu, sheria na miongozose ikiwa ni pamoja na kulipa kodi stahiki. "Maendeleo yoyo...

SERIKALI YAMWAGA VIFAA TIBA VYA SH. MILIONI 222.472 SINGIDA

Image
     Meneja    wa   Bohari ya Dawa  (MSD)  Kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa (katikati kulia) akipeana mkono na Mbunge wa Jimbo la Singida, Mashariki, Miraji Mtaturu   ikiwa ni ishara ya kumkabidhi jenereta na vifaa tiba vilivyotolewa na Serikali kupitia MSD kwenye hafla iliyofanyika Novemba 20,2023 katika Hospitali ya Wilaya ya Ikungi. ................................................. Na Dotto Mwaibale, Singida SERIKALI  ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Bohari ya Dawa (MSD) imekabidhi vifaa tiba Mkoa wa Singida vyenye jumla ya takribani Sh.Milioni 222.472. Vifaa hivyo ni pamoja na majenereta, sambamba na vifaa vitakavyotumika kuhudumia watoto wanaozaliwa kabla ya muda na huduma nyinginezo ambavyo vimekabidhiwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ikungi, Kituo cha Afya Sepuka na Hospitali ya Wilaya ya Singida, Ilongero. Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi vifaa hivyo ambayo ilishuhudiwa na wabunge, watendaj...

TIA KUJENGA JENGO LA GHOROFA TANO KAMPASI YA SINGIDA, LENGO NI KUSOGEZA HUDUMA PAMOJA

Image
  Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Profesa William Pallangyo, akihutubia katika Mahafali ya 21 ya taasisi hiyo yaliyofanyika Novemba 17, 2023 Kampasi ya Singida. ............................................................. Na Dotto Mwaibale, Singida TAASISI ya Uhasibu Tanzania (TIA) inatarajia kujenga jengo la ghorofa tano katika Kampasi ya Singida  ambalo licha ya kuupendezesha mji wa Singida lakini pia litaweka huduma za taaluma sehemu moja na hivyo kupunguza wingi wa majengo. Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa taasisi hiyo, Profesa William Pallangyo amesema hayo kwenye mahafali ya 12 katika kamapsi ya Singida yaliyofanyika Novemba 17, 2023 mjini hapa. Amesema ujenzi huo unatokana na mradi wa magezi ya kiuchumi wa vyuo vya elimu ya juu ambao ni matokeo ya mkopo wa masharti nafuu unaotekelezwa kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamo jana na Wizara ya Fedha ambapo Singida kupia TIA Kampasi ya Singida ni miongoni mwa mikoa nchini iliyo...

COTUL YATOA OMBI KWA SERIKALI KUSAIDIA MANUNUZI MACHAPISHO YA KIELEKITRONIKI

Image
Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Waziri Mkuu, Sakina Mwinyimkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi akifungua  kongamano la kisayansi ambalo limeandaliwa na Shirikisho la Maktaba za Vyuo Vikuu na Taasisi zinazofanya Utafiti Tanzania (COTUL) kwa niaba ya Katibu  Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi   ....................................................  Na Dotto Mwaibale, Singida SHIRIKISHO la Maktaba za Vyuo Vikuu na Taasisi zinazofanya Utafiti Tanzania (COTUL) limeiomba Serikali kupitia ofisi ya Waziri Mkuu kusaidia kununua machapisho ya kielekitroniki  yanayotumika kufundishia vyuoni kwa kuwa yanauzwa bei ghali ambayo shirikisho hilo haliwezi kumudu kuyanunua. Mwenyekiti wa Shirikisho hilo , Dkt. Sydney Msonde alitoa ombi hilo Novemba 9, 2023 wakati wa ufunguzi wa kongamano la kisayansi ambalo limewakutanisha wanataaluma mbalimbali katika ngazi ya wakutubi, walimu wafundishaji ku...