TIA KUJENGA JENGO LA GHOROFA TANO KAMPASI YA SINGIDA, LENGO NI KUSOGEZA HUDUMA PAMOJA

 

Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Profesa William Pallangyo, akihutubia katika Mahafali ya 21 ya taasisi hiyo yaliyofanyika Novemba 17, 2023 Kampasi ya Singida.

.............................................................


Na Dotto Mwaibale, Singida

TAASISI ya Uhasibu Tanzania (TIA) inatarajia kujenga jengo la ghorofa tano katika Kampasi ya Singida  ambalo licha ya kuupendezesha mji wa Singida lakini pia litaweka huduma za taaluma sehemu moja na hivyo kupunguza wingi wa majengo.

Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa taasisi hiyo, Profesa William Pallangyo amesema hayo kwenye mahafali ya 12 katika kamapsi ya Singida yaliyofanyika Novemba 17, 2023 mjini hapa.

Amesema ujenzi huo unatokana na mradi wa magezi ya kiuchumi wa vyuo vya elimu ya juu ambao ni matokeo ya mkopo wa masharti nafuu unaotekelezwa kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamo jana na Wizara ya Fedha ambapo Singida kupia TIA Kampasi ya Singida ni miongoni mwa mikoa nchini iliyonufaika na mpango huo kwa kupata Sh.Bilioni 18.

Profesa  Pallangyo amesema, jengo hilo litakuwa na ghorofa tano likiwa na kumbi za mihadhara,madarasa kumbi za mikutano pamoja na ofisi linatarajia kuanza kujengwa Februari mwaka 2024.

" Hadi kukamilika kwa ujenzi huo zitatumika Sh. Bilioni  16  na kwa sasa kinachofanyika ni uandaaji wa tathimini ya mazingira," aliseama Prof. Pallangyo.

Ujenzi huo umekuja hasa kwa kipindi hiki ambapo Kampasi ya Singida imepiga hatua katika uendeshaji wa mafunzo, huduma za ushauri wa kitaalam, rasimali watu pamoja na miundo mbinu ya kufundishia na kujifunzia.

Profesa Pallangyo amesema idadi ya wanaojiunga kwa mwaka imekuwa ikiongezeka huku akigusia kuwa kwa mwaka wa masomo 2023/2024 TIA Singida imepokea wanafunzi 1443 lengo likiwa ni kufikia 2600 ikilinganishwa na wanafunzi 1556 kwa mwaka wa masomo ya 2022/23.

Amesema ongezeko la wanafunzi kwa kiasi kikubwa limetokana na ubora wa elimu unaotolewa na taasisi hiyo na kuwajengea umahiri unaowawezesha kupata ajira sambamba na kujiajiri.

Amesema Sababu ya pili ni utaratibu wa serikali kuwapangia vyuo wahitimu wa kidato cha nne waliofaulu na kukidhi vigezo huku akifafanua kuwa kwa mwaka wa masomo 2023/24 jumla ya wanafunzi 1170 kutokana maeneo mbalimbali ya nchi wamejiunga na fani mbalimbali katika chuo hicho.

Ametaja sababu ya tatu kuwa pamoja na ongezeko la mikopo kwa wanafunzi wa ngazi ya Shahada na kwa mwaka huu pekee jumla ya wanafunzi 810 watanufaika na mikokopo katika kampasi ya Singida hilo likiwa ni ongezeko la asilimia 15.9 ikilinganishwa na wachuo 699 waliopata mikopo kwa mwaka 2022/23.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Iramba, Mh. Suleimani Mwenda ambaye amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mh. Peter Serukamba katika mahafali hayo amesema mafunzo wanayoyatoa kuhusu uhasibu ununuzi na ugavi, usimamizi wa biashara na uongozi wa rasimali watu unaendana na mtazamo wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hasani wa kutengeneza Diplomasia ya Uchumi.

Amesema mafunzo wanayoendelea kuyatoa yameendelea kuboresha ubora wa elimu na kuhamasisha matumizi ya teknolojia hususani Tehama.

Hata hivyo amesema licha ya kufundishwa kuhusu Tehama lakini matumizi yake bado ni ya kiwango cha chini hasa katika masula ya kuongeza maarifa kwa mtu mmoja mmoja hasa kwa kundi la vijana.

Ameshauri kuongeza juhudi katika kuwaelekeza vijana kuhusu matumizi sahihi ya Tehama na kuwa kwa Afrika Mashariki Tanzania inaongoza katika matumizi ya Tehama lakini watumiaji  wakubwa ambao ni vijana chini ya miaka 35 wanaitumia kwa mambo yasiyokuwa na tija.

Akizungumzia kuhusu ajira amewataka wahitimu kujiongezea thamani kwa kuwa wabunifu kwenye kazi ili wawe na mawanda mapana ya kupata ajira zisizo kuwa na shaka..

Viongozi wakiwa meza kuu wakishiriki kuimba wimbo wa Taifa. Kutoka kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wizara ya Fedha, Thabiti Dokodoko, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara, Wakili Said Chiguma, Mgeni rasmi wa Mahafali hayo, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, Afisa Mtendaji wa TIA, Profesa, William Pallangyo na Mkurugenzi wa TIA, Kampasi ya Singida, Dkt. James Mrema.
Waadhiri wakiwa kwenye mahafali hayo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Utafiti na Machapisho TIA, Dkt.Abdallah Gora, Mhadhiri Shibalyandumi Ulomi na Mhadhiri Dkt. CrispinRyakitimbo.
Wazazi na Walezi wa Wahitimu hao wakiwa kwenye mahafali hayo.

Viongozi wa TIA wakishiriki mahafali hayo. Kutoka kulia ni Mjumbe wa Bodi ya Ushauri, Mystica Ngongi, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo (NDC) ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Ushauri Nicolaus Shombe Mjumbe wa Bodi ya Ushauri na Mhadhiri Mwandamizi-Chuo Kikuu cha Mzumbe, Leonada Mwagike na Mkurugenzi wa Utawala, Menejiment na Usimamizi wa Rasilimaliwatu-Ofisi ya Rais TAMISEMI, Emma Lyimo.

Mshereheshaji wa mahafali hayo ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya mpango wa ukuzaji na uendelezaji wa wanafunzi kitaaluma na kitaalamu yaani(Career Development Program), TIA,  Imani Matonya akiwajibika. 

Muonekano wa viongozi mbalimbali na Waadhiri Jukwaa kuu.
Wasanii wa kikundi cha utamaduni cha Kabila la Wanyaturu wakitoa burudani kwenye mahafali hayo.


Mshereheshaji wa mahafali hayo Daud Mashauri akiwajibika.

Wahitimu wa Shahada ya Uhasibu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida wakirusha kofia juu kuonesha furaha zao katika mahafali ya 21 ya taasisi hiyo.


Picha za matukio mbalimbali ya mahafali hayo zikichukuliwa.

Mgeni rasmi wa mahafali hayo, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleimani Mwenda (katikati) akiahirisha mahafali hayo ya 21 kwa mwaka 2023. Kushoto ni Wakili Said Chuguma ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa wizara na kulia ni  Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Profesa. William Pallangyo. 


Comments

Popular posts from this blog

SUA, TAASISI ZOTE ZA WIZARA YA KILIMO WASAINI MKATABA WA KUINUA KILIMO NCHINI

HALMASHAURI WILAYA YA IKUNGI YABAINI MBINU MPYA UKUSANYAJI WA MAPATO

TAASISI TA UHASIBU SINGIDA YAZINDUA UMOJA WA WANAFUNZI WA FANI YA UNUNUZI NA UGAVI