Posts

Showing posts from October, 2023

WANAFUNZI WAPYA TAASISI YA UHASIBU MKOA SINGIDA WATAHADHARISHWA KUTOJIHUSISHA MAPENZI NA WALIMU

Image
   Kaimu  Mkurugenzi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida, ambaye pia ni Mratibu wa taaluma,   Flora Lemnge, akizungumza na wanafunzi wapya wa kampasi hiyo katika   semina elekezi kwa wanafunzi hao iliyofanyika Oktoba 30, 2023. Kutoka kushoto ni Mlezi wa Wanafunzi, Asia Hansy, Mshauri wa wanafunzi, Ambwene Kajula, Mratibu wa Mipango na Dawati la Malalamiko wa taasisi hiyo, Magreth Emmanuel.    .................................................................... NA DOTTO MWAIBALE, SINGIDA WANAFUNZI wapya waliochaguliwa kujiunga na Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida kwa msimu wa masomo wa 2023/2024 wametakiwa kutojihusisha na uhusiano wa kimapenzi na walimu. Kaimu Mkurugenzi wa kampasi hiyo ambaye pia ni Mratibu wa taaluma,  Flora Lemnge, ameyasema hayo jana Oktoba 30, 2023 katika semina elekezi kwa wanafunzi hao na kueleza kuwa mwanafunzi atakayejihusisha na uhusiano  wa kimapenzi  ...

TAKUKURU MKOA WA SINGIDA YAOKOA SH.MILIONI 54

Image
 Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU ) Mkoa wa Singida, Sipha Mwanjala akitoa taarifa  kwa waandishi wa habari kwa kipindi cha Julai-Septemba 2023 katika kikao kilichofanyika Oktoba 27, 2023. Kikao na waandishi wa habari na maofisa wa TAKUKURU Mkoa wa Singida, kikifanyika. Kikao kikiendelea. ......................................................... Na Dotto Mwaibale, Singida TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU),Mkoa wa Singida imeokoa Sh. 54,087,750.58 zilizotokana na wazabuni kutowasilisha kodi ya zuio Mamlaka ya Mapato,Tanzania (TRA) na kupeleka vifaa pungufu katika miradi mbalimbali. Hayo yamebainishwa Oktoba 27, 2023 na Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida Sipha Mwanjala wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kwa kipindi cha Julai-Septemba 2023. Alisema TAKUKURU Mkoa wa Singida kwa kipindi cha Julai –Septemba 2023 kwa upande wa uzuiaji rushwa walifuatilia utekelezaji wa miradi kumi na tatu yenye thamani ya zaidi Sh.Bilio...

DC WILAYA YA KALIUA AWATAKA VIJANA KUTUMIA VYAKULA VYENYE LISHE KUKABILIANA CHANGAMOTO YA NGUVU ZA KIUME

Image
Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Dk. Rashid ChuaChua akigawa vyandarua vyenye dawa vilivyotolewa na Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) kwa ajili kukabiliana na ugonjwa wa malaria wilayani humo. Na Mwandishi Wetu, Kaliua   MKUU wa Wilaya ya Kaliua Dk. Rashid ChuaChua amewataka wananchi wa Wilaya hiyo hususani vijana kutafuta mbadala wa tatizo la nguvu za kiume ikiwemo kuzingatia vyakula vya lishe na kuacha kisingizio kuwa matumizi ya vyandarua vyenye dawa ndio chanzo. Amesema upendo hekima na huruma ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kunusuru wananchi wake kwa kusambaza vyandarua katika wilaya hiyo ni juhudi ambazo haziwezi kufifishwa na imani potofu. Akizungumza jana mkoani Tabora wilayani Kaliua Dk. Rashidi amewataka wananchi hao hususani vijana kutafuta mbadala wa tatizo la nguvu za kiume, ikiwemo kuzingatia vyakula vya lishe na kuacha kisingizio kuwa matumizi ya vyandarua vyenye dawa ndio chanzo. “Kama mashine haifanyi kazi haifanyi tu sio kwa sababu ya kutumia vyandarua vyenye dawa, tu...

TRA YAFAFANUA MADAI YA MFANYABIASHARA EMMANUEL GADI

Image
Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Stephen Kauzeni akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam wakati akitoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu malalamiko ya Bw. Emmanuel Gadi ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Wintech Tanzania Ltd anayedai kuwa, TRA imetengeneza mfumo wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo halali wa Serikali kinyume na Sheria ya Forodha (Picha na Mpiga picha wetu). ........................................  Na: Mwandishi Wetu   MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) haina mfumo wowote mwingine inaouendesha wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo wa Forodha wa TANCIS ambao unatumika kwa mujibu wa Sheria ya Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Bw. Stephen Kauzeni kwa waandishi wa habari wakati akitoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu malalamiko ya Bw. Emmanuel Gad...

MSD YAFANYA MABORESHO MAKUBWA SEKTA AFYA SINGIDA, YATOA VIFAA TIBA, DAWA ZA MILIONI 532.4

Image
Mhandisi wa vifaa tiba wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Kati Dodoma , Jumanne Mapesa  (kulia) akimkabidhi boksi la dawa Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida, Paul Ndeki mjini Singida Oktoba 11, 2023. Wengine ni wafanyakazi wa hospitali hiyo. ......................................................... Na Dotto Mwaibale , Singida BOHARI ya Dawa (MSD) imetoa vifaa tiba na dawa zenye thamani ya zaidi ya Sh. Milioni 532.4 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida, Hospitali ya Wilaya ya Singida, Hospitali ya Wilaya ya Iramba Kiomboi, Hosptali ya Wilaya ya Ikungi na Kituo cha Afya cha Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kwa ajili ya kuboresha huduma za matibabu mkoani hapa. Akizungumza Oktoba 11, 2023 wakati wa kukabidhi vifaa hivyo kwenye hospitali hizo,  Meneja wa MSD Kanda ya kati Dodoma, Bi. Mwanashehe Jumaa  alivitaja vifaa tiba na dawa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida kuwa ni vitanda 9 (ICU  Beds) vya kisasa pamoja na  dawa.. A...

MAADHIMISHO YA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA NSSF SINGIDA YATAMBUA VINARA WA MICHANGO YA WANACHAMA

Image
Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida, Oscar Kalimilwa (katikati)Sr Franca Ogbunuju kutoka Shirika la Srs Medical Missionaries of Mary (MMM), (kulia) na Mwakilishi wa Kanisa la  Evangelist Assemblies of God  Tanzania (EAGT)  Kiomboi Iramba John Leonard wakikata keki maalumu kwa ajili ya maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja yaliyoandaliwa na NSSF Oktoba 6, 2023,  ........................................................... Na Dotto Mwaibale, Singida WAKATI maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja yakiadhimishwa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Singida limezitambua taasisi na kuwashukuru waajiri wanaojitolea kwa hali na mali kuhakikisha michango ya wanachama wake inawasilishwa kwa wakati. Hata hivyo shirika hilo pamoja na mambo mengine limezitaja taasisi takribani tano zilizoongoza kwa uwasilishaji wa michango hiyo kwa mwaka huu mkoani hapa zikiwemo Mount Meru Miller na Tree for the Future. Nyingine ni Makiungu Hospital,  Srs Medical Miss...