TANZANIA YETU BLOG
Thursday, April 18, 2024
Tuesday, April 9, 2024
MSD YAKUTANA NA WADAU WAKE KANDA YA IRINGA, RC RUVUMA ATAKA WELEDI SEKTA YA AFYA
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali. Ahmed Abbas Ahmed (kushoto) akipokea tuzo maalumu kutoka kwa Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa Bohari ya Dawa (MSD), Victor Sungusia wakati wa mkutano mkuu wa MSD na wadau wake wa Mkoa wa Ruvuma uliofanyika Aprili 8, 2024,
Na Mwandishi Wetu, Ruvuma
MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali. Ahmed Abbas Ahmed, amewataka watumishi wa sekta ya afya Mkoani Ruvuma, kuzingatia weledi na kutoa huduma bora kwa wananchi, ili kuakisi maboresho na uwekezaji mkubwa uliofanywa kwenye sekta ya afya, chini ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita.
Kanali Ahmed amesisitiza kuwa, serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imetoa fedha nyingi kwa ajili ya maboresho na ujenzi wa miundombinu ya afya mathalani majengo, ununuzi wa bidhaa za afya
na kuwezesha ajira za kutosha, lengo likiwa kuinua hadhi ya huduma zinazotolewa nchini, hasa zinazomgusa mtanzania wa kawaida.
Kanali Ahmed ametoa rai hiyo hii leo, wakati wa akifungua kikao kazi baina ya MSD Kanda ya Iringa na wadau wake kutoka halmashauri saba za mkoa wa Ruvuma (Madaba Tc, Madaba Dc, Songea MC, Songea DC, Nyasa DC, Mbinga TC na Mbinga DC), kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ruwiko, ulioko Manispaa ya mji wa Songea.
Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha viongozi hao wa sekta ya afya Mkoani humo, kufanya maoteo yao ya bidhaa za afya kwa usahihi, umakini na kwa wakati ili kuiwezesha Bohari ya Dawa (MSD) kutekeleza majukumu yake ya ugavi wa bidhaa za afya kwa weledi.
Mhe. Ahmed amewataka pia watendaji hao kusimamia ukusanyaji wa mapato, na kutumia vyema vyanzo vyao vingine vya mapato katika kulipa madeni ya MSD, huku akiwakumbusha pia kuhakiki taarifa sahihihi za utunzaji na utoaji wa bidhaa za afya, ili kuepuka upotevu wa bidhaa hizo.
Katika hatua nyigine, Mkuu huyo wa mkoa ameipongeza MSD kwa utendaji wake katika kuboresha hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya, huku akiwapongeza kwa kuitisha mkutano huo wa wadau kwani utasaidia kuboresha mahusiano na mawasiliano.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Ugavi na uendeshaji wa MSD Victor Sungusia, amebainisha maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanywa na MSD katika nyanja mbalimbali kupitia majukumu yake makuu ya uzalishaji, ununuzi, utunzaji na usambazaji.
Bw. Sungusia amebainisha jinsi MSD ilivyojizatiti katika utekelezaji wa majukumu yake kupitia mifumo ya kisasa ya kidigitali, ugatuzi wa majukumu ya Kanda, ujenzi wa viwanda mbalimbali vya dawa na vifaa tiba, maboresho ya mfumo wa usambazaji wa bidhaa, upanuzi wa maeneo ya uhifadhi na kuwajengea uwezo watumishi wake.
Naye Meneja wa MSD Kanda ya Iringa Bw. Robert Lugembe akiwakiribisha wajumbe wa kikao hicho, alibainnisha kuongezeka kwa uwezo wa MSD kuwahudumia wateja wake na kukidhi mahitaji, sambamba na maboresho ya upatikanaji wa bidhaa za afya mathalani vifaa tiba, mkoani humo.Meneja wa MSD Kanda ya Iringa Bw. Robert Lugembe akizungumza kwenye mkutano huo.
Thursday, April 4, 2024
WANANCHI ITIGI WAMSHUKURU RAIS , KITUO CHA AFYA KUANZA UPASUAJI
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida, Hussein Simba, akizungumza wakati akiongoza kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Aprili 3, 2024. Kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ayubu Kambi na na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Jonathan Hemed.
..................................
Na Mwandishi Wetu, Itigi
WANANCHI wa Kata ya Rungwa iliyopo wilayani Itigi mkoani Singida wamemshuru
Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea Kituo cha Afya ambapo sasa wajawazito
wameanza kupata huduma ya upasuaji na kuondokana na changamoto waliokuwa nayo
ya kufuata huduma hiyo Hospitali ya St. Gasper iliyopo Itigi.
Diwani wa Kata hiyo Said Sudi akitoa shukurani hizo kwa niaba ya wananchi
wake wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichoketi Aprili 3, 2024 alisema
hawana cha kumlipa Rais Samia zaidi ya kumpa kura zote katika uchanguzi mkuuu
utakaofanyika mwakani.
