Tuesday, April 9, 2024

MSD YAKUTANA NA WADAU WAKE KANDA YA IRINGA, RC RUVUMA ATAKA WELEDI SEKTA YA AFYA

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali. Ahmed Abbas Ahmed (kushoto) akipokea tuzo maalumu kutoka kwa Mkurugenzi wa Ugavi na Uendeshaji wa Bohari ya Dawa (MSD), Victor Sungusia wakati wa mkutano mkuu wa MSD na  wadau wake wa Mkoa wa Ruvuma uliofanyika Aprili 8, 2024, 

Na Mwandishi Wetu, Ruvuma

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Kanali. Ahmed Abbas Ahmed, amewataka watumishi wa sekta ya afya Mkoani Ruvuma, kuzingatia weledi na kutoa huduma bora kwa wananchi, ili kuakisi maboresho na uwekezaji mkubwa uliofanywa kwenye sekta ya afya, chini ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita.

Kanali Ahmed amesisitiza kuwa, serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imetoa fedha nyingi kwa ajili ya maboresho na ujenzi wa miundombinu ya afya mathalani majengo, ununuzi wa bidhaa za afya

 na kuwezesha ajira za kutosha,  lengo likiwa kuinua hadhi ya huduma zinazotolewa nchini, hasa zinazomgusa mtanzania wa kawaida.

Kanali Ahmed ametoa rai hiyo hii leo, wakati wa akifungua kikao kazi baina ya MSD Kanda ya Iringa na wadau wake kutoka halmashauri saba za mkoa wa Ruvuma (Madaba Tc, Madaba Dc, Songea MC, Songea DC, Nyasa DC, Mbinga TC na Mbinga DC), kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ruwiko, ulioko Manispaa ya mji wa Songea.

Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha viongozi hao wa sekta ya afya Mkoani humo, kufanya maoteo yao ya bidhaa za afya kwa usahihi, umakini na kwa wakati ili kuiwezesha Bohari ya Dawa (MSD) kutekeleza majukumu yake ya ugavi wa bidhaa za afya kwa weledi.

Mhe. Ahmed amewataka pia watendaji hao kusimamia ukusanyaji wa mapato, na kutumia vyema vyanzo vyao vingine vya mapato katika kulipa madeni ya MSD, huku akiwakumbusha pia kuhakiki taarifa sahihihi za utunzaji na utoaji wa bidhaa za afya, ili kuepuka upotevu wa bidhaa hizo.

Katika hatua nyigine, Mkuu huyo wa mkoa ameipongeza MSD kwa utendaji wake katika kuboresha hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya, huku akiwapongeza kwa kuitisha mkutano huo wa wadau kwani utasaidia kuboresha mahusiano na mawasiliano.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Ugavi na uendeshaji wa MSD Victor Sungusia, amebainisha maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanywa na MSD katika nyanja mbalimbali kupitia majukumu yake makuu ya uzalishaji, ununuzi, utunzaji na usambazaji.

Bw. Sungusia amebainisha jinsi MSD ilivyojizatiti katika utekelezaji wa majukumu yake kupitia mifumo ya kisasa ya kidigitali, ugatuzi wa majukumu ya Kanda, ujenzi wa viwanda mbalimbali vya dawa na vifaa tiba, maboresho ya mfumo wa usambazaji wa bidhaa, upanuzi wa maeneo ya uhifadhi na kuwajengea uwezo watumishi wake.

Naye Meneja wa MSD Kanda ya Iringa Bw. Robert Lugembe akiwakiribisha wajumbe wa kikao hicho, alibainnisha kuongezeka kwa uwezo wa MSD kuwahudumia wateja wake na kukidhi mahitaji, sambamba na maboresho ya upatikanaji wa bidhaa za afya mathalani vifaa tiba, mkoani humo.Meneja wa MSD Kanda ya Iringa Bw. Robert Lugembe akizungumza kwenye mkutano huo.

