Posts

Showing posts from March, 2024

WADAU WA MSD WAHIMIZWA KUSIMAMIA MATUMIZI SAHIHI YA TAKWIMU BIDHAA ZA AFYA

Image
Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni,  akifungua kikao cha wadau na wateja wa Bohari ya Dawa (MSD),  Kanda ya Mtwara Machi 22, 2024. ........................... Na Mwandishi Wetu , Mtwara WADAU wa Afya wa Bohari ya Dawa  (MSD) Kanda ya  Mtwara wamehimizwa kusimamia matumizi sahihi ya takwimu za mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, ili ziwawezeshe kufanya maamuzi sahihi juu ya bidhaa hizo katika maeneo yao. Akifungua kikao cha wadau na wateja wa MSD kanda ya Mtwara, Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni amesema uwepo wa takwimu sahihi unaiwezesha MSD kuagiza kwa usahihi bidhaa za afya na kuboresha upatikanaji wa bidhaa hizo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya. Aidha, amewashauri MSD kuhakikisha utaratibu wa vikao  vya mwaka vya wadau ni muhimu kwa pande zote mbili, yaani Bohari ya Dawa (MSD) yenyewe na wadau ili kwa pamoja kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya, kwa kujadili changamoto na kuzitafutia utatuzi. Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mtwar...

MSD YATOA UFAFANUZI KUDAIWA VIFAA TIBA VYA MILIONI 400

Image
 

MAAFISA WATENDAJI WATAKIWA AJENDA YAO KUWA ANWANI ZA MAKAZI, KUHAKIKI TAARIFA ZA WANANCHI

Image
Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Innocent Jacob akizungumza wakati wa siku ya pili ya mafunzo ya siku 14 kwa watendaji wa kata, mitaa, wenyeviti wa Serikali za mitaa na vijiji yanayohusu namna ya kukusanya taarifa za Anwani za Makazi  Manispaa ya Singida. ......................... Na Dotto Mwaibale, (Singidani Blog) MAAFISA Watendaji wa Mitaa kote nchini wametakiwa katika vikao vyao vyote vya msingi ajenda yao kubwa iwe ni anwani za makazi pamoja na uhakiki wa taarifa za wananchi. Ombi hilo limetolewa Machi 15, 2024 na Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Innocent Jacob wakati wa siku ya pili ya mafunzo ya siku 14 kwa watendaji wa kata, mitaa, wenyeviti wa Serikali za mitaa na vijiji  yanayohusu namna ya kukusanya taarifa za Anwani za Makazi  Manispaa ya Singida yaliyoanza Machi 14, 2024 ambayo yameandaliwa na wizara hiyo kwa kus...

SINGIDA HAWATAKI DAWA NA VIFAA TIBA VILIVYO CHINI YA KIWANGO

Image
Katibu Tawala Msaidizi wa Huduma za Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida, Stanslaus Choaji ambaye alikuwa mgeni rasmi akifungua mafunzo hayo. ........................... Na Dotto Mwaibale, (Singidani Blog) MKOA wa Singida hautakuwa tayari kuwa dampo la matumizi ya dawa, vitendanishi na vifaa tiba ambavyo havina havina ubora. Katibu Tawala Msaidizi wa Huduma za Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida, Stanslaus Choaji aliyasema hayo Machi 12, 2024 wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya wataalamu, wakaguzi na wafamasia wa Halmashauri za wilaya ambao wanakagua dawa, vifaa tiba na vitendanishi yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA)  Choaji alisema jukumu la Serikali ni kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya na kuweza kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali na kukuza uchumi wa Taifa. "Hilo ni jukumu kubwa la Serikali na mtaona jinsi inavyofanya kila jitihada kadili itakavyowezekana kwa kutumia rasilimali mbalimbali ili kuwawezes...

DSE, WADAU WANG’ARISHA HAFLA YA ‘PIGA KENGELE’ KWA USAWA WA KIJINSIA 2024

Image
Mkurugenzi wa Uwekezaji ndani ya Wizara ya Mipango na Uwekezaji Aristides Mbwasi (wa tatu kushoto) ambaye alimuwakilisha Waziri wa wizara hiyo, Profesa Kitila Mkumbo aliyekuwa mgeni rasmi, akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa yaliyofanyika Machi 8, 2028 jijini Dar es Salaam. .  Godwin Myovela, Dar es Salaam MAELFU ya wanawake nchini jana wamejitokeza kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake (8 Machi 2024) huku Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikitumia siku hii vilivyo kufanya tathmini ya hali ya usawa wa kijinsia, sambamba na kuongeza hamasa juu ya uelewa wa pamoja wa dhana hiyo kupitia mpango wa ‘Ring the Bell for Gender Equality’ (piga kengele kwa usawa wa kijinsia). Mlio huo wa kengele wa kimataifa, ikiwemo Tanzania, unalenga kuleta umakini kwa jukumu muhimu ambalo taasisi na makampuni mbalimbali zinaweza kutekeleza katika kukuza dhana ya usawa wa kijinsia, ili kutimiza matakwa ya Malengo ya Maendeleo Endelevu, sambamba na ku...