"Kata yetu tutampa kura asilimia 100 mama yetu kwa kazi kubwa
aliyotufanyia si kwa kituo cha afya pekee bali na miradi mingine mingi iliyotekelezwa.
wajawazito walikuwa wakilazimika kusafiri umbali wa kilometa 194 pale walipohitaji
kupata huduma ya upasuaji lakini sasa wanaipata hapahapa nyumbani ni jambo la
kumshuruku sana Mungu kupitia Rais wetu," alisema Sudi.
Sudi alisema Rais Samia aliwapa Sh. Milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa
kituo hicho cha afya ambacho kimeanza kutoa huduma hiyo Februari 27, 2024
ambapo wajawazito watano wamenufaika na huduma.
Alisema wajawazito walionufaika na huduma hiyo ni kutoka vitongoji vya
Mkora A na B na kata za jirani za Kiloli
na Kambikatoto.
Sudi alitumia nafasi hiyo kuomba wasaidiwe kupata gari la kubebea wagonjwa,
mashine ya kufulia na kunyoshea nguo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Hussein Simba alisema ukusanyaji
wa mapato katika halmashauri hiyo upo vizuri hadi kufikia mwezi februari
walikuwa wamefikia asilimia 95 ya mapato ya Serikali mapato huru na mapato
lindwa ilikuwa ni asilimia 35 na kuwa
wanaamini kwa kasi hiyo hadi mwezi machi ambao bado hawajaujadili watafikia
asilimia 100.
Simba alisema kupitia fedha za Serikali kuu na wahisani wamefikia asilimia
77 ya lengo ambapo zaidi ya Sh.Bilioni 4.9 halmashauri hiyo imekwishapewa ili
kukamilisha miradi mbalimbali na kuwa asilimia iliyobaki ni ndogo ambapo amewahimiza
madiwani kuisimamia miradi hiyo kwa kufanya kazi kwa vitendo zaidi badala ya
maneno ili kufikia malengo ya wananchi.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Kemirembe Lwota, aliomba miradi
yote inayotekelezwa ikikamilike ifikapo
Aprili 30, 2024 ambapo pia aliwaomba madiwani kuhimiza kampeni ya kupata
madawati kufuatia kuwepo kwa changamoto ya kukosekana kwa madawati katika shule zote wilayani humo.
Aidha, Lwota alihimiza mazao yote kuuzwa kwa njia ya stakabadhi gharani
badala ya kuuzwa kiholela jambo linalosababisha Serikali kukosa mapato ambapo
utaratibu wa kuyauza mazo hayo unafanyika.
Katika hatua nyingine Lwota amewataka madiwani hao na watumishi wengine
katika wilaya hiyo kuanza maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru ambao
unatarajiwa kuanza kukimbizwa wilayani humo mwanzoni mwa mwezi wa Julai, 2024.
Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Manyoni, Jumanne
Ismail alishukuru mshikamano uliopo baina ya chama na Serikali ambao unaendelea
kuifanya halmashauri hiyo kusonga mbele.
Ismail alisema Aprili 15, 2024 wanatarajia kuanza kufanya mikutano ya
hadhara katika kata zote wakianzia wilayani Manyoni na kisha Itigi na lengo la
mikutano hiyo ni kuzungumza na wananchi kuhusu miradi yote iliyotekelezwa
katika maeneo yao na Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa
CCM.
Katika kikao hicho cha baraza la madiwani ambacho kilikuwa na ajenda nane Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Hussein Simba aliweza kumkaribisha Mkurugenzi mpya wa halmashauri hiyo, Ayubu Kambi na kutoa taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa lengo la kumpa picha halisi ya miradi hiyo ili aielewe na atakapoanza kazi ajue pa kuanzia.
Katibu wa CCM Wilaya ya Manyoni Maimuna Likunguni, akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Friday, March 22, 2024
WADAU WA MSD WAHIMIZWA KUSIMAMIA MATUMIZI SAHIHI YA TAKWIMU BIDHAA ZA AFYA
Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni, akifungua kikao cha wadau na wateja wa Bohari ya Dawa (MSD), Kanda ya Mtwara Machi 22, 2024.
...........................
Na Mwandishi Wetu, Mtwara
WADAU wa Afya wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Mtwara
wamehimizwa kusimamia matumizi sahihi ya takwimu za mnyororo wa ugavi wa bidhaa
za afya, ili ziwawezeshe kufanya maamuzi sahihi juu ya bidhaa hizo katika
maeneo yao.
Akifungua kikao cha wadau na wateja wa MSD kanda
ya Mtwara, Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni amesema uwepo wa takwimu
sahihi unaiwezesha MSD kuagiza kwa usahihi bidhaa za afya na kuboresha
upatikanaji wa bidhaa hizo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.
Aidha, amewashauri MSD kuhakikisha utaratibu wa
vikao vya mwaka vya wadau ni muhimu kwa
pande zote mbili, yaani Bohari ya Dawa (MSD) yenyewe na wadau ili kwa pamoja
kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya, kwa kujadili changamoto na kuzitafutia
utatuzi.
Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay
ameeleza kuwa kwa sasa kanda ya MSD Mtwara inahudumia vituo vya kutolea huduma
za afya 631, na inasambaza bidhaa za afya kila baada miezi miwili.