Wadau wa MSD wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Wadau wa MSD wakiwa kwenye mkutano huo.
Picha ya pamoja na viongozi.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali. Ahmed Abbas Ahmed  akiwakabidhi vyeti wadau wa MSD kwa kutambua mchango wao.
Picha ya pamoja na viongozi waliohudhuria mkutano huo.
Vyeti vikiendelea kutolewa.
Vyeti vikiendelea kukabidhiwa kwa wadau wa MSD.
Vyeti vikiendelea kukabidhiwa kwa wadau wa MSD.

Thursday, April 4, 2024

WANANCHI ITIGI WAMSHUKURU RAIS , KITUO CHA AFYA KUANZA UPASUAJI

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida, Hussein Simba, akizungumza wakati akiongoza kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Aprili 3, 2024. Kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ayubu Kambi na na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Jonathan Hemed.

..................................

Na Mwandishi Wetu, Itigi

WANANCHI wa Kata ya Rungwa iliyopo wilayani Itigi mkoani Singida wamemshuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea Kituo cha Afya ambapo sasa wajawazito wameanza kupata huduma ya upasuaji na kuondokana na changamoto waliokuwa nayo ya kufuata huduma hiyo Hospitali ya St. Gasper iliyopo Itigi.

Diwani wa Kata hiyo Said Sudi akitoa shukurani hizo kwa niaba ya wananchi wake wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichoketi Aprili 3, 2024 alisema hawana cha kumlipa Rais Samia zaidi ya kumpa kura zote katika uchanguzi mkuuu utakaofanyika mwakani.

"Kata yetu tutampa kura asilimia 100 mama yetu kwa kazi kubwa aliyotufanyia si kwa kituo cha afya pekee bali na miradi mingine mingi iliyotekelezwa. wajawazito walikuwa wakilazimika kusafiri umbali wa kilometa 194 pale walipohitaji kupata huduma ya upasuaji lakini sasa wanaipata hapahapa nyumbani ni jambo la kumshuruku sana Mungu kupitia Rais wetu," alisema Sudi.

Sudi alisema Rais Samia aliwapa Sh. Milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha afya ambacho kimeanza kutoa huduma hiyo Februari 27, 2024 ambapo wajawazito watano wamenufaika na huduma.

Alisema wajawazito walionufaika na huduma hiyo ni kutoka vitongoji vya Mkora A na B  na kata za jirani za Kiloli na Kambikatoto.

Sudi alitumia nafasi hiyo kuomba wasaidiwe kupata gari la kubebea wagonjwa, mashine ya kufulia na kunyoshea nguo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Hussein Simba alisema ukusanyaji wa mapato katika halmashauri hiyo upo vizuri hadi kufikia mwezi februari walikuwa wamefikia asilimia 95 ya mapato ya Serikali mapato huru na mapato lindwa ilikuwa  ni asilimia 35 na kuwa wanaamini kwa kasi hiyo hadi mwezi machi ambao bado hawajaujadili watafikia asilimia 100.

Simba alisema kupitia fedha za Serikali kuu na wahisani wamefikia asilimia 77 ya lengo ambapo zaidi ya Sh.Bilioni 4.9 halmashauri hiyo imekwishapewa ili kukamilisha miradi mbalimbali na kuwa asilimia iliyobaki ni ndogo ambapo amewahimiza madiwani kuisimamia miradi hiyo kwa kufanya kazi kwa vitendo zaidi badala ya maneno ili kufikia malengo ya wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Kemirembe Lwota, aliomba miradi yote inayotekelezwa ikikamilike ifikapo  Aprili 30, 2024 ambapo pia aliwaomba madiwani kuhimiza kampeni ya kupata madawati kufuatia kuwepo kwa changamoto ya kukosekana kwa  madawati katika shule zote wilayani humo.

Aidha, Lwota alihimiza mazao yote kuuzwa kwa njia ya stakabadhi gharani badala ya kuuzwa kiholela jambo linalosababisha Serikali kukosa mapato ambapo utaratibu wa kuyauza mazo hayo unafanyika.

Katika hatua nyingine Lwota amewataka madiwani hao na watumishi wengine katika wilaya hiyo kuanza maandalizi ya mbio za Mwenge wa Uhuru ambao unatarajiwa kuanza kukimbizwa wilayani humo mwanzoni mwa mwezi wa Julai, 2024.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Manyoni, Jumanne Ismail alishukuru mshikamano uliopo baina ya chama na Serikali ambao unaendelea kuifanya halmashauri hiyo kusonga mbele.

Ismail alisema Aprili 15, 2024 wanatarajia kuanza kufanya mikutano ya hadhara katika kata zote wakianzia wilayani Manyoni na kisha Itigi na lengo la mikutano hiyo ni kuzungumza na wananchi kuhusu miradi yote iliyotekelezwa katika maeneo yao na Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa CCM.

Katika kikao hicho cha baraza la madiwani ambacho kilikuwa na ajenda nane Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Hussein Simba aliweza kumkaribisha Mkurugenzi mpya wa halmashauri hiyo, Ayubu Kambi na kutoa taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa lengo la kumpa picha halisi ya miradi hiyo ili aielewe na atakapoanza kazi ajue pa kuanzia.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Ayubu Kambi akizungumza.
Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Kemirembe Lwota akizungumza.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Manyoni, Jumanne Ismail, akizungumza.
Katibu wa CCM Wilaya ya Manyoni Maimuna Likunguni, akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Mchumi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Emmanuel Dyilu, akizungumza kwenye kikao hicho.
Mratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAFU)  wa wilaya hiyo, Valence Kilasara akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya wafufaika wa mfuko huo.
Diwani wa Viti Maalumu, Elizabeth Kidolezi akiomba ukamilishwaji wa mabweni kwa wanafunzi wa Sekondari wa Kata ya Rungwa.
Diwani wa Kata ya Mgandu, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Martin Kapona,akisoma taarifa katika baraza hilo.
Diwani wa Kata ya Sanjaranda, Nikodemas Nkuwi, akizungumzia wanaufaika wa TASAFU na changamoto ya Tembo wanaokula mazao ya watu ambapo ameomba msaada wa kumaliza changamoto hiyo. 
Diwani wa Kata ya Rungwa, Said Sudi akitoa shukurani zake baada ya kata yake kujengewa kituo cha afya ambacho Februari  mwaka huu kimeanza kutoa huduma za upasuaji kwa wajawazito.
Mwenyekiti wa Wanawake wa Samia Mkoa wa Singida, Asha Mohamed Mwandala akiutambulisha umoja huo katika kikao hicho.
Waratibu wa vikao wa Halmashauri hiyo wakiwa kazini. Kushoto ni  Makandaiga Magabe na Constantine Mihambo.

Naibu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Jonathan Hemed, akitoa taarifa za kamati katika kikao hicho.
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Manyoni wakiwa kwenye kikao hicho.
Diwani wa Viti Maalumu, Utukufu Gwimile (kushoto) akiwa na madiwani wenzake katika kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Baadhi ya wakuu wa Taasisi za Umma wa Wilaya ya Manyoni na Itigi na wakuu wa idara wa Wilaya ya  Itigi wakiwa kwenye kikao hicho.
Wakuu wa idara wakiwa kwenye kikao hicho.
Wanachama wa Wanawake na Samia Mkoa wa Singida wakiwa kwenye kikao hicho.
Taswira ya kikao hicho.
Viongozi wa Halmashauri hiyo wakiwa meza kuu wakati wa kikao hicho.
Kikao kikiendelea. Kutoka kushoto ni Diwani wa Viti Maalumu, Amina Msita, Diwani wa Kata ya Mgandu, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Martin Kapona, Diwani wa Viti Maalumu, Utukufu Gwimile na Diwani wa Viti Maalumu, Elizabeth Kidolezi.
 