Naye Meneja Huduma kwa Wateja na Miradi Dkt.
Pamella Sawa ameeleza kuwa vikao vya MSD na wadau wake kuanzia sasa vitakuwa
endelevu kila mwaka.
MSD Kanda ya Mtwara inahudumia mikoa ya Lindi,Mtwara na Wilaya ya Tunduru.Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay, akizungumza kwenye kikao hicho
Tuesday, March 19, 2024
Saturday, March 16, 2024
MAAFISA WATENDAJI WATAKIWA AJENDA YAO KUWA ANWANI ZA MAKAZI, KUHAKIKI TAARIFA ZA WANANCHI
Na Dotto Mwaibale, (Singidani Blog)
MAAFISA Watendaji wa Mitaa kote nchini wametakiwa katika vikao vyao vyote
vya msingi ajenda yao kubwa iwe ni anwani za makazi pamoja na uhakiki wa taarifa
za wananchi.
Ombi hilo limetolewa Machi 15, 2024 na Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Innocent Jacob wakati wa siku ya pili ya mafunzo ya siku 14 kwa watendaji wa kata, mitaa, wenyeviti wa Serikali za mitaa na vijiji yanayohusu namna ya kukusanya taarifa za Anwani za Makazi Manispaa ya Singida yaliyoanza Machi 14, 2024 ambayo yameandaliwa na wizara hiyo kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na kuwa siku mbili kati ya hizo 14 zitatumika kwa ajili ya kuhakiki taarifa. .
Jacob alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwawzesha wenyeviti hao ili waweze
kutoa taarifa kwa wanananchi za zoezi hilo ndani ya siku hizo na wananchi nao
waweze kutoa za kwao kama NIDA, namba ya simu, Tin namba ya biashara na taarifa
nyingine za majengo, makazi kama walivyoelekezwa watendaji wa mitaa jinsi ya
kulifanya zoezi hilo.
"Watendaji wa mitaa ndio watakao kwenda kukusanya taarifa hizi kwa
wakazi wao kwa sababu katika maeneo yote ya utawala wao ndio wahusika wakubwa
na watashirikiana na wenyeviti wa mitaa kufanya kazi hiyo," alisema Jacob.
Alisema Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), kwa
kushirikiana na TAMISEMI, wameandaa zoezi hilo kwa lengo la kuhakiki taarifa za
makazi kwa awamu ya pili baada ya awali kufanyika kwa njia ya operesheni ambapo
huenda kuna baadhi ya wakazi hawakuweza kupata fursa ya kuingia katika
kanzidata ya Anwani za Makazi.
Alitaja baadhi ya vitu ambavyo viliweza kusahulika kuwekwa kwenye kanzidata
kuwa ni taarifa ya majengo, viwanja, majina katika vibao vya mitaa hivyo
kurudiwa tena katika zoezi hilo la awamu ya pili la uhakiki.
Jacob alisema umuhimu wa Anwani za Makazi zitarahisisha utambuzi kwa wakazi
wa eneo husika na kuweza kupata huduma mbalimbali kwa kufikiwa kiurahisi mahala
walipo kwa kutumia programu tumizi kwa ajili ya umma inayoitwa NAPA ambayo
inapakuliwa kupitia simu janja ambapo wananchi wote hapa nchini wakiwemo wa
Manispaa ya Singida wataweza kuingia katika mfumo huo kwa kuandika NAPA
Tanzania.
Alisema mafunzo hayo yanafanyika Manispaa ya Kigoma, Iringa na Singida na
yatakuwa endelevu kwa kufanyika katika mikoa mingine.
Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Dkt. Adrianus
Kalekezi alisema katika mafunzo hayo wataalamu wanaelekeza namna ya kuingiza
taarifa katika mfumo wa Anwani za Makazi na kuwa hivi sasa wanauhisha taarifa
za awali baada ya kazi hiyo kufanyika awamu ya kwanza.
Dkt. Kalekezi alisema suala hilo la Anwani za Makazi ni la muhimu katika
manispaa hiyo kwani wananchi watapata huduma kwa urahisi na alitumia nafasi
hiyo kuwaomba wananchi kuilinda miundombinu ya Anwani za Makazi iliyowekwa kama
vibao vinavyoonesha majina ya mitaa na barabara na kueleza kuwa ni lazima
ilindwe ili waweze kunufaika na zoezi hilo kwani bila miundombinu hiyo inakuwa
vigumu kwao kuelekezwa na kuitambua mitaa na barabara.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Mwankoko, Habiba Juma akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo alisema zoezi hilo litawarahisishia kutoa huduma kwa wananchi na kupunguza gharama ya fedha na muda kutoka sehemu moja kwenda nyingine na wananchi wataweza kupata huduma kupitia anuani za makazi.Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka WHMTH, George Leonard, akitoa mafunzo kwa watendaji hao.Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka WHMTH, Janeth Peter , akiwajibika wakati wa mafunzo hayo.Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Dkt. Adrianus Kalekezi, akizungumzia zoezi hilo.