Friday, March 22, 2024

WADAU WA MSD WAHIMIZWA KUSIMAMIA MATUMIZI SAHIHI YA TAKWIMU BIDHAA ZA AFYA

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni,  akifungua kikao cha wadau na wateja wa Bohari ya Dawa (MSD),  Kanda ya Mtwara Machi 22, 2024.

...........................

Na Mwandishi Wetu, Mtwara

WADAU wa Afya wa Bohari ya Dawa  (MSD) Kanda ya  Mtwara wamehimizwa kusimamia matumizi sahihi ya takwimu za mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya, ili ziwawezeshe kufanya maamuzi sahihi juu ya bidhaa hizo katika maeneo yao.

Akifungua kikao cha wadau na wateja wa MSD kanda ya Mtwara, Mkuu wa Wilaya ya Masasi Lauteri Kanoni amesema uwepo wa takwimu sahihi unaiwezesha MSD kuagiza kwa usahihi bidhaa za afya na kuboresha upatikanaji wa bidhaa hizo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, amewashauri MSD kuhakikisha utaratibu wa vikao  vya mwaka vya wadau ni muhimu kwa pande zote mbili, yaani Bohari ya Dawa (MSD) yenyewe na wadau ili kwa pamoja kuboresha upatikanaji wa bidhaa za afya, kwa kujadili changamoto na kuzitafutia utatuzi.

Kwa upande wake Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay ameeleza kuwa kwa sasa kanda ya MSD Mtwara inahudumia vituo vya kutolea huduma za afya 631, na inasambaza bidhaa za afya kila baada miezi miwili.

Naye Meneja Huduma kwa Wateja na Miradi Dkt. Pamella Sawa ameeleza kuwa vikao vya MSD na wadau wake kuanzia sasa vitakuwa endelevu kila mwaka.

MSD Kanda ya Mtwara inahudumia mikoa ya Lindi,Mtwara na Wilaya ya Tunduru.Meneja wa MSD Kanda ya Mtwara Tea Malay, akizungumza kwenye kikao hicho

Wadau wa MSD wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Wadau wa MSD Kanda ya Mtwara wakifuatilia mada kwenye kikao hicho.
Taswira ya kikao hicho.
 

Saturday, March 16, 2024

MAAFISA WATENDAJI WATAKIWA AJENDA YAO KUWA ANWANI ZA MAKAZI, KUHAKIKI TAARIFA ZA WANANCHI

Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Innocent Jacob akizungumza wakati wa siku ya pili ya mafunzo ya siku 14 kwa watendaji wa kata, mitaa, wenyeviti wa Serikali za mitaa na vijiji yanayohusu namna ya kukusanya taarifa za Anwani za Makazi  Manispaa ya Singida.

.........................

Na Dotto Mwaibale, (Singidani Blog)

MAAFISA Watendaji wa Mitaa kote nchini wametakiwa katika vikao vyao vyote vya msingi ajenda yao kubwa iwe ni anwani za makazi pamoja na uhakiki wa taarifa za wananchi.

Ombi hilo limetolewa Machi 15, 2024 na Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Innocent Jacob wakati wa siku ya pili ya mafunzo ya siku 14 kwa watendaji wa kata, mitaa, wenyeviti wa Serikali za mitaa na vijiji yanayohusu namna ya kukusanya taarifa za Anwani za Makazi Manispaa ya Singida yaliyoanza Machi 14, 2024 ambayo yameandaliwa na wizara hiyo kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na kuwa siku mbili kati ya hizo 14 zitatumika kwa ajili ya kuhakiki taarifa.  .

Jacob alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwawzesha wenyeviti hao ili waweze kutoa taarifa kwa wanananchi za zoezi hilo ndani ya siku hizo na wananchi nao waweze kutoa za kwao kama NIDA, namba ya simu, Tin namba ya biashara na taarifa nyingine za majengo, makazi kama walivyoelekezwa watendaji wa mitaa jinsi ya kulifanya zoezi hilo.

"Watendaji wa mitaa ndio watakao kwenda kukusanya taarifa hizi kwa wakazi wao kwa sababu katika maeneo yote ya utawala wao ndio wahusika wakubwa na watashirikiana na wenyeviti wa mitaa kufanya kazi hiyo," alisema Jacob.

Alisema Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), kwa kushirikiana na TAMISEMI, wameandaa zoezi hilo kwa lengo la kuhakiki taarifa za makazi kwa awamu ya pili baada ya awali kufanyika kwa njia ya operesheni ambapo huenda kuna baadhi ya wakazi hawakuweza kupata fursa ya kuingia katika kanzidata ya Anwani za Makazi.

Alitaja baadhi ya vitu ambavyo viliweza kusahulika kuwekwa kwenye kanzidata kuwa ni taarifa ya majengo, viwanja, majina katika vibao vya mitaa hivyo kurudiwa tena katika zoezi hilo la awamu ya pili la uhakiki.

Jacob alisema umuhimu wa Anwani za Makazi zitarahisisha utambuzi kwa wakazi wa eneo husika na kuweza kupata huduma mbalimbali kwa kufikiwa kiurahisi mahala walipo kwa kutumia programu tumizi kwa ajili ya umma inayoitwa NAPA ambayo inapakuliwa kupitia simu janja ambapo wananchi wote hapa nchini wakiwemo wa Manispaa ya Singida wataweza kuingia katika mfumo huo kwa kuandika NAPA Tanzania.

Alisema mafunzo hayo yanafanyika Manispaa ya Kigoma, Iringa na Singida na yatakuwa endelevu kwa kufanyika katika mikoa mingine.

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Dkt. Adrianus Kalekezi alisema katika mafunzo hayo wataalamu wanaelekeza namna ya kuingiza taarifa katika mfumo wa Anwani za Makazi na kuwa hivi sasa wanauhisha taarifa za awali baada ya kazi hiyo kufanyika awamu ya kwanza.

Dkt. Kalekezi alisema suala hilo la Anwani za Makazi ni la muhimu katika manispaa hiyo kwani wananchi watapata huduma kwa urahisi na alitumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi kuilinda miundombinu ya Anwani za Makazi iliyowekwa kama vibao vinavyoonesha majina ya mitaa na barabara na kueleza kuwa ni lazima ilindwe ili waweze kunufaika na zoezi hilo kwani bila miundombinu hiyo inakuwa vigumu kwao kuelekezwa na kuitambua mitaa na barabara.  

Afisa Mtendaji wa Kata ya Mwankoko, Habiba Juma akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo alisema zoezi hilo litawarahisishia kutoa huduma kwa wananchi na kupunguza gharama ya fedha na muda kutoka sehemu moja kwenda nyingine na wananchi wataweza kupata huduma kupitia anuani za makazi.Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka WHMTH, George Leonard, akitoa mafunzo kwa watendaji hao.Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka WHMTH, Janeth Peter , akiwajibika wakati wa  mafunzo hayo.Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Dkt. Adrianus Kalekezi, akizungumzia zoezi hilo.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Mwankoko, Habiba Juma akizungumzia umuhimu wa mafunzo hayo.
Wataalamu wa mfumo wa Anwani za Makazi wakiwa kwenye mafunzo hayo. Kushoto ni Mtaalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Innocent Jacob na aliyekuwa Katibu wa Kamati ya Ufatiliaji Operesheni Anwani za Makazi Mkoa wa Singida ambaye pia ni Afisa TEHAMA, Athumani Simba. .
Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Manispaa ya Singida, Abdillai Hussein akimshuru Rais Samia kwa kuwezesha mafunzo hayo kupitia wizara hiyo.
Washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
Mafunzo yakiendelea.

Attachments area Preview YouTube video MAAFISA WATENDAJI WATAKIWA AJENDA YAO KUWA ANWANI ZA MAKAZI